Waziri Mkuu Majaliwa ashangaa kukuta wanafunzi wanakaa chini Mkuranga, atoa wiki mbili madawati yapatikane!



Nashukuru sana.. 😊 mimi sipo serikalini wala kwa chama chochote.. ila namufatilia Magufuli.. tangu zamani alivyo kikazi..
naona ipo vizuri.. vizuri kuwaita.. wamuone wenyewe.. naamini iliwanyanyua kiutendaji wale wanaojua nini kinatakiwa kwa kazi zao.. migogoro ya viongozi hao.. kama ipo sana.. inakuwa sehemu ya wengi.. kutotambulika kiurahisi wale wasio na uwezo wa kazi walizopewa.. na mfano wa mashule hayo kukosa madawati.. mwalimu mkuu.. afisa elimu etc.. yaani wao inakuwaje.. hawajui kuripoti au wakishindwa kwa wa juu yao.. je wana mwingine juu ya wote kuwataarifu.. muhimu wajuwe waatweza kosa kazi.. wasaini mengine mapya.. yaongezwe na survey ifanyike kujua mengi.. wawe anonymous waweke labda wilaya na mkoa au vyote..
 
Wanajifanya hawajui? Sehemu nyingi tuu madawati hayatoshi, Kuna baadhi ya wilaya wanatoa taarifa za uongo kuwa wanamadawati mpaka ya akiba wakati Hali ni mbaya watoto hawana viti, wakurugenzi ma DC wanajua
Sahihi kabisa, wakurugenzi na wakuu wa wilaya wanaficha ukweli wa upungufu wa madawati, hata pale shule inapotembelewa na kiongozi wa juu basi anapelekwa ktk yale madarasa yenye utoshelevu wa madawati huku wakihakikisha kbs hafiki kwenye madarasa yenye upungufu.
 
Mwezi jana meko so alipita hapo akachangia madawati
 
Magufuli na CCM Mpya wameshindwa kuunda mfumo utakao mpa mrejesho mtendaji kata, afisa tarafa, DED, DC na RC kiasi hata watendaji hao hawajui kinachoendelea / mahitaji ktk maeneo yao zaidi ya kujua wapi kuna mkutano wa chama cha upinzani wawatie ndani watu wa upinzani kuwafurahisha kisiasa wakubwa waliopo Dodoma na Dar esSalaam.

Kama kungekuwa na mfumo thabiti masuala ya madawati, shule, hospitali za wilaya, vituo vya afya, barabara za vijijini, mabwawa ya Umwagiliaji, masoko ya mazao n.k vingepatiwa ufumbuzi ngazi hizo za mikoa / wilaya / Halmashauri na siyo kitaifa na waziri Mkuu au Rais.
 
Hongera Mh. waziri mkuu hili zoezi lingefaa liwe nchi nzima DED, mkuu wa wiliya na afisa elimu ambao wanafunzi wao wanakaa chini au kukosa vyoo ni vyema wakatumbuliwa tu maana ni aibu. Tunahitaji viongozo wabunifu na wenye maono ili Taifa lisonge mbele. Haipendezi kabisa Taifa limeingia uchumi wa kati halafu baadhi ya viongozi wanashindwa kufanya mageuzi katika utendaji wao.
 
wangeacha kununua ndege wakatuachia fastjet yetu kila mtoto angekuwa na dawati lake.
Hakuna kitu kinanikera kama ile biashara ya kuunga juhudi,halafu uchaguzi unarudiwa tena. HIZO PESA ZILIKUWA ZINATOSHA KUJENGA MADARASA NA KUTENGENEZA MADAWATI NCHI NZIMA. Kama kituo Cha afya kinagarimu mil 400 tu,ni vyumba vingapi vya MADARASA vingejengwa huko Tabora,Lindi,Simiyu,Mara etc? Namalizia kwa kusema yeyote aliyeshiriki kwenye hiyo biashara kwa namna moja au nyingine, ni mpumbavu yeye na kizazi chake halafu alaaniwe milele na milele.
 
Kumbe kuna wanafunzi wanakaa chini hata baada ya miaka 5 ya majigambo na kelele nyingi za awamu hii?!
Tumejenga Flyover,
Tunajenga SGR,
Tumenunua Ndege
 
Nini madawati shule nyingi hazina walimu
Walimu waliyopo hawana nyumba za kuishi, hawajapadishwa madaraja, hawajapewa nyongeza ya mshahara ya mwaka.
Nao wanatakiwa washangilie midege, maflyover, madaraja ya baharini kutoka Upanga kwenda Masaki.
 
Nini madawati shule nyingi hazina walimu
Walimu waliyopo hawana nyumba za kuishi, hawajapadishwa madaraja, hawajapewa nyongeza ya mshahara ya mwaka.
Nao wanatakiwa washangilie midege, maflyover, madaraja ya baharini kutoka Upanga kwenda Masaki.
 
Teh! Siri kali ya viwanda
 
Kumbe kuna wanafunzi wanakaa chini hata baada ya miaka 5 ya majigambo na kelele nyingi za awamu hii?!

DC & DED lazima wapigwe chini, hiyo kazi ilitakiwa kuisha tokea 2017.. Wenyewe wanakaa tu ofisini.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…