Waziri Makamba avunja Kitengo cha Habari na Mawasiliano TANESCO kwa tuhuma za kushindwa kulisemea Shirika

Waziri Makamba avunja Kitengo cha Habari na Mawasiliano TANESCO kwa tuhuma za kushindwa kulisemea Shirika

Waziri wa Nishati Mh Makamba amevunja kitengo cha habari na mawasiliano Tanesco akikituhumu kimeshindwa kulisemea shirika na kulitetea shirika kwenye nyakati ambazo kitengo na watu wake kimetakiwa kufanya hivyo!

Ikumbukwe kitengo cha habari na mawasiliano kinaongozwa na mwana dada Badra Masoud kwa misingi hiyo amekali kuti kavu ...

Maswali ya kujiuliza...
Ni kweli kitengo hichi ndicho tatizo kwenye shirika?
Ni kweli wameshindwa kuitetea tanesco?
View attachment 2095460
Kwa erratic nature ya flow ya umemem kwa sasa nchini, hakuna kitengo chochote cha habari ambacho kingeweza kuhabarisha umma adequately. Umeme unakatika saa nne kamili , unarudi saa nne na dakika saba, unakatika tena baada ya dakika 12 na unarudi ndani ya dakika 3. Sijui wewe kama mtu wa kitengo cha habari unasemaje kuhusu mtiririko huu wa umeme?
 
TATIZO LA TANESCO NI MAKAMBA MWENYEWE NA ANATAKIWA AJIFUNGE KAMBA MWENYEWE.

ASITAFUTE WA KUMUANGUSHIA JUMBA BOVU.

KITENGO CHA HABARI WANGESEMA NINI KILA SIKU WAKATI HAKUNA SABABU ZA KUSEMA?

MWISHO WA UONGO UMEKARIBIA.
Nchi inasimamiwa na kuendeshwa na Rais mstaafu, what do you expect?
 
Huyu toka enzi waziri wa mazingira alikua na blabla nyingi kuhusu mifuko ya plasti sasa hayo hayo ndo yatazugukia tanesco
Makamba anavyodai kitengo kimeshindwa kuitetea Tanesco ana maana gani? anataka kitengo kiwe kinazalisha propaganda au kifanyeje?

Navyojua hao watu wa idara ya habari wanatakiwa kupewa taarifa za majibu ya kero za wateja kutoka kwa wahusika (waziri, naibu wake, katibu mkuu nk) then wao ndio watangaze taarifa hizo kwa umma.

Sasa mfano wananchi wakiulizia ujio wa ile winchi ya tani 26 toka huko ilipoagizwa mbona mpaka leo kimya? Makamba anataka hao jamaa wa kitengo cha habari wajibu kitu gani kama hajawapa majibu?
 
Waziri wa nishati, January Makamba ameagiza kuvunjwa kwa Idara ya Habari na Mawasiliano ya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kwa kushindwa kulisemea shirika hilo

Makamba ametoa agizo hilo leo Jumanne Januari 25, 2022 wakati alipotembelea kituo cha usambazaji umeme kilichopo Njiro jijini Arusha ambapo amesema amevunja idara hiyo kutokana na kushindwa kutimiza majukumu yao ikiwemo kulisemea shirika hilo pamoja na kutoa taarifa kwa wateja wao.

"Sisi kama Serikali hatufurahishwi na malalamiko ya wananchi kuhusu kukatika kwa umeme pamoja na upungufu wa taarifa zitolewazo kwa wateja,"amesema Makamba.

Makamba amesema haiwezekani kumgeuza Waziri wa Nishati kuwa msemaji wa Shirika hilo kila inapotokea changamoto.

Mwananchi
 
Hii habari it's just a distruction...too bad hii habari inapewa uzito mkubwa kuliko habari ya mkataba wa gas consultation na kampuni ya Uingereza uliosainiwa jana.
Wanatupa mambo madogo ya kutukeep bze kujadili ili tunaache makubwa yatupite.
Jana ht aliepewa kazi ya mikataba kabudi hakuwepo kwenye utiaji saini.
 
Taarifa ni muhimu
Kuna kipindi tulikuwa tunapata sms kuwa tarehe fulani saa 3 asubuhi hadi saa 11 jioni hakutakuwa na umeme, kuna matengenezo
Siku hizi taarifa wanatoa Twitter
 
Mwandishi wetu,Arusha

Waziri wa nishati ,January Makamba ameagiza kuondolewa Mara moja afisa habari wa shirika la umeme nchini(Tanesco) huku akiagiza kuvunjwa kwa idara ya uhusiano wa shirika hilo na kuwekwa watu wapya.

