Waziri Ndumbaro awajibishwe kwa matokeo mabovu Law School

Waziri Ndumbaro awajibishwe kwa matokeo mabovu Law School

Mnaopiga mayowe wengi humu itakua mna supp au mmekuwa discontinued, LST ni habari nyingine ngumu lakini lazima profession iwe na njia yakugovern na kupunguza flow ya professionals mtaaani . Waendelee na utaratibu huo huo cz wakiachia mawakili wajae mtaani tayari itakuwa ni pigo kwa taaluma ndio maana hata sikuhizi unaskia kuna wakili au mtumishi wa mahakama anafanya double dealing. Waendelee kubana hata watoe watu kumi kwa mwaka ndio itakua poa ili na sisi tuiheshimu taaluma na tuheshimiane. Hapo uwaze umetoka kati ya hao wachache halafu mtu aje akuambie nifanyie notirization kwa alf tatu uone utakavyo mtimua, lakini wakiachiwa wakawa lukuki mtaani inakua ni changamoto tayari. Waziri asiwajibishwe bali aendelee na utendaji kazi wachuje mpaka tupate the best lawyers sio tu mauza uza wakili anafika mahakamani hawezi hata kujenga hoja.
 
Mnaopiga mayowe wengi humu itakua mna supp au mmekuwa discontinued, LST ni habari nyingine ngumu lakini lazima profession iwe na njia yakugovern na kupunguza flow ya professionals mtaaani . Waendelee na utaratibu huo huo cz wakiachia mawakili wajae mtaani tayari itakuwa ni pigo kwa taaluma ndio maana hata sikuhizi unaskia kuna wakili au mtumishi wa mahakama anafanya double dealing. Waendelee kubana hata watoe watu kumi kwa mwaka ndio itakua poa ili na sisi tuiheshimu taaluma na tuheshimiane. Hapo uwaze umetoka kati ya hao wachache halafu mtu aje akuambie nifanyie notirization kwa alf tatu uone utakavyo mtimua, lakini wakiachiwa wakawa lukuki mtaani inakua ni changamoto tayari. Waziri asiwajibishwe bali aendelee na utendaji kazi wachuje mpaka tupate the best lawyers sio tu mauza uza wakili anafika mahakamani hawezi hata kujenga hoja.

Mawazo mufilisi kabisa. Wengine haki yako tu inatuhusu hata kama hatuna maslahi nayo ya moja kwa moja:

Kama tunataka Katiba Mpya, Tusiionee "Haya" Haki ya awaye yote

Lau post #2 au 3 uliziona?

Ila kwa utambulisho wako umejieleza vizuri sana ndugu. Wewe utakuwa mtanzania halisi:

"Inasikitisha kuwa Tanzania bara ni jamii ya watu waliojaa ubinafsi, wivu, choyo, husuda, fitna, ujinga, na ujuaji uliopitiliza."

Watanzania wajinga na kuvuna wanayopanda

Umetuwakilisha vyema kabisa!
 
Waziri Ndumbaro aliunda tume ya Mwakyembe mwaka jana kutafuta suluhu ya matokeo mabovu Law School.

Ikumbukwe (kipindi hicho) wadau mbali mbali walilivalia njuga vilivyo suala la matokeo mabovu shuleni hapo.

Majaji waliunda tume yao ambayo waziri Ndumbaro aliwahakikishia suluhu, na kuwa hawakuwa na haja ya kuendelea jitihada zao.

Tume ya Mwakyembe ilikusanya maoni na kuja na yake. Post #2 na #3 ni moja ya maoni yaliyowasilishwa kwa Mwakyembe kama yalivyo.

Kwamba matokeo ya leo ni mabovu kuliko ya yaliyopelekea tume ya Mwakyembe kuundwa:

1. Tume hiyo kumbe ilikuwa ya kazi gani?
2. Pesa za mlipa kodi zilizotumika kwenye tume hiyo kumbe zilitupwa bure?
3. Kwa nini waziri angali ofisini?

