Nafaka
JF-Expert Member
- Feb 17, 2015
- 12,154
- 31,246
Hakuna waliotoka na uhasidi dhidi ya dogo, hao madada wametoa story yao kama walivyotoa wengine. Wamehojiwa nao wakasema kilichotokea wala hawakumtaja dogo na wala hawakujiita wao ni mashujaa.Hii nchi watu wanaroho mbaya ajabu watu badala ya kushukuru tu tumetoka salama bado wametoka na uhasidi juu huyu kijana kosa lake ni nini? aliomba haya? kwa kawaida ajali yoyote watu wanakuwa hawaoni kila kitu hasa unapokuwa unapigania maisha lakini hawa wametoka salama lakini utadhani humo ndani walikuwa wanajiokoa huku wanacheka, wahudumu wa ndege ni kazi yao na kama wamefungua ni kazi yao huyu kijana sio kazi yake kajitoa kwenda hata kama kafanya 1% lakini kajitoa kufanya wala hakuna shangazi yake kwenye ndege. Hamjui basi hata kusema Ttunashukuru Mungu maana kuna 19 wamekufa mnaanza wivu. Rizki anatoa Mungu na kijana ndio rizki yake. Swali Majaliwa alikwenda kuokoa au hapana? na yule Mama alisema mvuvi aliingia ndani na kumfungua mkanada kumsukuma nje naye alikuwa muhudumu au?
Wamesema kilichotokea na walichofanya. Sasa raia baada ya kusikia upande wa hao wahudumu ndipo wakaanza kuwa na mashaka ya story na ushujaa wa dogo.
Ila mwisho wa siku, Mungu akikufungulia milango ya riziki anakufungulia kweli kweli na pasipo kutaraji. Ndivyo mambo yanavyokuwa. Hata nyerere hakupigania uhuru peke yake, wapo wengi nyuma ambao hata hatujawahi kuwasikia.