Siku hizi binti akiwa pisi kali anaruka na lecturers tu analamba GPA kali, kijana akiwa yupo kwenye circle ya huyo binti (wanafanya discussion pamoja ya mapepa anayovujishiwa) nae anakula GPA kali. Wakienda kwenye practical makazini wanaanza upya. Ufanisi hauendani na GPA.
Wale wenzangu na mie shule za kuunga unga msuli tembo marks sisimizi, wakikaza zaidi wanakula 4.0 kushuka chini.
Nimekumbuka mwaka wa pili chuoni kuna lecturer pisi kali haswa tuliletewa kala GPA 4.7 aje atufundishe parasitology, cha ajabu hata kudadavua lifecycle za Plasmodium na Wuchereria bancrofti ilikua changamoto.
Kwahiyo naunga mkono hoja, suala la kuangalia GPA katika kuajili hawa T.A na Lecturers vyuoni lisipewe mkazo sana bali wawe strict na usaili ili wapate cream iliyo bora kuwafundisha vijana wetu huko vyuoni.