Bila aibu waziri alikuwa bungeni kuwasilisha ya kwake kana kwamba hakujatokea kitu. Huku ni kuwakejeli wananchi.

Shit hole countries hazina utamaduni wa kuwajibika. Bila kuwachukulia hatua hawawezi kufahamu wapo kuwajibika na si kumcheza mtu shere.

Waziri huyu awajibishwe kwa kushindwa majukumu yake.

Ieleweke hakuna shule wanayokwenda kusomea kufeli.
Waziri haimhusu hiyo anayetakiwa kuwajibishwa ni wahadhiri chuoni walikotokea hao wanafunzi. Wanasiasa mnashindana kupeleka watoto wenu kwenda kusomea sheria kama kitega uchumi cha kujipatia pesa kwa njia za kitapeli wakati hawana uwezo kiakili kuchambua mambo kisheria. Shule ya sheria ina darasa la kimahakama na kitengo cha uchunguzi makosa; ukiwasikiliza waendesha mashitaka, mahakimu na mawakili wanafunzi kwenye zoezi zima utasikitika sana kwamba kwanza walifikaje kudahiliwa kuingia kenye shule ya sheria wakati kwanza lugha ya kigeni ni mbovu na hawana uwezo wa kujenga hoja zenye mashiko.

Kwa muktadha huo ni ndoto kufaulu hata nusu ya darasa sembuse hao 23. Si kila mtu anayesomea sheria lazima awe wakili washauriwe wajiingize kwenye fani zingine wanazozimudu vizuri sio kukikimbilia kwamba nataka niwe kama Lissu, Kibatala, Jebra, Chenge au Mkono. Practice ya sheria ni 'serious and aggressive commitment which is not politically motivated with vengeance ambition's hapo utakwama tu kama ilivyotokea hata wakipewa nafasi zaidi ya mara tatu hawatoboi maana msingi wa elimu yao ni dhaifu kwa matumizi ya akili pevu.
 
Mnaopiga mayowe wengi humu itakua mna supp au mmekuwa discontinued, LST ni habari nyingine ngumu lakini lazima profession iwe na njia yakugovern na kupunguza flow ya professionals mtaaani . Waendelee na utaratibu huo huo cz wakiachia mawakili wajae mtaani tayari itakuwa ni pigo kwa taaluma ndio maana hata sikuhizi unaskia kuna wakili au mtumishi wa mahakama anafanya double dealing. Waendelee kubana hata watoe watu kumi kwa mwaka ndio itakua poa ili na sisi tuiheshimu taaluma na tuheshimiane. Hapo uwaze umetoka kati ya hao wachache halafu mtu aje akuambie nifanyie notirization kwa alf tatu uone utakavyo mtimua, lakini wakiachiwa wakawa lukuki mtaani inakua ni changamoto tayari. Waziri asiwajibishwe bali aendelee na utendaji kazi wachuje mpaka tupate the best lawyers sio tu mauza uza wakili anafika mahakamani hawezi hata kujenga hoja.
Kumbe lengo lao ni kupunguza flow ya professionals mtaani.
Unafikiri wapo sahihi??
 
Waziri haimhusu hiyo anayetakiwa kuwajibishwa ni wahadhiri chuoni walikotokea hao wanafunzi. Wanasiasa mnashindana kupeleka watoto wenu kwenda kusomea sheria kama kitega uchumi cha kujipatia pesa kwa njia za kitapeli wakati hawana uwezo kiakili kuchambua mambo kisheria. Shule ya sheria ina darasa la kimahakama na kitengo cha uchunguzi makosa; ukiwasikiliza waendesha mashitaka, mahakimu na mawakili wanafunzi kwenye zoezi zima utasikitika sana kwamba kwanza walifikaje kudahiliwa kuingia kenye shule ya sheria wakati kwanza lugha ya kigeni ni mbovu na hawana uwezo wa kujenga hoja zenye mashiko.

