#COVID19 Waziri Mkuu Majaliwa: Zoezi la chanjo ya Uviko-19 limefikia zaidi ya asilimia 80

#COVID19 Waziri Mkuu Majaliwa: Zoezi la chanjo ya Uviko-19 limefikia zaidi ya asilimia 80

Chanjo ya Korona ni kwa wote,hiyari yashindwa utumwa.
Bora kuchanja kwa hiyari sasa,kuliko kulazimishwa kuchanja hapo baadae.
Tusiochanjwa ni wakati wetu sasa kuchanja,hapo baadae tukilazimishwa
kuchanja kwa mawimbi mengine yajayo hayumkini tukapoteza kinga zetu kwa hofu.
 
Dah!!! Mbona taarifa kwenye database ya dunia inaonyesha tuna asilimia chini ya moja!!!
 
Wanafurahi 80& hehehe watu hawajafika hata 1m kwenye nchi ya watu 60m.🤣🤣🤣🤣
 
Kwa hiyo unabisha? Watu wanachanjwa kwa wingi mitaani. Hata wenyewe JF wameibuka na hashtag #UjanjaKuchanja.
Wameanza kudanganya tena.
JUMApili tu ilikuwa ni 40% na leo ni 80%

Tz tuwe serious.Tuache kudanganya.Tuzidi kuwahamasisha watu.Wananchi walichanganyikiwa na meseji pingana kutoka kwa viongozi.
 
Dodoma. Waziri wa Mkuu, Kassim Majaliwa amesema zoezi la chanjo ya Uviko-19 limefikia zaidi ya asilimia 80 na zilizobakia mikoani hivi sasa ni chache.

Jumla ya chanjo milioni 1.058 zilizopokelewa nchini kutoka nchini Marekani Julai 24, 2021 na uchanjaji ulizinduliwa rasmi Julai 29, 2021 na Rais Samia Suluhu Hassan.

Kauli hiyo imekuja baada ya Serikali kuanzisha kampeni maalum ya kuhamasisha uchanjaji wa chanjo hiyo katika maeneo mbalimbali ikiwemo makanisani na kwenye mikusanyiko ya watu.

Majaliwa ameyasema hayo leo Jumatatu Oktoba 4 2021, wakati akifungua kongamano la tano la uwezeshaji lililoandaliwa na Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (Neec).

“Tunalo zoezi la uchanjaji. Namshukuru Mungu tumefikia asilimia 80 na kitu huko, tumebaki na chanjo chache sana kwenye mikoa hiyo. Kila mmoja awahi huko na kama kuna mahitaji tutaleta nyingine malengo ni afya,”amesema.

Amesema suala la chanjo sio lazima lakini ni muhimu kwaasababu linasaidia kuongeza virutubisho mwilini na iwapo mtu atapata hawezi kuwa mwepesi kama vile mtu ambaye hajachanjwa kabisa.

Amewaagiza wakuu wa mikoa kutoa elimu na kuhamasisha kuhusu umuhimu wa kuchanja chanjo hiyo.

Mwananchi​

Baada ya kudanganya msikitini kwamba Rais yupo bize anaendelea na majukumu yake, huwa simuamini kabisa huyu mwamba
 
Baada ya kudanganya msikitini kwamba Rais yupo bize anaendelea na majukumu yake, huwa simuamini kabisa huyu mwamba

Katiba mpya ni muhimu sana kuondosha watu kama hawa kwenye nafasi ambazo uaminifu hauwezi kuwa na mbadala.
 
Usiseme ni uwongo. Wewe kutochanja, usidhani wote hawajachanjwa.

Jana nimeongea na ndugu yupo kijijini. Anasema zilipoletwa walichanja watu 6 tu, lakini baada ya Paroko wa RC, wachungaji wa KKKT na Anglikana kuwahuburia waumini wao Jumapili iliyopita, mpaka kufikia jana, chanjo zote zilizopelekwa katani zimekwisha, na wameomba nyingine.
Watanzania milioni zaidi ya 60 chanjo milioni moja tu mpaka kwa mbinde na kulazimishana huoni kama kuna tatizo mahala tangu ziije huu ni mwezi wa ngapi? na bado kampeni zinafanyika ili watu wajitokeze, think big
 
Kuna hela walichukua kwa mabeberu, ili waongezewe lazima chanjo ziishe. Hata wakiziteketeza/choma hat mbwa/ng’ombe hakuna ushahidi.

Si mnakumbuka wale watakaam walienda kuchoma ng’ombe chanjo na ng’ombe wakafa. Dkt Magufuli sijui yupo wapi.

Ila Mama Samia tunampongeza kwa msimamo wake wa hiari. Ila kuna upupu wa vikaragosi vinadhani eti iwe lazima
Mhh Mambo mengine ya kufikirika ...hivi Kuna ugumu gani was kuwadanganya the so called MAbeberu kuwa ...niongezee chanjo zile za awali zimeisha...!
Kwaninwataingia store?!
 
Mhh Mambo mengine ya kufikirika ...hivi Kuna ugumu gani was kuwadanganya the so called MAbeberu kuwa ...niongezee chanjo zile za awali zimeisha...!
Kwaninwataingia store?!

IMG_20211005_121843_647.jpg
 
Dodoma. Waziri wa Mkuu, Kassim Majaliwa amesema zoezi la chanjo ya Uviko-19 limefikia zaidi ya asilimia 80 na zilizobakia mikoani hivi sasa ni chache.

Jumla ya chanjo milioni 1.058 zilizopokelewa nchini kutoka nchini Marekani Julai 24, 2021 na uchanjaji ulizinduliwa rasmi Julai 29, 2021 na Rais Samia Suluhu Hassan.

Kauli hiyo imekuja baada ya Serikali kuanzisha kampeni maalum ya kuhamasisha uchanjaji wa chanjo hiyo katika maeneo mbalimbali ikiwemo makanisani na kwenye mikusanyiko ya watu.

Majaliwa ameyasema hayo leo Jumatatu Oktoba 4 2021, wakati akifungua kongamano la tano la uwezeshaji lililoandaliwa na Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (Neec).

“Tunalo zoezi la uchanjaji. Namshukuru Mungu tumefikia asilimia 80 na kitu huko, tumebaki na chanjo chache sana kwenye mikoa hiyo. Kila mmoja awahi huko na kama kuna mahitaji tutaleta nyingine malengo ni afya,”amesema.

Amesema suala la chanjo sio lazima lakini ni muhimu kwaasababu linasaidia kuongeza virutubisho mwilini na iwapo mtu atapata hawezi kuwa mwepesi kama vile mtu ambaye hajachanjwa kabisa.

Amewaagiza wakuu wa mikoa kutoa elimu na kuhamasisha kuhusu umuhimu wa kuchanja chanjo hiyo.

Mwananchi​



Na mnao wakati wa kuwasikiliza CCM na matapishi yao ??
 
Wakitaka hizo chanjo zote ziishe watangeze tu kila atakayechanjwa atapewa sahani ya wali na soda.

Watanzania wengi wanafikiri kwa kutumia tumbo kwahiyo tangazo hili litapelekea hadi watu kuchanja hata mara mbili ili wapewe wali wa bure.
 
Back
Top Bottom