Waziri Ndumbaro: Wamasai waishio Ngorongoro siyo wenyeji halisi wa Ngorongoro

Waziri Ndumbaro: Wamasai waishio Ngorongoro siyo wenyeji halisi wa Ngorongoro

Wakati wa mahojiano na DW Waziri ndumbaro amekaririwa akisema Wamasai washio Ngorongoro siyo wenyeji halisi wa ngorongoro.

Imeibua mjadala mingi baada ya wananchi wasomi kutoka jamii ya kimasai kumwomba rais kutengua waziri wa mali ya asili kwa kauli yake kwamba Wamasai kwao ni sudan na siyo Ngorongoro.

Pia wananchi walitaka kujua kama hiyo ni kauli chama na serikali au ni kauli ya ndumbaro kama ndumbaro!!

Ni sahihi waasisi wetu, NYERERE, SOKOINE et.all walituachia taifa la Tanzania likiwa na makabila 120 na lugha yetu pendwa ya kiswahili ili kuweza kuwaleta watanzania wote bila kujali itikadi yao, dini yao, wala makabila yao na wote tunajitambulisha ni watanzania na siyo waamasi au Wachagga

Kumekuwa na malalamiko mengi kutoka kwa jamii ya kimasai kwamba wanaonewa serikali ya CCM kwasababu wao wanachukuliwa kama Wamasai na siyo watanzania!!

Baadhi ya wananchi wamemwomba mkuu wa nchi kumchukulia hatua mhusika huyo kwa kuvunja umoja wa watanzania uliopiganiwa na waasi wa taifa hili!!

Malalamiko hayo na mgogoro mkubwa huo unatokana na hatua ya wizara kuendelea na mchakato wa kuwaondoa wenyeji hao ili kupisha shughuli za uhifadhi na utalii!

Na wenyeji wameapa kwa aina ya uongozi wa wizara ya maliasili na utalii na baadhi wataalam kamwe mgogoro wa wananchi na uhifadhi hautaishia!!
Waziri wa ajabu sana huyu. Naona amechoka kazi hiyo ya kuwatumikia Watanzania.
 
Eneo la Ngorongoro kihistoria watu wa Kwanza kuishi hapo ni Wadatooga na Wairaqwi kwani ndio walikuwa wanafuatana na kuishi kindugu tokea Ethiopia... so walipokuja Wamasai kutokea huko Sudan kwa watu weusi nubian wakawafanyia fujo Wairawi na Wadatooga wakakimbia bila kupenda japo walionywa na Mtabiri wao waondoke wakabaki kupigana kama waukraine dhidi ya Urusi... so Masai waache ujinga kama wambulu walitoka hata wao watatoka tu
Mungu anawavuruga. Endeleeni kuchanganyikiwa hivyo hivyo.
 
Mie mwenyewe nimezaliwa hapa na mababu zangu kibao lakini leo naweza kuambiwa mkimbizi ghafla. Tz kila kitu ni imaginations utadhani ni nchi ya wachawi
 
🐒🐒🐒
 
Watu msipotoshe kauli ya waziri
Waziri alikua anajibu swali kuhusuNgorongoro kuwa "acentral land" ya Wamasai. Na akajaribu kuonyesha huo uwongo unaokuzwa na NGO's lukuki zilizo jazana Ngorongoro kuwa hao waliletwa hapo na Wakoloni mwishoni mwa miaka ya hamsini tuu, na sio kweli kuwa hiyo ni ardhi yao ya miaka na mikaka kwani miaka hiyo walikuwa njiani toka Sudan.
 
Hii ni kweli kwa upande mmoja na sii kweli kwa upande mwingine.

Ni kweli kwa sababu wakati NCAA inaanzishwa Ile 1959, Wamasai waliondolewa maeneo yao ya asili ya Serengeti na wakapelekwa Ngorongoro, hivyo ni kweli, Ngorongoro kuna baadhi ya Wamasai ni watu wakuja.

Sii kweli kwasababu ndani ya Ngorongoro kuna baadhi ya Wamasai ni wa asili pale.

Na ukweli wa mwisho, Tanzania ni eneo la asili la Bantustans, watu wa asili kabisa wa Tanzania ni Wagogo, Wasukuma na makabila machache ya asili ya Kibantu, Masai sio Bantu, ni Semi Nilotic, asili yao ni North Africa wame descend from Nubi, Walihamia East Africa kutokea Northern Sudan during early migration baada ya kutimuliwa na Wakushi.

Hata Waziri mwenyewe ni Mngoni, nao asili yao sio Tanzania, ni jamii ya Wazulu waliokimbia Mfecane wars , wakiongozwa na Zongendamba ndio wakaingia Tanzania na ku settle Songea. Makabila mengi ya mipakani wakiwemo Wachagga, ni wahamiaji tu.

Lakini Ile siku tunapata Uhuru, kuanza saa 6:01 ya usiku wa December ,9, 1961, kila mtu aliyekuwepo kwenye ardhi ya Tanganyika, alipewa uTanzania bure. Hivyo sio busara kuwabagua watu based on early migration.