Kwa muktadha huo ni ndoto kufaulu hata nusu ya darasa sembuse hao 23. Si kila mtu anayesomea sheria lazima awe wakili washauriwe wajiingize kwenye fani zingine wanazozimudu vizuri sio kukikimbilia kwamba nataka niwe kama Lissu, Kibatala, Jebra, Chenge au Mkono. Practice ya sheria ni 'serious and aggressive commitment which is not politically motivated with vengeance ambition's hapo utakwama tu kama ilivyotokea hata wakipewa nafasi zaidi ya mara tatu hawatoboi maana msingi wa elimu yao ni dhaifu kwa matumizi ya akili pevu.

Hivi uliwahi iongelea lugha ya kigeni ya jiwe - PhD holder? Au yule waziri wa elimu - Prof? Au tuseme ndiyo umefika duniani leo?

Umeelewa waziri aliunda tume kutafuta ufumbuzi na akatumia pesa zetu?

Vipi tija ya tume hiyo ya waziri? Hivi hata ilichukua maoni ya wadau kweli au ilikuwa na yake tu? Post #2 na #3 ziliwasilishwa kwenye tume kama maoni. Kumbe tume ilizingatia maoni kutoka wapi? Au ilichukua maoni toka kwenu tu?

Waziri aliwataka wadau kuwa na subira kuwa anakuja na suluhu. Akawaomba majaji kuondoa tume yao iliyokuwa imepanga kufanya uchunguzi huru.

Bado wewe huoni kwa nini waziri anapaswa kuwajibishwa?

Kwa akili yako hudhani hata CAG labda angeachana tu na hizi audits zake kwani anaowaletea ni heri mbuzi?
 
Waziri haimhusu hiyo anayetakiwa kuwajibishwa ni wahadhiri chuoni walikotokea hao wanafunzi. Wanasiasa mnashindana kupeleka watoto wenu kwenda kusomea sheria kama kitega uchumi cha kujipatia pesa kwa njia za kitapeli wakati hawana uwezo kiakili kuchambua mambo kisheria. Shule ya sheria ina darasa la kimahakama na kitengo cha uchunguzi makosa; ukiwasikiliza waendesha mashitaka, mahakimu na mawakili wanafunzi kwenye zoezi zima utasikitika sana kwamba kwanza walifikaje kudahiliwa kuingia kenye shule ya sheria wakati kwanza lugha ya kigeni ni mbovu na hawana uwezo wa kujenga hoja zenye mashiko.

Kwa muktadha huo ni ndoto kufaulu hata nusu ya darasa sembuse hao 23. Si kila mtu anayesomea sheria lazima awe wakili washauriwe wajiingize kwenye fani zingine wanazozimudu vizuri sio kukikimbilia kwamba nataka niwe kama Lissu, Kibatala, Jebra, Chenge au Mkono. Practice ya sheria ni 'serious and aggressive commitment which is not politically motivated with vengeance ambition's hapo utakwama tu kama ilivyotokea hata wakipewa nafasi zaidi ya mara tatu hawatoboi maana msingi wa elimu yao ni dhaifu kwa matumizi ya akili pevu.
Sasa huyu wakili mjinga akiingia mtaani si soko lenyewe tu litamtema mzee!! Atapata kesi siku ya kwanza, atashindwa kwa uzembe basi wateja watamhama na kuchagua mawakili bora

Ukisoma kanuni za LST zihusuzo mitihani na rufaa, na ukaulizia utekelezaji wa hizo kanuni hapo chuoni, huenda utabadili mtazamo wako na kuona kuwa wanafunzi hawana shida.
 
