Waziri mkuu Majaliwa aagiza hospital ya Uhuru mjini Dodoma iwe imekamilika ndani ya siku 15 ili Rais Magufuli aifungue 09/12/2020

Viongozi Watanzania wajifunze kufanya kazi zao kwa upeo mkubwa, kuna kazi za kufanya usiku na mchana na kumalizika bila kuleta athari kwenye viwango na zingine haiwezekani.

Hivi Viongozi wetu huwa wanashindwa nini kuwa na mipango ya ufuatiliaji makini? Sio lazima kila wanapkwenda wanatoa kauli ili wasitumbuliwe. We need to be more careful. People should know that, when they fail to deliver what was promised there will be consequences.
 
Kuna Viyu vya Kuvilazimisha ili vikamilike kwa haraka, ila siyo kwa Hospitali. Waziri Mkuu Majaliwa asianze Kuchanganyikiwa bado mapema tu hivi.

Ile lugha ya kuwa uwaziri mkuu hauna guarantee, lazima utamfanya afe siku si zake.
 

Hapo suala la viwango halipo tena, bali inatakiwa tarehe 9 desemba sifa ipatikane, na waziri Mkuu cheo chake kibaki salama. Miradi mingi ya awamu hii ya tano ni substandard ili kukidhi political millage. Jaribu kupitia majengo na barabara za awamu hii, majengo mengi yana ufa, na barabara nyingi zina mashimo. Sasa hivi wingi ndio unatakiwa, lakini ubora hauna nafasi. Nadhani baada ya Magufuli kutoka madarakani, serikali itakayoingia itabeba lawama ya ukarabati wa miundombinu iliyo chini ya viwango, huku deni la taifa likiwa limeshika kasi kwenye marejesho.
 
Walazimishe hizo siku kumi na tano kama hawajaenda kuwalaza wagonjwa chini, na dripu mgonjwa anashikiwa na ndugu yake.
 
Waziri mkuu apunguzee wenge afanye kazi yake bila woga

Sasa wakikamilisha kwa siku 15 ikawa chini ya kiwango huku ikiwa imefunguliwa na raisi si itakkuwa fedhea
 

Duh!
Ikamilike katika siku 15 ili izinduliwe na Rais Dec 9? Hadi 2025 au zaidi tutaona vituko vingi zaidi!
 
Acha wehu mataga so mkandarasi alipue tu ujenzi kisa siku 15, likianguka je?
 
Ukiona hivyo ujue hizo ndio terms za mkataba..
 
Wajenge kwa mabanzi ili iishe haraka
 
Hahaha haraka ya nini hospitali hazina dawa vifaa tiba ,wala wataalamu?!
 
Kumbe lengo si kukamilika kwaajili ya matumizi ya umma bali kwaajili ya sifa za kipumbavu
Kwani hospital inafunguliwa kwaajili ya maonyesho au matumizi? Mbona unalalamika sana kama vile imeshafunguliwa na haijafanya kazi?
Sidhani Kufungua hospitali ni sifa ya kipumbavu mkuu
 
Jaribu kupitia majengo na barabara za awamu hii, majengo mengi yana ufa, na barabara nyingi zina mashimo.

Ungetuletea hata mifano kadhaa ingependeza, nimepita katika barabara ya kuelekea Airport kule Mwanza, daraja la furahisha, barabara za Dodoma (barabara bira kabisa kuwahi kutokea), majengo ya hospitali za wilaya kadhaa, majengo ya vituo vya afya kadhaa, majengo ya mahakama mpya kadhaa. Sijakutana na hiyo barabara yenye shimo na jengo nililokuta lina ufa ni hospitali moja ya wilaya ambayo kwa maelezo ni kwamba palitokea tetemeko la ardhi ambalo halizuiliki.
 
Hahaha haraka ya nini hospitali hazina dawa vifaa tiba ,wala wataalamu?!
Subiri ifunguliwe uende kutibiwa halafu ukose dawa, vifaa tiba na wataalamu ndio uje ulalamike basi
Watanzania mmekuaje? Yaani chochote cha maendeleo lazima kiwape hasirašŸ¤”
 
Subiri ifunguliwe uende kutibiwa halafu ukose dawa, vifaa tiba na wataalamu ndio uje ulalamike basi
Watanzania mmekuaje? Yaani chochote cha maendeleo lazima kiwape hasirašŸ¤”
Hahaha zilizopo hazina dawa wala vifaa, sasa hiyo itakuwa na tofauti gani?!

Hospitali gani hiyo wewe, umeiona lakini wameezeka mabati baada ya uzinduzi tu yanaanza kuoza yote.
 
Akili za kukopa kwa lisu hizi
 
halafu ni waziri mkuu Hugo,chamsingi hospitalit izunduliwe na Rais,sio ikamilike kwa ubora
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…