Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kumuwakilisha Rais Samia UNGA79

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kumuwakilisha Rais Samia UNGA79

hivi hajawahi kwenda US?
Shuleni kama ulibahatika kuuangalia mchezo wa kuigiza mchezo huo wa kuigiza ukiwa mrefu na matukio marefu na mpangilio maalum mkamuweka na muhusika mkuu, (steering), ambaye akifa anaweza akotokea baadae kwenye mchezo hua huo, huitwa filamu, mfumo huu wa mhusika mkuu aliye kufa akaibuka baadae hutumika kwenye picha za kihindi, (filamu)
 
Naona mnahangaika sana. Vipi maandamano yenu yameishia wapi?
Katika mkutano huo ambao hufanyika kila mwaka, viongozi wa nchi mbalimbali wanatarajiwa kushiriki mijadala tofauti chini ya mada kuu ambayo ni “Hakuna kuachwa nyuma yeyote: Kushirikiana pamoja kuendeleza amani, maendeleo endelevu na heshima ya binadamu kwa vizazi vya sasa na vijavyo" (Leaving no one behind: Acting together for the advancement of peace, sustainable development and human dignity for present and future generations).
Yule 2025 ndio mwisho wake acha uchawa tengeneza future yako.

Kiongozi wa nchi ni Majaliwa ?
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, alitakiwa kuhudhuria kikao cha UN (UNGA) Lakini amemtuma Waziri Mkuu wa JMT MH. Kassim Majaliwa kumuwakilisha.
My take: Tayari Raisi keshaingia hofu kutokana na hotuba yake aliyoitoa juzi kwenye maazimisho ya miaka 60 ya kumbukizi ya Jeshi la Polisi? Maana tunafahamu sote Raisi wetu ni mtu anayependa sana kusafiri.
Kama ameshaanza kumtuma msaidizi wake kwenye majukumu aliyopaswa kihudhuria, Je safari za nchi za Magharibi atakuwa hahudhurii ?
Safari zake zitakuwa ni za South Korea, Turkey, Uarabuni na China……

Nawasilisha

Zaidi soma hapa.
WAZIRI MKUU KUMWAKILISHA RAIS SAMIA UNGA79

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameondoka nchini leo (Alhamisi, Septemba 19, 2024) kwenda Marekani ambako atamwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye Mkutano wa 79 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UNGA79).

Mkutano huo unaotarajiwa kufanyika kuanzia Septemba 20-26, 2024, utafanyika jijini New York, Marekani ambapo masuala ya kiuchumi, biashara, nishati, siasa, mazingira, afya, vijana na watoto yatajadiliwa. Masuala mengine ni ya maji, bahari, athari za hali ya hewa na haki za binadamu.

Katika mkutano huo ambao hufanyika kila mwaka, viongozi wa nchi mbalimbali wanatarajiwa kushiriki mijadala tofauti chini ya mada kuu ambayo ni “Hakuna kuachwa nyuma yeyote: Kushirikiana pamoja kuendeleza amani, maendeleo endelevu na heshima ya binadamu kwa vizazi vya sasa na vijavyo" (Leaving no one behind: Acting together for the advancement of peace, sustainable development and human dignity for present and future generations).

Mbali na kukuza diplomasia, ushiriki wa Tanzania kwenye mkutano huo unatoa fursa ya nchi kuwasilisha maslahi yake katika jukwaa la kimataifa, kujifunza kutokana na uzoefu wa nchi nyingine na pia kuwasilisha ajenda na mipango ya maendeleo ya nchi kwa jamii ya kimataifa.

(mwisho)
jambo usilolijua ni kama usiku wa kiza 🐒
 
Na wakina Mange walikuwa wanaenda kumletea noma kama angekanyaga 🤣🤣🤣
Sasa atawakacha mpaka lini? Si bora aende wakayamalize huko huko. Sisi wananchi tunahitaji huduma na lazima aende kutuhemea sisi watoto wake, la sivyo tutakufa kwa njaa. Nakumbuka kipindi cha njaa ya mwaka 1984 shuleni tuliletewa Unga ule wa Njano ( yellow) toka USA. Mchonga alienda kule akaomba huo unga akisema anawaletea mifugo yake huku, maana angesema ni chakula cha kulisha watu wake asingepewa. Chakula hcho kweli kilituvusha kpindi hicho kigumu hapa kwetu. So angalia umuhimu na ukubwa wa Uncle Sam ulivyo.
 
jambo usilolijua ni kama usiku wa kiza 🐒

Katika mkutano huo ambao hufanyika kila mwaka, viongozi wa nchi mbalimbali wanatarajiwa kushiriki mijadala tofauti chini ya mada kuu ambayo ni “Hakuna kuachwa nyuma yeyote: Kushirikiana pamoja kuendeleza amani, maendeleo endelevu na heshima ya binadamu kwa vizazi vya sasa na vijavyo" (Leaving no one behind: Acting together for the advancement of peace, sustainable development and human dignity for present and future generations).