Mbali na agizo hilo pia amegiza hatua za haraka zichukuliwe kwa watendaji ambao ni wazembe ndani ya shirika hilo ikiwa ni pamoja na kuwawajibisha.

Waziri Makamba ametoa maagizo hayo Leo wakati alipotembelea kituo cha kupoza umeme cha mkoani Arusha kilichopo Njiro jijini hapa na kukagua hali ya upatikanaji wa umeme mkoani hapa kufuatia malalamiko ya wananchi kuhusu kukatika kwa umeme Mara kwa Mara.

Akizungumza na wanahabari Mara baada ya kukamilisha ziara hiyo Makamba alisema kwamba ifikapo Febuari mosi mwaka huu ateuliwe msemaji mpya wa shirika hilo.

"Ninaelekeza msemaji abadilishwe ifikapo febuari mosi mwaka huu achaguliwe mpya " alisema Makamba

Waziri Makamba alisema kwamba kumekuwa na changamoto kwa Tanesco kuwasiliana na wateja wake pindi umeme unapokatika ghafla hali ambayo imekuwa ikipelekea malalamiko mengi na lawama kwa serikali.

"Tanesco lazima iwasiliane na wateja wake kwa wakati hii ni changamoto umeme unapokatika hivyo ni lazima wawasiliane na wateja wao kwa wakati" alisema Makamba

Hatahivyo,alisisitiza kuwa idara nzima ya uhusiano ndani ya shirika hilo lazima ivunjwe na wawekwe watu wapya wanaoweza kuendana na kasi na uweledi ndani ya shirika hilo.

"Mnawasikia wasemaji wa vilabu vya soka vya Simba na Yanga hivi mmeshamsikia msemaji wa Tanesco?" Alihoji Makamba

Hatahivyo,Makamba alisema kuwa serikali haifurahishwi na hali ya kukatika kwa umeme Mara kwa Mara na kuitaka Tanesco kutojificha nyuma ya mgongo wa waziri.

"Hatutaki waziri wa nishati ageuke kuwa msemaji wa shirika tumewaambia menejimenti wasijifiche nyuma ya wizara " alisisitiza Makamba

Waziri Makamba alisema kuwa serikali inakusudia kubadilisha mfumo teknolojia wa Luku ndani ya miezi 18 kuanzia sasa ambapo wateja watakuwa wakinunua umeme moja kwa moja kupitia simu zao za mkononi na kisha kupata umeme bila kuweka tokeni.

"Mtu ananunua umeme kupitia simu yake ya mkononi na unaingia moja kwa moja kwenye mfumo na sio kuchukua tokeni na kwenda kuingiza kwenye mita" alisema Makamba

Alisema kwamba ifikapo mwezi Juni mwaka huu wateja wote takribani elfu 80 wanaosubiria kuunganishiwa umeme wataunganishiwa umeme huku akibainisha kuwa serikali inatarajia kubadilisha mfumo wa maombi ya umeme ambapo utakuwa kupitia mtandao.

Waziri Makamba alibainisha kwamba serikali inakusudia kubadili mfumo wa usambazaji wa umeme kote nchini ili uendane na kasi ya ongezeko la wateja kwa kuwa mfumo uliopo kwa sasa ni wa kizamani.

Mwisho.

View attachment 2095358View attachment 2095359View attachment 2095360View attachment 2095361View attachment 2095362
Hasemi Arusha alifata nn anakimbilia kwenye wasemaji
 
Taarifa ni muhimu
Kuna kipindi tulikuwa tunapata sms kuwa tarehe fulani saa 3 asubuhi hadi saa 11 jioni hakutakuwa na umeme, kuna matengenezo
Siku hizi taarifa wanatoa Twitter
labda kule twita kuna wadau wao wa nguvu, sisi wengine wakina kabwela kajamba nani, taarifa wanaona hazina umuhimu kwetu.
 
