Waziri Mkuu Majaliwa ashangaa kukuta wanafunzi wanakaa chini Mkuranga, atoa wiki mbili madawati yapatikane!

Waziri Mkuu Majaliwa ashangaa kukuta wanafunzi wanakaa chini Mkuranga, atoa wiki mbili madawati yapatikane!

Mtu mzima haitwi muongo hasa.kwa mtu mwenye cheo cha Waziri Mkuu. Atwambie tumpe list ya shule ambazo wanafunzi wanakaa chini tuone kama hazitojaza daftari. Tuwachilie mbali shule zilizokuwa hazina madarasa wansomea chini ya miti. Na zenye madarasa ni vibanda vya udongo. Hiyo kwenye Avatar yangu ni shule iko jimbo la Nape!
Mkuu hii picha ilipigwa awamu ile kwa awamu hii inayojali wanyonge haiwezekani kuwa na shule Kama hii.
Tena yenye majigambo ya kuzidi
 
Mkuu hii picha ilipigwa awamu ile kwa awamu hii inayojali wanyonge haiwezekani kuwa na shule Kama hii.
Tena yenye majigambo ya kuzidi
Na Mkuranga kukaa chini itakuwa basi ni kosa la awamu ijayo!
 
Waziri mkuu mh Majaliwa amefanya ziara ya kushtukiza katika moja ya shule za wilaya ya mkuranga na kukuta wanafunzi wa msingi na sekondari wamekaa chini.

Mh Majaliwa ameshangazwa na hali hiyo na kutu muda wa wiki mbili madawati yapatikane na watoto wote wakae.

Majaliwa amesema wilaya hiyo ina viwanda zaidi ya 70 sasa inakuwaje DC na DED wanashindwa kutumia fedha za CSR kununulia madawati.

Chanzo: ITV habari!

Kwani Serikali ya CCM haijafika au haipo pia huko Mkuranga Mkuu? Sasa kama hapa tu Mkuranga hali ni hiyo je, huko Kyaka Nkunde kutakuwaje?
 
Mkuu mi mwenyewe hili nimelishangaa, tena hapo Mkuranga njia ya kuelekea kusini karibu na Mbagala?😨😨
Nastaajabu ya mengine kununua kwa cash na miti tunayo kibao na wanafunzi bado wanakaa chini. Sijui katika sera za elimu CCM watajipanga waseme nini?🙄🙄
Uzembe mkubwa sana na aibu juu kuanzia mkuu wa shule hadi uongozi wa mkoa
 
Mkuu hii picha ilipigwa awamu ile kwa awamu hii inayojali wanyonge haiwezekani kuwa na shule Kama hii.
Tena yenye majigambo ya kuzidi
Kwa hiyo shule hizi zimekosa madawati wakati wa JPM?
 
Uzembe mkubwa sana na aibu juu kuanzia mkuu wa shule hadi uongozi wa mkoa
Inamaana hakuna ukaguzi unaofanyikaga? Ile sera ya kutengeneza madawati haikukamilika? JKT walitengeneza madawati mengi sana miaka ya 2015/16 je yaligawiwa kiuoendeleo au ndio ilikuwa kiki ya kuingilia madarakani kwa mbwembwe?
Katika swala la elimu serikali imeshindwa, waziri mwenye dhamana anaogopa hata kubuni njia za kuirevamp elimu nchini?!
 
Sio huko tu hata hapa hapa Dar shule ya msingi Mzambarauni iliyopo Jimbo la Ukonga wanafunzi wanakaa chini.
Achana na ujinga wa watanzania kutumiwa na wanasiasa wachumia tumbo. Imagine Mbunge wa Mkuranga ndani ya miaka mitano hajaweza kujua ktk jimbo lake shule hakuna madawati na wanafunzi wanakaa chini. Miezi miwili kabla ya uchaguzi mkuu huku akipigania kupita bila kupingwa anakuja kustuka na kutoa agizo na wananchi wanamshngilia. Aisee.

cc johnthebaptist
 
Kufanya kazi kwa kiki ndio huku sasa!Amefanya ziara hiyo huku akijua hakuna madawati,!Sio kwamba ni bahati mbaya!Ningemwona wa maana kama angesema apewe list ya shule nchi nzima wanakokaa chini!Haya ni maigizo
Yeye ni mbunge wa jimbo hilo, miaka yote 5 hajawahi kuhangaika na tatizo hilo leo ndo ang'ake? Ingekuwa wananchi wenye akili nzuri wngefanya maamuzi mazito ya kumpiga chini mbunge wao ili atie akili.
 
Waziri mkuu mh Majaliwa amefanya ziara ya kushtukiza katika moja ya shule za wilaya ya mkuranga na kukuta wanafunzi wa msingi na sekondari wamekaa chini.

Mh Majaliwa ameshangazwa na hali hiyo na kutu muda wa wiki mbili madawati yapatikane na watoto wote wakae.

Majaliwa amesema wilaya hiyo ina viwanda zaidi ya 70 sasa inakuwaje DC na DED wanashindwa kutumia fedha za CSR kununulia madawati.

Chanzo: ITV habari!
Viwanda vingapi??? Definition ya kiwanda ilishabadilishwa???
 
Sio huko tu hata hapa hapa Dar shule ya msingi Mzambarauni iliyopo Jimbo la Ukonga wanafunzi wanakaa chini.
Hivi zile porojo za kapeni za kutengeneza madawati 95 sijui 99 % ziliishia wapi...!? Au ndiyo kusema madawati yameshavujika ndani ya miaka 5... Tatizo la mambo ya awamu hii mengi hayako sustainable ni kama wanafanya kwa show flani .... ikipita wanasahau!!
 
Mkuu mi mwenyewe hili nimelishangaa, tena hapo Mkuranga njia ya kuelekea kusini karibu na Mbagala?[emoji32][emoji32]
Nastaajabu ya mengine kununua kwa cash na miti tunayo kibao na wanafunzi bado wanakaa chini. Sijui katika sera za elimu CCM watajipanga waseme nini?[emoji849][emoji849]
SASA kama hapo mkuranga tuu hali ipo hivyo akija huku Jitombashisho shinyanga vijijini si atajinyanga huyu majaliwa???
 
Waziri mkuu mh Majaliwa amefanya ziara ya kushtukiza katika moja ya shule za wilaya ya mkuranga na kukuta wanafunzi wa msingi na sekondari wamekaa chini.

Mh Majaliwa ameshangazwa na hali hiyo na kutu muda wa wiki mbili madawati yapatikane na watoto wote wakae.

Majaliwa amesema wilaya hiyo ina viwanda zaidi ya 70 sasa inakuwaje DC na DED wanashindwa kutumia fedha za CSR kununulia madawati.

Chanzo: ITV habari!
pesa walinunua ndege
 
Back
Top Bottom