Mbali na kukuza diplomasia, ushiriki wa Tanzania kwenye mkutano huo unatoa fursa ya nchi kuwasilisha maslahi yake katika jukwaa la kimataifa, kujifunza kutokana na uzoefu wa nchi nyingine na pia kuwasilisha ajenda na mipango ya maendeleo ya nchi kwa jamii ya kimataifa.
 
..ule upumbavu wake alitakiwa akauseme ktk mkutano wa unga.
Huyu mama tangu anaingia madarakani nilimuunga mkono sana, alionekana ni mwanamke mpole, mwenye hekima busara na upendo.

Nililaani sana kwa mfano, kitendo cha kijana wa tukuyu kuchoma picha yake.

Lakini kwa mshtuko mkubwa, nashangaa kuona anafanya mambo ambayo sikutarajia kabisa.
 
Katika mkutano huo ambao hufanyika kila mwaka, viongozi wa nchi mbalimbali wanatarajiwa kushiriki mijadala tofauti chini ya mada kuu ambayo ni “Hakuna kuachwa nyuma yeyote: Kushirikiana pamoja kuendeleza amani, maendeleo endelevu na heshima ya binadamu kwa vizazi vya sasa na vijavyo" (Leaving no one behind: Acting together for the advancement of peace, sustainable development and human dignity for present and future generations).

Mbali na kukuza diplomasia, ushiriki wa Tanzania kwenye mkutano huo unatoa fursa ya nchi kuwasilisha maslahi yake katika jukwaa la kimataifa, kujifunza kutokana na uzoefu wa nchi nyingine na pia kuwasilisha ajenda na mipango ya maendeleo ya nchi kwa jamii ya kimataifa.
UGA hata wanamapinduzi walopigwa stop AU kama vile Capt. Ibrahim Troure Traore, Capt. Dumboya n.k wanazama US bila mbambamba yoyote kama akina mugabe tu wakiamua 🐒

hakuna ushirikiana wala miujiza.
TANZANIA inahitajika mno duniani kuliko dunia inavyohitajika Tanzania 🐒
 
Huyu mama tangu anaingia madarakani nilimuunga mkono sana, alionekana ni mwanamke mpole, mwenye hekima busara na upendo.

Nililaani sana kwa mfano, kitendo cha kijana wa tukuyu kuchoma picha yake.

Lakini kwa mshtuko mkubwa, nashangaa kuona anafanya mambo ambayo sikutarajia kabisa.

..Mange Kimambi anasema ni wa jinsia mseto.
 
Anavyopenda safari mbona amagwaya ?
sio kupenda,
anahitajika mno katika Jumuiya ya Kimataifa, na kwakweli dunia inamtegemea sana hasa maeneo yenye mkwamo au changamoto za uchumi na ndio maana makongamano mengi sana duniani yanaahirishwa Dr.Samia Suluhu Hassan akitoa udhuru, kumsubiri awepo 🐒
 
Mbona alishamtuma mara nyingi
Heko PM, Kufa kufaana. Yeye angepata lini hiyo Trip
,sio mara ya kwanza kiongozi yeyote kumuwakilisha Mh Rais Samia ,
20240621_173534.jpg
 
Akili za kuambiwa Changanya na Za kwako, ailijiisemea mzee wa Musgoa. Alikuwa sahihi kabisa. Huyu baba alikuwa ni mtaalamu wa Siasa, Sijui kwa nini hawamtumii vizuri mambo yakaenda murwa pasipo purukushani, Ila na yeye alitukwamisha kwenye suala la Ktiba Mpya. Nia na dhamira alikuwa nayo ila alizidiwa nguvu na genge la akina Lowasa waliongoza kampeni za ndani ya CMM kuikwamisha na kuichakachua, Lowasa akiaamini itampunguzia madaraka akishakuwa Rais wa JMT maana alljiaminisha 100% kwamba he is next after JK, hesbau zikaenda mrama. Kwa hilo Mzee wa MVI sisi watanzania hatutamsamehe lakini pia na JK alikisoa msimamo akayaumbishwa na akina Ben akangatuka kabla yakutupatia Katiba Mpya aliyokuwa ametuahidi. Jiwe akaja na agenda zake akidai hiyo haikuwemo katika ahadi zake kwa wapiga Kura. Labda tuweke matumaini kwa huyu naye, ingawa kauli zake za wakati anaanza ni tofauti na sasa kuhusu suala hilo hilo. Ama kweli wanasiasa ni kama Chameleon . Tofauti na hapo mpaka kwa Mwigulu labda muda wake ukifika hapo 20------???.
 
Back
Top Bottom