Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kukutana na kuongea na Vyama vya Siasa Oktoba 21 - 23

Nashauri Chadema wasishiriki kikao na watesi wa viongozi wao...
  • unampora bills unaibomoa
  • mashamba yake unabomoa
  • hoteli yake unaivuruga
  • account ulizifunga
  • kesi nyingi unampa zisizo na maana
  • mara kadhaa unamweka kizuizini
  • unamtuhumu anahusika na madawa
*Sasa unampiga kesi ya ugaidi!!!!!

MTU awafanyie yooote hayo nazaidi alafu unakaa nae muelewane mtaelewana nini hasa??
Hivi gaidi ni mfanya uovu ama mfanyiwa uovu??
Nchi zenye watu conscious wangepinga kila mahali uovu huu...makanisani,misikitini,mitandaoni,kwenye mabasi,kwenye makongamano nk. kiiila mahali, THIS IS VERY UNFAIR!!!
Obama aliwahi kusema vema kwamba
"INJUSTICE TO ONE AMERICAN IS INJUSTICE TO ALL AMERICANS"
Hapa kwetu watu wanafurahia MTU akiteswa na kunyimwa haki zake alimradi wanatofautiana vyama vya siasa! Very stupid ndomana tuliitwaga nyani na ndomana kamanchi hatuendelei tunaishi kiporipori
 
Kwani Waziri mkuu yeye ni Nani kwenye vyama vya siasa? Yeye sio hata mwenyekiti wa chama Sasa anaitisha huo mkutano kama nani? Chadema kaza msiende huo ni mtego baadaye waje kusema tulikubaliana hivi na vile. Chadema na ACT waendelee kukaza until their demands are granted.CCM hawaaminiki baada ya kuona njia ya kumtumia msajili imeshtukiwa wanabuni ya kuja na Waziri mkuu.
 
Waziri Mkuu siye anayepanga nini vyama vya siasa vifanye na nini visifanye. Hayo yote yameshaainishwa ndani ya Katiba. Aache kujibaraguza na kupotezea watu muda wao. Vyama vinavyojitambua havitatia mguu bali vyama UCHWARA vitakuwepo.

Kulikuwa na haja ya kupeleka ujumbe kwenda kumwambia Majaliwa hayo huko na point blank.

Bila kujali nani anatoa mwaliko ni vyema ujumbe taslimu ukawafika.

Angalia bila kesi ya Mbowe yangetokea wapi haya?





Tusikatae miito makamanda.

Kama vipi atimbe kule mwakilishi wetu mtalaamu wa PGO bwana Petro Kibatala ingependeza zaidi.

Penye wengi haliharibiki neno.
 
Ushauri kwa Vyama vya Upinzani KIKAO kiwe na RAIS sio WAZIRI MKUU na pia haya Yafanyike kabla ya Kikao
1.Mh Mbowe Aachiwe Huru bila Masharti
2.Waliokamatwa wote kwa Kesi za Kisiasa Waachiwe
 
Waziri Mkuu kama Majaliwa hana Mamlaka yoyote ya kisheria ya kukutana na vyama vya siasa .

Bila shaka Chadema haitahudhuria jambo hilo

Badala ya kuukataa wito kabisa vipi kama timu ya wawakilishi ingetimba huko kwenda kumpa somo kiungwana tu?

Watalaamu wetu wa PGO akina Petro Kibatala wangeweza kutuwakilisha vyema tu.

Tusikatae miito makamanda.
 

Rais Yuko tayari kukutana na vyama vya siasa sio chadema Peke Yao
 
Kwani huyo mama Hana mdomo mpaka atumie dalali

Hana uhakika bado nini Chadema anataka. Kwa vile haipo cha kuficha kuwaona watu hawa kuwapa yetu ya moyoni haiwezi kuwa fyongo.

Power of attorney anaruhusiwa kumwakilisha yeyote labda jela tu.
 
Ni vituko Sana
 
Mapendekezo yangu ni kuwa mkutano huo uwe ni wa maandalizi ya ahadi ya Rais wa jamhuri ya muungano, kukutana na kuzungumza na vyama vya siasa,ila wale walioonyesha kuto aminiwa nawaliochochea mfarakano na sitofahamu kama Siro, na Mtungi walete wawakilishi wasio tiliwa shaka, ila mawaziri wenye dhamana wasikosekane kuwepo.
 
Huyu ni muongo muongo hana credibility kabisa
 
Sheria za nchi huwa hazijadiliwi na kutekelezwa ipasavyo na kila mmoja wetu!
 
Wapinzani nao ni matatizo sana,yana unakaa kumbembeleza mshindani wako ukae nae mzungumze ili iweije??
Kama matakwa ya vyama vya siasa hazingatiwi ingia uraiani washawishi watu-kama ni watu kufa wave uone Hugo SAMIA hats wabembeleza yeye Kuwait's.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…