Waziri Mkuu Majaliwa, Vijijini hatuhitaji taa za barabarani, hii ni kejeli

Wewe jamaa inaonekana kijijini kwenu hakuna maendeleo... Nenda Moshi na Kagera ujionee maendeleo ya vijijini...Vijijini Kuna centers...Muhimu kuwa na taa... Kwani taa kitu gani??
 
Taa ni lazima popote,barabara kuu zote zinapita kwenye vijiji,mbali mbali.Taa zitakapokuwa zipo kwenye barabara kuu za Vijijini,wananchi watafanya biashara mpaka usiku,gari zinazopita usiku,watanunua bidhaa zao,uchumi wa vijiji utainuka.
Kama igawa na mabadaga kule mbeya
 
Serikali hii ni ya vituko. Technology hivi sasa ipo solar zinaweza kusaidia lakini je, hicho ndio kipaumbele cha Serikali hii? Ningefikiria Serikali ingejikita kutoa social welfare kwa raia wake. Maana kuna watu huko Serikalini wanakula na kusaza wakati wale wanaotakiwa kuangaliwa na wenye mali wanateseka.
 
Kijana dar haina Kijiji

Ila sisi tuliopo bush mpimbwe huku acha tuwekewe mataa
 
Tunataka taa sisi,acha ujuaji.
 
Ni vema sana yaani zikiwekwa.

Lakini je, ni nani atalipa bili za umeme wake?

Ndani ya majiji tu huwa wanazima kuogopa bili...uko kijijini je?
Ni solar hakuna cha bill, acha taa ziwekwe
 
Ukiona zinakukera na umezoea uchawi wa gizani zikifika kijijini kwenu hamia polini zaidi utakua umemkomesha.
 
Mpuzi huyu
 
zikija taa na umeme inawezekana utaletwa Boss,Serikali ya CCM haiwezi kuleta vyote hivo kwa pamoja, Ndalichako jimboni kwake wanakunywa maji yana rangi ya chai ya maziwa
Taa za solar mkuu....
 
Moron, taa ni moja ya miundo mbinu hiyo, wewe huoni mijini ndio kuna street lights??, au wewe hujafika mjini hata siku moja??
Jinga Sana,kwa hiyo kijijini hakutakiwi kuwa na street lights? Ulivyokuwepo mshamba inaonesha hata hujawahi ona popote ndio maana unashangaa..

Vijiji vingi sana vya mkoa wa Rukwa vita taa za solar miaka mingi Sana na ndiko PM kajifunza.
 
Sasa huko vijijini mnaweka katika eneo Gani.Kijiji chote au pale palipochangamka watu wanakunywa ulanzi na komoni.
 
Taa ni sehemu ya maendeleo. Kwa ufupi umeme ukishafika sehemu maisha yanakuwa yameshabadilika. Sidhani kama PM Majaliwa ameongea kwa nia ya dharau.

Anawakumbusha waliopewa dhamana ya nishati kuhakikisha umeme unafika kila sehemu kama alivyoahidi hayati JPM akifanya kampeni 2020.

Hayo ndio maendeleo, ukienda Ujerumani huwezi kutofautisha kati ya kijijini na Berlin. Kinachopatikana kijijini ndicho kinachopatikana Berlin.
 
Mkuu labda tujue umuhimu wa taa usiku. Zinasaidia nini? Kwanini mjini ziwepo ila kijijini zisiwepo?
 
Mkuu labda tujue umuhimu wa taa usiku. Zinaidia nini? Kwanini mjini ziwepo ila kijijini zisiwepo?
Mjini kuna vibaka, vijijini hamna.
Mjini usiku kucha watu wanatembea au ulala night kali vijijini saa moja jioni watu wapo vitandani.
 
Ni vizuri ukajielimisha kwanza juu ya historia na maana ya ustaarabu na maendeleo jumuishi. Kwani kuweke taa za barabari ni kizuizi au ni kichocheo cha shughuli nyingine za maendeleo vijijini ?
Taa vijijini si kichocheo cha maendeleo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…