Kwa hisani ya mkuu MALCOM LUMUMBA:

Anaandika mdau:


Binafsi naomba nisema yafuatayo kuhusu shule ya sheria Tanzania:

Mosi, kutokana na uhitaji wa elimu ya kusoma kwa vitendo (Post-Graduate Diploma in Legal Practice) haikutakiwa kuwe na shule moja nchi nzima tena ambayo iko kwenye mji kama Dar es salaam. Walau hizi shule zingekuwepo kikanda ili kuwaepusha na kadhia wale wanafunzi wanaotoka mikoa ya mbali kuja kurudia mitihani Dar es Salaam. Mtoto anasafiri kutoka Tarime, hana hata mkopo halafu anakuja Dar es salaam kufanya mtihani akiwa na 50/50 kwamba hilo somo analorirudia atafuaulu au lah.

Pili, mbinu ya kumpima mwanafunzi (Mode of Assessment) siyo rafiki kabisa na haizingatia utaalamu wa kisaikolojia kwamba wanafunzi wana uelewa tofauti. Mtoto anasoma mwaka mzima halafu anapewa mitihani 24 ndani ya mwaka ambayo kama akifeli hata mmoja basi anaweza kupoteza zaidi hata ya miaka 2 anarudia tu kozi hiyo hiyo. Kikawaida tulitegemea kwenye elimu ya vitendo wanafunzi wapimwe kupitia kazi nyingine muhimu ambazo lazima ziwe na alama, kama PRESENTATIONS, GROUP ASSIGNMENTS, CLINICS + WORKSHOPS and INTERNSHIP WITH MARKS.

Sasa wanaitwa DIPLOMA IN LEGAL PRACTICE huku wakichukua ada ya zaidi ya milioni moja, ilhali vipimo vyote vinatolewa kupitia mitihani. Hii siyo sahihi, kwasababu hata mahakamani kwenyewe wanasheria huwa hatuviziani ila tunapewa muda wa kujiandaa. Sasa mtoto anakaa INTERNSHIP miezi zaidi ya sita huku akija kukaguliwa kihunihuni tu mara moja, bila kupewa alama yoyote ile ya muhimu. Kwanini hawa wanafunzi wasipangiwe hata miezi miwili-miwili kufanya kazi la lazima zenye alamu mahakama za mwanza, mabaraza ya ardhi, mabalaza ya usuluhishi, dawati la jinsia ???

Jingine, ambalo nimeliona ni jambo la kipumbavu kufanywa na watu wanaojiita wasomi ni kitendo cha kutoa matokeo ya mitihani yote ya mwaka mzima ndani ya siku moja, baada ya mwaka mzima na miezi mitatu kupita. Kwanini matokeo ya ICA (Individual Continous Assessment), WPE (WRITTEN PRACTICAL EXAMINATION) na FINALS NON-CORE hayatolewi mapema, ili mwanafunzi ajue mbivu na mbichi na aweze kujipanga vizuri kwenye mitihani ya mwisho ??? Pia wawekewe utaratibu maalamu kabisa wa kuyarudia haya masomo wakati hata wako shule, hasa wiki moja baada ya kumaliza WPE ???

Lingine muhimu ni kwamba LST, kuna mitihani ya WPE (Written Practical Examination) ambayo kwingineko duniani mwanafunzi huifanya kwa kufanya tafiti pamoja na majadiliano na wanafunzi wenzake, kisha baadae huenda kufanya huo mtihani. Ilhali sasa pale LST, wanafunzi wanafungiwa masaa manne (4) wakisoma mavitabu, bila kuruhusiwa kuzungumza halafu wanapewa saa moja kupumzika, ili warudi kufanya mtihani huohuo kwa masaa matatu. (It's just emotional debilitating)

Tatu, hili la kulazimisha kila anayesoma sheria awe wakili nadhani ni jambo la kishenzi ambalo lilifanywa kwa mihemko bila kufikiriwa. Miaka yote huko nyuma watu tuliajiriwa kama STATE ATTORNEYS bila hata kuwa wanasheria. Tulitakiwa tu tufanye INTERNSHIP miezi tisa kwa ATTORNEY GENERAL halafu tunaenda kufanya BAR-EXAMINATION kule Arusha. Kinachoshangaza ni kwamba wengi ambao hawakupita Law School wako vizuri kuliko hata hawa watoto wenu wa Mawasiliano nyuma kule.

