Waziri Mkuu Kassim Majaliwa aagiza zawadi ya cheni aliyopewa mkewe iuzwe ili kujenga bweni la Wanafunzi Simanjiro

naunga mkono hoja, sheria hiyo inaruhusu watumishi wa umma tuu, zawadi hiyo ni kwa mke wa Majaliwa, wake wa viongozi sio watumishi wa umma.
P
 
ni ishu ndogo ila maadili yamembeba hasa kuhusu vijizawadi vya kupewa
 
Nakusahihisha kidogo, inachotakiwa Kama umepewa zawadi kwa xheo chako unapaswa kuiwasilisha kwa mwajiri na Kuna form unajaza kudeclare kwamba umepewa zawadi na sio hongo them ukikamilisha unaichukua hiyo Zawadi Kama yako n utaitumia hata ikiwa pesa.

Cha msingi ni kuonyesha kwamba haujalewa sababu ya influence yeyote Ila wamekuzawadia in good faith.

Sioni sababu ya yeye PM kuirudisha although ni maamuzi yake Ila sio sawa amemkosea mkewe hiyo mkewe ndio angeamua yeye.
 
Ni avyojua taratibu ni kuwa zawadi yeyote anayopewa mtendaji wa umma wakati anawajibika anatakiwa aikabidhi serikali maana sio ya kwake. Kuwaruhusu wazibinafsishe ni kufungulia milango rushwa za waziwazi.

Amandla...
 
Kwenye rasimu ya Warioba,kuna sehemu walisema Rais,Makamu wa Rais na Waziri Mkuu wakipewa zawadi,zinakua Mali za Uma,na zinapelekwa Ikulu! Sasa sijui kama wajuba waliona hili suala kama linawapa shida kidogo
Ndivyo ilivyo hata sasa,

Amandla...
 
Reactions: Ame
Sidhani kama uko sahihi. Ninavyojua kuna kiwango ambacho zawadi ikiwa chini yake unaruhusiwa kukaa nayo baada ya kutoa taarifa. Kiwango hicho ni kidogo sana. Ukiachia wazi hivi, mtu atapewa ndege kama zawadi na tutashindwa la kufanya. Watu wa zamani watakumbuka hadithi zilizoenea kuwa aliyenunua mabasi ya Ikarus alipewa kamoja kama shukrani!
Na huu mtindo wa kuwapa zawadi wake au waume wa viongozi ni yale yale. Wenye nia mbovu watapitia huko ili waku compromise. Zawadi za kuwapa viongozi ni peni ( sio Montblanc n.k.) na mke wake box la chocolate au maua. Mkufu wa Tanzanite ni too much.

Amandla...
 
Kabisa, kama kweli wana nia njema kwanini hawampi tu mtu yeyote wanawapa viongozi tu?
 

Kimaadili, zawaidi yoyote ya thamani (kwa vigezo vilivyowekwa na sheria au code of ethics) anayopewa kiongozi wa umma kwa sababu ya nafasi yake, ni mali ya umma. Kiongozi hapaswi kuifanya hiyo zawadi kuwa mali yake binafsi.
 
Majaliwa for President !

For God’s sake, we need no liars! We wrote this SOB off the very day he brazenly lied to all Tanzanians about the health of the then President of Tanzania, the Late Dr. John Pombe Joseph Magufuli, who died within less than one week of that big lie.

Even the other liar that’s currently holding the presidency should be sent packing as soon as her default presidency expires in 2025!
 
Kama haijabadilishwa tangia enzi za Mwalimu Nyerere, Sheria inasema kuwa, Mtumishi wa Umma, Mke wake au Mtoto wake akipewa zawadi ambayo thamani yake inazidi Shilingi Elfu 50 (Hamsini), zawadi hiyo ni mali ya Umma.
Kitendo cha Waziri Mkuu kuipangia matumizi kinamaanisha kuwa kwanza kabisa ameipokea hiyo zawadi na sasa ameipangia matumizi.
Na huko ni kukiuka Sheria.
Au labda Sheria imebadilika.
 

Kimsingi, ninakubaliana na hoja yako isipokuwa sijaona msingi wa jibu lako kwa yule uliyekuwa unajibu hoja yake!
 
Izo barakoa vp mbn zinavaliwa nusu nusu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…