Kunja kitengo cha habari/mawasiliano pekeake sijaona/si suruhisho sahihi
Kwasababu wanaokata umeme ni wengne huenda hawatoi taarfa katka kitengo cha habar

Ilitakiwa kutatuliwa tatizo la kukatika kwa umeme hapa mkurugenz mtendaji wa tanesco wa manispaa husika alitakiwa kuwajibishwa

Pia waziri kurizishwa na utolewaji wa taarfa za kukatika kwa umeme sio sahihi
Ni sawa na kuacha tatizo la kukatika umeme liendelee ni sawa na kuhalalisha ukatikaji wa umeme


Mkurugenz wa umeme awajibishwe kwenye hili la umeme
 
Kwa hiyo Badra Masoud anahamishiwa kwenye kubeba mistimu ya umeme sio
 
Mwandishi wetu, Arusha

Waziri wa Nishati, January Makamba ameagiza kuondolewa Mara moja Afisa Habari wa Shirika la Umeme nchini (Tanesco) huku akiagiza kuvunjwa kwa idara ya uhusiano wa shirika hilo na kuwekwa watu wapya.

Mbali na agizo hilo pia amegiza hatua za haraka zichukuliwe kwa watendaji ambao ni wazembe ndani ya shirika hilo ikiwa ni pamoja na kuwawajibisha.

Waziri Makamba ametoa maagizo hayo leo wakati alipotembelea kituo cha kupoza umeme cha mkoani Arusha kilichopo Njiro jijini hapa na kukagua hali ya upatikanaji wa umeme mkoani hapa kufuatia malalamiko ya wananchi kuhusu kukatika kwa umeme Mara kwa Mara.

Akizungumza na wanahabari Mara baada ya kukamilisha ziara hiyo Makamba alisema kwamba ifikapo Febuari mosi mwaka huu ateuliwe msemaji mpya wa shirika hilo.

"Ninaelekeza msemaji abadilishwe ifikapo febuari mosi mwaka huu achaguliwe mpya" alisema Makamba

Waziri Makamba alisema kwamba kumekuwa na changamoto kwa Tanesco kuwasiliana na wateja wake pindi umeme unapokatika ghafla hali ambayo imekuwa ikipelekea malalamiko mengi na lawama kwa serikali.

"Tanesco lazima iwasiliane na wateja wake kwa wakati hii ni changamoto umeme unapokatika hivyo ni lazima wawasiliane na wateja wao kwa wakati" alisema Makamba

Hatahivyo,alisisitiza kuwa idara nzima ya uhusiano ndani ya shirika hilo lazima ivunjwe na wawekwe watu wapya wanaoweza kuendana na kasi na uweledi ndani ya shirika hilo.

"Mnawasikia wasemaji wa vilabu vya soka vya Simba na Yanga hivi mmeshamsikia msemaji wa Tanesco?" Alihoji Makamba

Hatahivyo,Makamba alisema kuwa serikali haifurahishwi na hali ya kukatika kwa umeme Mara kwa Mara na kuitaka Tanesco kutojificha nyuma ya mgongo wa waziri.

"Hatutaki waziri wa nishati ageuke kuwa msemaji wa shirika tumewaambia menejimenti wasijifiche nyuma ya wizara" alisisitiza Makamba

Waziri Makamba alisema kuwa serikali inakusudia kubadilisha mfumo teknolojia wa Luku ndani ya miezi 18 kuanzia sasa ambapo wateja watakuwa wakinunua umeme moja kwa moja kupitia simu zao za mkononi na kisha kupata umeme bila kuweka tokeni.

"Mtu ananunua umeme kupitia simu yake ya mkononi na unaingia moja kwa moja kwenye mfumo na sio kuchukua tokeni na kwenda kuingiza kwenye mita" alisema Makamba

Alisema kwamba ifikapo mwezi Juni mwaka huu wateja wote takribani elfu 80 wanaosubiria kuunganishiwa umeme wataunganishiwa umeme huku akibainisha kuwa serikali inatarajia kubadilisha mfumo wa maombi ya umeme ambapo utakuwa kupitia mtandao.

Waziri Makamba alibainisha kwamba serikali inakusudia kubadili mfumo wa usambazaji wa umeme kote nchini ili uendane na kasi ya ongezeko la wateja kwa kuwa mfumo uliopo kwa sasa ni wa kizamani.

Mwisho.

View attachment 2095358View attachment 2095359
Wapatie watu vifaa mkuu sio unapanga kwa maneno tu., sasa umeme unakatika mara kwa mara unategemea ni maneno mdomoni tu, mwaga nguzi za umeme kila kata kila kijiji mamashine tuone kama kweli mnataka mitano tena
 
Badra masoud wa wapi wewe, si kila kitu u akurupuka tu. Google hapo afisa habari wa tanesco
Si umtaje tu maana nimesoma mwananchi wamemtaja huyo dada, Kama unamjua unasema tu sio iwe ishu sana
 
Back
Top Bottom