Kubwa zaidi, wanasheria tuko kwenye nyanja kuu mbili ambazo ni LEGAL PRACTITIONER (ADVOCATES) na JURIST (LEGAL SCHOLARS/LEGAL RESEARCHERS). Hawa ni watu wawili tofauti na wanafanya kazi tofauti kabisa, sasa ukitaka kuwalazimisha wawe kitu kimoja utakuwa unapuyanga mno. Leo hii ushauri wa sheria wa JURIST unaweza kuwa una uzito kuliko hata ORDINARY LEGAL PRACTITIONER, kutokana na tafiti na ufahamu. Sasa kwenye nchi fulani ya kusadikika, wenyewe kwasababu hawana SPECIALIZATION basi wanalazimisha kila mtu awe wakili, kwamba hata JURIST haweza kutoa ushauri kama hana muhuri. Just Lackadaissical and Nonsensical....

Nne, mtaala wa shule ya sheria ni wa kizamani sana na hauwezi kumfanya mwanafunzi awe vizuri kwenye soko la kimataifa. Kuna baadhi ya masomo tulitegemea yafundishwe pale LST, lakini hayapo kwenye mtaala. Mfano, INTERNATIONAL COMMERCIAL ARBITRATION, INVESTMENT LAW, BASICS OF INTERNATIONAL ECONOMICS LAW/ INTERNATIONAL TRADE AND FINANCE LAW. Nchi haina wataalamu wa haya masomo, sisi tunakomaa kufundisha PROPABATE & ADMINISTRATION OF ESTATES, COMMERCIAL LAW, LEGAL ETHICS, HUMAN RIGHTS and ACCOUNTS FOR LAWYERS masomo ambayo vyuo vingi vinayafundisha na vinaweza kuyafundisha vizuri.

Kesi kubwa kama zila za makinikia, DOWANS, ESCROW n.k zinahitaji mwanasheria walau awe anajua masomo ya INTERNATIONAL COMMERCIAL ARBITRATION, ambapo anatakiwa aifahamu mikataba mikubwa BIT (Bilateral Investment Treaties), pamoja na taasisi muhumu kama ICSID, PIC, ICC. Lakini sisi tunakomaa kuwafelisha watoto masomo kama ACCOUNTS. Sijui hii nchi haina watu wenye akili kabisa. Mambo ya ajabu yanafanyika na hakuna hata anayestuka.

Tano, mradi wa LST tangu mwaka 2006 marehemu Prof. Mukoyogo aliupinga kweli kwasababu aliona hauna maana zaidi ya kuwatengenezea ulaji baadhi ya wataalamu wa pale University of Dar es Salaam. Hivi kweli, tuna uhakika kwamba haya masomo ya LST hayawezi kufundishwa vizuri kwenye vyuo ambavyo wanafunzi wanasoma wakiwa wanatafuta Shahada ya kwanza kweli ???

Jambo jingine ni kwamba wataalamu wengi wa pale LST wameamua kufanya biashara ya vitabu. Wanatunga mitihani ambayo majibu yake utayapata kama tu umenunua vitabu vyao. Hili nilishawahi kuambiwa nikathibitisha mwenyewe kwenye baadhi ya vitabu. Hii ni tabia ya kishezi ambayo inaumiza na kukwamisha wengine huku wengine wakipata ukwasi mkubwa. Mwanafunzi anataoa pesa nyingi za Ada lakini hivyo vitabu havipo maktaba, utavipata mpaka umfuate mwandishi mwenyewe na umlipe 50,000. Kwanini msiweke vitabu vingi kule maktaba wanafunzi wakavisoma ???

