Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Johnson matatani, kupigiwa kura ya kutokuwa na imani

Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Johnson matatani, kupigiwa kura ya kutokuwa na imani

Richard

JF-Expert Member
Joined
Oct 23, 2006
Posts
15,692
Reaction score
23,038
Leo jioni wabunge wa chama cha wahafidhina watapiga kura ya kutokuwa na imani na kiongozi wa chama hicho na waziri mkuu bwana Boris Johnson.

Hatua hiyo yafuatia barua za wabunge wa chama hicho kwa kamati maalum iitwayo 1922 committee ambazo zilipaswa kufikia asilimia 15 yaani sawa na barua 54 ili kuweza kupiga kura ya kutokuwa na imani.

Zoezi hilo la upoigaji kura litaenda haraka na bwana Johnson ana imani kubwa kuwa atashinda kura hiyo ambapo wengi wa wabunge wa chama chake wana imani nae.

Ili kumtoa bwana Johnson idadi ya wabunge wanotaka kumtoa bwana Johnson yatakiwa ifikie kura 108 huku bwana Johnson akiwa atembea kifua mbele kwa kuwa na wabunge 116 ambao tayari ni mawaziri katika serikali yake.

Katika kipindi cha wiki mbili mfululizo kumekuwa na kauli na wito kadha wa kadha za kumtaka kiongozi huyo ajiuzulu kutokana na kashfa za kufanya tafrija katika ofisi maalum ya namba 10 katikati ya muda wa kujitenga yaani "lockdown" kati ya mwaka 2021 na 2022.

Ushahidi mbalimbali umetolewa ukionyesha bwana Johnson kushiriki kuvunja kanuni na sera za kujitenga wakati wa ugonjwa wa Covid -19 ambapo watu zaidi wa 6 hawakutakiwa kukusanyika ndani ya nyumba moja au ofisi au mazingira ya kukutana katika chumba kimoja.

Baadhi ya wabunge wanoogopa kupoteza kura katika uchaguzi mkuu ujao wamekuwa wakikutana kufanya vikao vya siri kutengeneza mazingira ya kumtoa bwana Johnson kwa kuhofia watashindwa katika uchaguzi mkuu.

Pamoja na tatizo la kashfa bwana Johnson anakabiliwa na matatizo mengine makubwa manne ambayo ni ripoti ya kashfa tafrija ndani ya ofisi ya namba 10, sera ya kuwapeleka Rwanda wakimbizi wengi wenye asili ya Afrika, suala la Brexit na kushindwa kuwa na sera madhubuti za kujikinga na matatizo ya ukali wa maisha kwa wananchi wa Uingereza.
 
Nchi nyingine raha sana, kiongozi akizingua tu raia mnamtos fasta
 
Sijui kwanini waingereza hawataki kutulia siku hizi. Kila mara wanataka kubadilisha waziri mkuu.
 
Sijui kwanini waingereza hawataki kutulia siku hizi. Kila mara wanataka kubadilisha waziri mkuu.
Hali ya uchumi haijawa Sawa na pm Jonson alichangia nchi kujitoa umoja WA ulaaya na Hali ya gesi na mafuta kupanda wanaona sababu ni yeye sidhani kama atachomoka apa manaa wakimlimda uchaguzi ujao ukifika wabunge wengi WA chama chake watakosa nafasi na chama cha labour kitapata ajenda nyingi
 
Leo jioni wabunge wa chama cha wahafidhina watapiga kura ya kutokuwa na imani na kiongozi wa chama hicho na waziri mkuu bwana Boris Johnson.

Hatua hiyo yafuatia barua za wabunge wa chama hicho kwa kamati maalum iitwayo 1922 committee ambazo zilipaswa kufikia asilimia 15 yaani sawa na barua 54 ili kuweza kupiga kura ya kutokuwa na imani.

Zoezi hilo la upoigaji kura litaenda haraka na bwana Johnson ana imani kubwa kuwa atashinda kura hiyo ambapo wengi wa wabunge wa chama chake wana imani nae.

Ili kumtoa bwana Johnson idadi ya wabunge wanotaka kumtoa bwana Johnson yatakiwa ifikie kura 108 huku bwana Johnson akiwa atembea kifua mbele kwa kuwa na wabunge 116 ambao tayari ni mawaziri katika serikali yake.

Katika kipindi cha wiki mbili mfululizo kumekuwa na kauli na wito kadha wa kadha za kumtaka kiongozi huyo ajiuzulu kutokana na kashfa za kufanya tafrija katika ofisi maalum ya namba 10 katikati ya muda wa kujitenga yaani "lockdown" kati ya mwaka 2021 na 2022.

Ushahidi mbalimbali umetolewa ukionyesha bwana Johnson kushiriki kuvunja kanuni na sera za kujitenga wakati wa ugonjwa wa Covid -19 ambapo watu zaidi wa 6 hawakutakiwa kukusanyika ndani ya nyumba moja au ofisi au mazingira ya kukutana katika chumba kimoja.

Baadhi ya wabunge wanoogopa kupoteza kura katika uchaguzi mkuu ujao wamekuwa wakikutana kufanya vikao vya siri kutengeneza mazingira ya kumtoa bwana Johnson kwa kuhofia watashindwa katika uchaguzi mkuu.

Pamoja na tatizo la kashfa bwana Johnson anakabiliwa na matatizo mengine makubwa manne ambayo ni ripoti ya kashfa tafrija ndani ya ofisi ya namba 10, sera ya kuwapeleka Rwanda wakimbizi wengi wenye asili ya Afrika, suala la Brexit na kushindwa kuwa na sera madhubuti za kujikinga na matatizo ya ukali wa maisha kwa wananchi wa Uingereza.
Johnson hakutakiwa kuwa prime minister in first place
 
anajificha kwenye vita ya urursi na ukoraine ambayo hata hivyo imesababisha ugugmu wa maisha ya waingereza
 
Borison inaonesha ni mwongo UK haijawahi tokea

Lakini ni mwepesi wakusema yaliyopita si ndwele tigange yajayo

[emoji38]
 
Katika kipindi cha wiki mbili mfululizo kumekuwa na kauli na wito kadha wa kadha za kumtaka kiongozi huyo ajiuzulu kutokana na kashfa za kufanya tafrija katika ofisi maalum ya namba 10 katikati ya muda wa kujitenga yaani "lockdown" kati ya mwaka 2021 na 2022.
Usishangae ikawa kama ile ya Kigamboni 2020, ambao hawakumtaka walimchomekea jamaa akaenda kichwakichwa mwisho nje ya reli
 
Back
Top Bottom