Waziri Mwigulu: Makato ya Miamala ya Simu tunatunisha mfuko, ni 'Solidarity Fund'

Shida aliinhia kwa mbwembwe sasa aliona kila alichofanya mtqngulizi wake kama alikosea sana kumbe ye ndo kapuyanga! Ameteua mpaka mshauri wake binafsi wa uchumi sijui maendeleo ya jamii na Mpaka Hotuba zina mshauri jamani!!!!
 
Aisee
Aisee una hasira sana bro! Utakufa bure mdogo wangu; just relux kidogo..saivi dakika ya saba unataka umtoe Chama umueweke nani tena? Mbona anaupiga mwingi!!! Ahahah
 
Kweli haya ni mateso!
Baba Mungu uliyetuumba Watanzania, ikumbuke nchi yetu Tanzania, Wakumbuke Watanzania, Vikumbuke vizazi vyetu kama ulivyowakumbuka watoto wako wana wa Israel wakiwa utumwani Misri. Baba usiyakumbuke maovu ya ujana wetu wala maasi yetu yote. Tumekukimbilia wewe Bwana tusigharikishwe na mkono wa adui. Tutendee kwa ukarimu sawa na wingi wa Rehema zako.i Katika Jina Takatifu ya Yesu Kristo aliyehai milele tunakuomba. Amen.
 
Hizo kodi zimepitishwa na wabunge 100% CCM waliopita bila kupingwa na mawaziri wa Magufuli. Lipa kodo acha kulalamika
 
Mama anaupiga mwingi

Kapunguza 1% may mosi

Kalipizia kwenye mafuta na miamala mnapiga kelele

Miaka 100 kwa mama akeeeeeee[emoji12][emoji12][emoji12][emoji12][emoji12]
mikumi tena🤣🤣maccm bwana. yameanza kulialia tuliwambia huu uchaguzi wa mahunduki wa Magufuki utawakosti huko mbeleni hamkusikia
 
Kama nchi tulipita kipindi kigumu sana. Biashara zilifungwa, watu walifilisiwa, kodi nyingi za haramu zilibambikwa kwa wafanyabiashara. Aliyejaribu kufungua mdomo wake kulalamikia hayo labda asijulikane. Vinginevyo angetekwa kisha ama akapotea kabisa au akabambikiwa kesi itakayomuweka mahabusu muda mrefu au angehujumiwa kwa namna yoyote

Inashangaza kuona Wabongo ni wasahaulifu kiasi hiki. Angalau sasa kuna japo kauhuru ka kulalamikia hayo hadharani na usiwe na hofu ya kupotezwa. Au labda wanaotoa maneno makli dhidi ya awamu ya sita ni wale wachache sanasana waliokua wafaidika wa utawala ule!


Kodi hizi za miamala ni mbaya lakini haiondoi ukweli kwamba awamu iliyopita ilikua ya kidhalimu sana. Lakini kutamani eti ile hali ya mambo ya awamu ya tano irudie tena kwa Watanzania ni roho mbaya na utovu wa shukrani kwa Mungu wetu. Angalau Mama na serikali yake hamkamati mtu kwa kupinga sheria mbaya.

Mimi naamini ni suala la muda tu kodi kandamizi zitafutwa kutokanana na usikivu wa awamu ya sita. Lakini kutamani kurudi tulipotoka HAPANA
 
Kuchochea kamali na unywaji Pombe hapo ndo nimechoka kabisa yaani
 
Shida aliinhia kwa mbwembwe sasa aliona kila alichofanya mtqngulizi wake kama alikosea sana kumbe ye ndo kapuyanga! Ameteua mpaka mshauri wake binafsi wa uchumi sijui maendeleo ya jamii na Mpaka Hotuba zina mshauri jamani!!!!
Kusema ukweli Mama Samia amezingua kweli hili. Watu sio kwamba hawataki kuchangia cha msingi ongezeko lingekuwepo si kwa kiasi kile.
 
Zitafutwa lini? Umesahau alivyosema wameongeza kidogo tu sh 100 kwenye mafuta? Anashindwa kuelewa impact ya 100 kwa litre anahisi watu wanatumia sijui litre 1 tu
Acheni ujinga, tupo awamu ya 6, hivyo Jambo lolote la hovyo tutalipinga kwa nguvu zote
Unasema zitafuta zitafutwa, Kama zitafutwa kwa nini waliziweka?? Ili iweje
Asilimia kubwa ya watanzania wamejiajiri kwenye kilimo, lakini Cha kushangaza sasa hivi mbolea bei imeongezeka Mara mbili.
 
Jamani si tulikubaliana hapa kwamba mama anaupiga mwingi imekuaje tena tunamgeuka!!

Sent from my TECNO-J8 using JamiiForums mobile app
... tulifanya sherehe tulipoingizwa uchumi wa kati; tulipe kodi sasa maana hayo ndio matokeo ya kuingizwa uchumi wa kati. Watu walipe kodi haswa; hakuna kucheka na kima! Tuliipenda wenyewe, wapinzani wanachelewesha maendeleo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…