Sita, hivi inawezekanaje mwanafunzi ambaye amefauli vizuri shahada yake afeli vibaya kwa kiwango cha DISCONTINUE pale LST ??? Ina maana huyu mwanafunzi hafahamu kitu chochote kabisa ??? Lakini, kubwa zaidi ni hili la wanafunzi 600 kuanza pamoja, lakini wanaofaulu ni watu 30, huku nusu ingine ikiwa inafanya SUPPLEMENTARY au DISCONTINUED. Sijui kwanini hili haliwastui Majaji na Wizara. Watu hufeli, lakini siyo kwa kiwango hicho ambacho kinafanyika pale Law School.

Pia, pale pana rushwa sana ya ngono, kukomoana na kubadilishiana matokeo. Kuna jamaa niliwahi kuwa naye mahakamani aliwahi niambia kwamba kuna rafiki zake wanafundisha pale walimuahidi kwamba watamfaulisha, na kweli alifauri vizuri hadi tukashangaa. Alikuwa na maswali hata kabla mitihani haijaanza. Nikasema HIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIII...


TANZANIA HAKUNA KITU KINACHOFANYA KAZI VIZURI KUSEMA TUNAWEZA JIVUNIA
Mkubwa umeandika vizuri sana. Ambaye atashindwa kukuelewa ana lake jambo. Wahusika kama wapo serious wanapakuanzia kufanya reform just kwa ushauri wako huu. Ubarikiwe sana.
 
Kufaulu ni jambo la kawaida na linalotegemewa (expected). Watu wanasoma ili kuondoa ujinga na pia kufaulu mitihani, hatuwezi kushangaa kwa nini watu wanafaulu wakati tunajua ndio lengo mojawapo la kusoma, tunashangaa na kuhoji pale watu wanapofeli.

Waziri hawezi kusifiwa kwa kuongoza chuo chenye ufanisi mdogo, tunamhoji kuwa kwa nini asiwajibishwe kwa kutumia fedha nyingi kuendesha chuo bila manufaa!!
Naona umeandika vitu vingi visivyo na maana!

Hoja hapa ni moja, wanafunzi kufeli. Nikasema shida ya kufeli haipo kwa walimu au law school iko kwa wanafunzi wenyewe. Ningesema law school wana shida ikiwa hakuna mwanafunzi hata mmoja amefaulu.

Kama kuna wanao fauli ina maana mfumo wa law school unaeleweka na hauna shida.
 
Huku secondary ndo balaa! Mtoto wa kidato Cha pili anafundishwa 'functions of electral committee'!! Semeni wenyewe kama mtoto wa kidato cha pili anapaswa kufundishwa mambo haya.. kama mnashangaa ya TLS basi shangaeni na hili.
 
Mkubwa umeandika vizuri sana. Ambaye atashindwa kukuelewa ana lake jambo. Wahusika kama wapo serious wanapakuanzia kufanya reform just kwa ushauri wako huu. Ubarikiwe sana.

Kama ilivyo kwenye mada, hayo yote yaliwasilishwa tume ya Mwakyembe wakaona ni upuuzi mtupu.

Hawana nia njema bali ule ule uswahili wetu na akina Upepo wa Pesa tuliouzowea.
 
Naona umeandika vitu vingi visivyo na maana!

Hoja hapa ni moja, wanafunzi kufeli. Nikasema shida ya kufeli haipo kwa walimu au law school iko kwa wanafunzi wenyewe. Ningesema law school wana shida ikiwa hakuna mwanafunzi hata mmoja amefaulu.

Kama kuna wanao fauli ina maana mfumo wa law school unaeleweka na hauna shida.
Tufanye umeongea jambo la maana. Umeongelea mfumo, sasa hebu soma kanuni za Rufaa uone huo mfumo ulivyo sawa.
 
Back
Top Bottom