Waziri Mkenda hawa walimu walikosea nini hadi wapewe hii adhabu ya kuporwa madawati ya kukalia?

Kibaya zaidi wakiacha kuingia darasani wanafukuzwa kazi na hao wakurugenzi …hivi kweli mwalimu gani atapenda watoto wafaulu?
 
Walimu wanadharauliwa sana sana na wao wanakubali kabisa…..
 
Kama waliweza kumnunulia fomu ya uchaguzi mama inakuwaje washindwe kujinunulia viti vyao, usiwatetee hao, pia wapigwe marufuku kukalia vitabu kwani kutabu hakisomwi kwa makalio kinasomwa kwa macho.
Hao ni wajinga wajinga lakini hawa walimu hawana kosa la kuwafanya waadhibiwe kwa fedheha kabisa ….
 
Walipewa msaada wenye msaada wao wameyachukua wamejifunza kwa semaji haji manara mkigombana unachukua mali zako. wasubirie ya serikali
 
Mimi nawashangaa sana hata hap walimu walipata hata ujasiri wa kuendelea kusahihisha madaftari eti wamekaa juu ya madaftari………. Yani kama ningelikuwa wao nisingeyagusa kabisa hayo madaftari kisa hao so called takataka wa mtaaa….huu ni udhalilishaji wa kiwango chajuu hati wakae kwenye sakafu…

Hao taka taka kwenye ofisi zao za mitaa wana furniture nzuri tuu na kunafungu kabisa….aiseee kwakweli jua ni kali kweli kweli kwa Walimu…
 
Hao walimu nao wameni dissapoint sana kwa woga wa kufukuzwa kazi hii ni aibu…..
 
Duh kuna walimu vilaza,ila mimi sio kilaza,kiti changu kingekuwa cha mwisho kupelekwa kwa wanafunzi baada ya kumung'oa jino mwenyeketi wa bodi/kamati yashule na mtendaji kurudi kwake akiwa na bandeji usoni.


Walimu tujitambue,tuache kuwa wanyonge.
Aisee ni fedheha sana wanafanyiwa..,
 
Hao,wametaka waonekane.
Wanapenda kulialia&kutaka public sympathy.
Sijui ni kwa nini hawajipendi,hivi kweli hata furnitures tu wanashindwa kutengeneza kupitia fedha za elimu bure?
Maafisa wazima na elimu zao,wanafurahia kukalia madawati ya wanafunzi?
Aah...ni ajabu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…