Waziri Mkuu Majaliwa azindua Tume Maalum ya Wajumbe 21 kuchunguza ajali ya Jengo Kariakoo
Kwa mujibu wa maelekezo ya Rais Dkt. Samia, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amezindua Tume maalum ya wajumbe 21 ambao wamebobea kwenye masuala ya ujenzi kuchunguza chanzo cha tukio la ajali ya jengo lililoanguka Kariakoo, pamoja na kufahamu ubora na uimara wa majengo yote yaliyoko Kariakoo. Tukio hilo lilisababisha maafa makubwa, na Tume hiyo imepewa maagizo mazito, huku ikiongozwa na Mkurugenzi wa Idara ya Menejimenti ya Maafa, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge na Uratibu, Brigedia Jenerali Hosea Ndagala.

PIA SOMA: Live Updates Kuporomoka kwa Ghorofa Kariakoo Nov 16: Kamati ya Uchunguzi kuporomoka kwa jengo Kariakoo yazinduliwa Nov 21, 2024
Wanazidi kugawana keki ya taifa,
 
Awamu ya sita inaongoza kuwa na viongozi vichaa.kila siku tume na hakuna majibu.utaundaje tume kuchunguza sababu za kuanguka jengo wakati sababu zinajulikana kabisa za ujenzi holela usiofuata uimara na usalama wa jengo ambapo vibali vya ujenzi vimetolewa na hii serikali yenu isiyofuata tarabibu za ujenzi.mliunda tume kuchunguza mauaji ya mzee kibao lakini Hadi Sasa kimya,mkaunda tume ya kutatua kero za kikodi kariakoo lakini Hadi Sasa kimya,mkaunda tume ya kuchunguza mauaji ya lisu lakini kimya,mkaunda tena tume ya kuchunguza mauaji ya mfanyabiashara wa madini kule mtwara yaliyotekelezwa na polis lakini Hadi Sasa kimya.Hizi tume mnaunda ili kujilipa posho ?
 
Posho ya mjumbe kwa siku haipungui Tshs 500,000 kwa siku ongezea ofisi na usafiri.

Hadi tume inamaliza kazi bil 50 - 100 jambo la kawaida. tunywe mchuzi tusichoke nyama tumezikaribia.
 
NI mwendo wa Tume mpaka kieleweke. Lowasa aliunda Tume kama hii ya kuporomoka ghorofa
Kuna jamaa 10 walikuwa wanasafiri kwa ngalawa..maji yakaanza kuingia ndani ya ngalawa yao - walichofanya wakaunda tume ili ichunguze maji hayo yanaingiaje ingiaje kwa ngakawa yao.
Unaweza kujua nini kiliwasibu baadaye.
 
Hivi hata kuangalia tu kwa macho kunahitaji TUME..., badala ya kuangalia Jengo hili kuanguka wangeangalia kwanini majengo kama haya hatarishi yanaendelea kuongezeka kama Uyoga.

By the way kuna uhitaji wa kuanzisha Tume ya kuangalia Tume zinazoanzishwa kama huwa zina Tija
 
Hivi hata kuangalia tu kwa macho kunahitaji TUME..., badala ya kuangalia Jengo hili kuanguka wangeangalia kwanini majengo kama haya hatarishi yanaendelea kuongezeka kama Uyoga.

By the way kuna uhitaji wa kuanzisha Tume ya kuangalia Tume zinazoanzishwa kama huwa zina Tija
Hakuna haja ya tume, aliyechimba pembeni ndiye aliyesababisha janga. Unganisha na mkandarasi aliyesimamia jengo.

Suala hili linafikirisha, Je, tukio hilo ni hujuma za makusudi ? Tazama hii video kisha toa maoni yako.
 

Attachments

  • 5885669-2da9d10310d2077cab41f4c737a3e62f.mov
    2.4 MB
Kwa mujibu wa maelekezo ya Rais Dkt. Samia, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amezindua Tume maalum ya wajumbe 21 ambao wamebobea kwenye masuala ya ujenzi kuchunguza chanzo cha tukio la ajali ya jengo lililoanguka Kariakoo, pamoja na kufahamu ubora na uimara wa majengo yote yaliyoko Kariakoo. Tukio hilo lilisababisha maafa makubwa, na Tume hiyo imepewa maagizo mazito, huku ikiongozwa na Mkurugenzi wa Idara ya Menejimenti ya Maafa, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge na Uratibu, Brigedia Jenerali Hosea Ndagala.

PIA SOMA: Live Updates Kuporomoka kwa Ghorofa Kariakoo Nov 16: Kamati ya Uchunguzi kuporomoka kwa jengo Kariakoo yazinduliwa Nov 21, 2024
Atoe taarifa ya tume Ile ya mapendekezo ya wafanya biashara Kariakoo kwanza
 
Hamna kitu hapo blah blah
Tushazizoea

Ova
 
Ile Tume iliyoundwa na Waziri mkuu kipindi kile(Edward Lowasa) baada ya ajali ya chang'ombe village inn ripoti yake ilifanyiwa kazi? Vp ripoti ya Ile Tume ya Manispaa ya ilala ?
Ni upuuzi mtupu kuunda tume ya kuchunguza Jambo Kisha ripoti yake haifanyiwi kazi..
Ni matumizi mabaya ya fedha za umma.
Uhuni tu

Ova
 
Back
Top Bottom