Waziri Ndumbaro: Royal Tour ya Rais Samia yaanza kuzaa matunda kwa kuleta wawekezaji

Waziri Ndumbaro: Royal Tour ya Rais Samia yaanza kuzaa matunda kwa kuleta wawekezaji

MBWARI

Member
Joined
Sep 8, 2021
Posts
27
Reaction score
782
SHUGHULI za Royal Tour zilizokuwa zikifanywa kwa mara ya kwanza nchini na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan za kutangaza vivutio vya Utalii, Biashara na Uwekezaji nchini zimeanza kuzaa matunda kwa wawekezaji kuanza kujitokeza kuwekeza hoteli za kisasa ndani ya hifadhi za Taifa.

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Damas Ndumbaro amesema mara baada ya mkutano wake maalum na Wawekezaji uliofanyika Dar es Salaam mapema leo. Wawekezaji hao wanatoka Bara la Ulaya katika nchi ya Bulgaria na watajenga hotel za Nyota tano mithili ya Kempinski kwenye hifadhi Nne za Taifa nchini.

Waziri Dk. Damas Ndumbaro amesema mpango mkakati wa Rais Samia Suluhu Hassan kupitia kuandaa kipindi cha Royal Tour umeweza kuzaa matunda hayo na wao kama Wizara wameupokea na sasa ni utekelezaji.

''Juhudi kubwa za kimkakati za Royal Tour zilizoendeshwa na Rais wetu zimeweza kuzaa matunda ambapo leo tumepokea wawekezaji mahiri kutoka Bara la Ulaya ambao watawekeza kwenye hoteli kwa kujenga hoteli tatu za nyota tano za 'brand' ya Kempinski kwa uwekezaji wa Dola za Kimarekani Milioni 72.

''Mkutano wetu huu hii leo umekwenda vizuri sana na Wawekezaji hawa kwa hiyo unaweza kuipata hoteli ya Kempinski baada ya ujenzi huo kukamilika. .. Kempinski Serengeti, Kempinski Manyara, Kempinski Tarangile na Kempinski Ngorongoro." Amesem Dk. Ndumbaro.
 
Ule uongo wa awamu ya 5 bado unaendelea?

IMG_20210528_133707.jpg
 
Nchi hii ndugu zangu watu wana vituko sana.

Yaani mwenye kurekodi alisema video itarushwa next year mara paaap, 'ROYAL TOUR IMEZAA MATUNDA' ni kwa njia au matangazo gani hayo?

Hivi kweli tunachotwa akili hivi hivi na wanasiasa?.

Alafu hao wawekezaji wanakuja kujenga ndani ya hifadhi wakati huo huo mnakataa kujenga miundombinu ya uhakika as barabara/reli ya kutoka Musoma to Arusha kisa itaharibu uasili na kuua ekolojia sijui bainuai mmh😳!.
 
Wana-CCM ni watu wa ajabu sana, hivi mama Samia haoni hili nj tatizo?
Waziri anasifia mafanikio ya royal tour ikiwa hata haijazinduliwa Wala kuonyeshwa popote?
 
Mitego ya Rais Samia ya Royal Tour yanasa TZS 158.4bl | Hoteli nne kubwa za kitali hadhi ya Kempinski kujengwa Serengeti, Ngorongoro,Manyara & Tarangire,
________________________________

Wawekezaji toka Bulgaria matokeo ya Royal Tour kuwekeza US$ 72M karibu sawa na Tsha 158.4BL kwa kujenga Hotel nne kubwa za nyota tano ( Five Stars Hotel ) katika mbunga za Serengeti, Ngorongoro, Manyara & Tarangire,

Utawala wa Rais Samia Suluhu Hassan kwa kipindi kifupi cha miezi sita umeonesha matokea makubwa katika kila kona ya nchi, madhalani uwekezaji tayari umekua kwa 400% toka uwekezaji wa US$ 510M hadi US$ 2.98BL sawa na Tshs 7trilioni pesa ambayo itamfikila kila Mtanzania popote alipo katika njia moja au nyingine,

#Mliokuwa mnalalamikia gharama ya Royal Tour mnasemaje kuhusu hizi bilioni 158.4 za fasta !??


.........Kazi iendelee.........

IMG-20210923-WA0081.jpg
 
#MSIKILIZE WAZIRI WETU DK NDUMBARO
 

Attachments

  • VID-20210924-WA0028.mp4
    12.1 MB
Documentary ya Royal Tour bado haijazinduliwa so bado haijaanza kuonekana huko ulimwenguni ni vipi unahusanisha huu uwekezaji (kama kweli) na hiyo documentary! Lakini kama ni kweli kuna huu uwekezaji basi ni habari njema sana! hasa kwa sekta ya utalii
 
Kempsiki inajulikana mwenye share kubwa tanzania ni nani mkuu
 
Nakata tamaa mpaka nimechoka

Sasa nataka nianze kukata kuchoka mpaka niikute tamaa
 
Musiba wa awamu hii ya Samia

[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Mkuu msikilize waziri wetu huyu makini kabisa hapo juu,
Documentary ya Royal Tour bado haijazinduliwa so bado haijaanza kuonekana huko ulimwenguni ni vipi unahusanisha huu uwekezaji (kama kweli) na hiyo documentary! Lakini kama ni kweli kuna huu uwekezaji basi ni habari njema sana! hasa kwa sekta ya utalii
 
Kwa mbali inaonekana ni jambo jema sana....., ILA.....

Wanakodishwa ardhi kufanya huo ujenzi na kulipa malipo yote au tunawapa grace period ya miaka mingapi

Nilishajua siku hizi bila kuona mkataba ni vigumu kushangilia haya mambo
 
Mkuu msikilize waziri wetu huyu makini kabisa hapo juu,
Kati ya mwaziri ambao sina imani nayo ni huyu Ndumbalo! kama source hi huyu basi sikubali kuwa uwekezaji huu umetokana na Royal tour!
 
Back
Top Bottom