P
Maasai wahame au wapunguzwe, ķupunguza watu sio ubàguzi, ni maendeleo kwani ardhi ni mali ya rais. Hivyo basi waondolewe kama wana madhara, mbona sehem7 nyingine watu waliamishwa mfano kahama baada ya ugunduzi wa dhahabu.
 
Maasai wahame au wapunguzwe, ķupunguza watu sio ubàguzi, ni maendeleo kwani ardhi ni mali ya rais. Hivyo basi waondolewe kama wana madhara, mbona sehem7 nyingine watu waliamishwa mfano kahama baada ya ugunduzi wa dhahabu.
Nikurekebishe kidogo, ardhi sio Mali ya rais, ni Mali ya umma wa Watanzania, rais ni mdhanini tuu, kwa niaba yetu
P
 
Na wamasai wakijibu kwamba wangoni nao sio wenyeji wa Ruvuma.Huyu waziri atajisikiaje?
Kuna kauli zingine za kipumbavu hata hazifai kujadiliwa kwa kina.Hii ni mojawapo.
Huyu waziri awaombe radhi wamasai wa Ngorongoro na watanzania kwa ujumla.
 
  • Thanks
Reactions: Tui
Hii ni kweli kwa upande mmoja na sii kweli kwa upande mwingine.

Ni kweli kwa sababu wakati NCAA inaanzishwa Ile 1959, Wamasai waliondolewa maeneo yao ya asili ya Serengeti na wakapelekwa Ngorongoro, hivyo ni kweli, Ngorongoro kuna baadhi ya Wamasai ni watu wakuja.

Sii kweli kwasababu ndani ya Ngorongoro kuna baadhi ya Wamasai ni wa asili pale.

Na ukweli wa mwisho, Tanzania ni eneo la asili la Bantustans, watu wa asili kabisa wa Tanzania ni Wagogo, Wasukuma na makabila machache ya asili ya Kibantu, Masai sio Bantu, ni Semi Nilotic, asili yao ni North Africa wame descend from Nubi, Walihamia East Africa kutokea Northern Sudan during early migration baada ya kutimuliwa na Wakushi.

Hata Waziri mwenyewe ni Mngoni, nao asili yao sio Tanzania, ni jamii ya Wazulu waliokimbia Mfecane wars , wakiongozwa na Zongendamba ndio wakaingia Tanzania na ku settle Songea. Makabila mengi ya mipakani wakiwemo Wachagga, ni wahamiaji tu.

Lakini Ile siku tunapata Uhuru, kuanza saa 6:01 ya usiku wa December ,9, 1961, kila mtu aliyekuwepo kwenye ardhi ya Tanganyika, alipewa uTanzania bure. Hivyo sio busara kuwabagua watu based on early migration.

P
Tukianza kuchimbana hapa kutakuwa hakuna mtanzania wa asili, nchi kama Sudan, somalia etc sababu ya vita visivyoisha ni upuuzi kama huu unaoitwa asili, Kiongozi mkubwa kama waziri hatakiwi kutoa statement careless namna ile
 
  • Thanks
Reactions: Tui
Kuna Mkataba unaodaiwa kusainiwa na waitwao Wazee wa Kimila na Mkoloni Mwingereza mwaka 1958 mbao umesemwa sana hapa JF uliowahamisha Wafugaji wa Kimasai kutoka Serengeti kuhamia Ngorongoro.

Kama huo Mkataba upo, basi ni dhahiri Wafugaji wa Kimasai siyo wenyeji wa Ngorongoro.

Ni Wahamiaji.
Warudisheni huko Serengeti Sasa.
 
  • Thanks
Reactions: Tui
Basi warudishwe Serengeti kama Ngorongoro siyo kwao. Jamii hii ya wafugaji ndiyo ambao wametusaidia hadi leo tina hizo hifadhi za wanyama sasa kama zawadi yao ni mateso basi semeni. All we enjoy mpaka sasa ni kwasababu yao, get your facts right!
Ame, wanaotaka Jamii ya Wafugaji wa Kimasai waendelee kuishi bila haki ya kumiliki ardhi, bila haki ya kuishi kwenye nyumba bora, bila kuendesha vyombo vya moto, waeleze bayana kuwa wako tayari kuhamia huko Ngotongoro, wao na wake zao au waume wao na watoto wao. Kinyume cha hapo, wajiitao Watetezi ni Wanafiki
 
Wangoni, wamasai, wachaga, waha, wahaya, wanyakyusa, wawanji, wamakonde na wamakua, wajaluo, wahangaza, na kadhalika hao ni watu wakuja Tanzania sio asili yao waangalie hata mfumo wa maisha yao
vikauli vya kipuuzi kama hivi mwisho wake ni vita tuu na chuki tuu
 
Watu msipotoshe kauli ya waziri
Waziri alikua anajibu swali kuhusuNgorongoro kuwa "acentral land" ya Wamasai. Na akajaribu kuonyesha huo uwongo unaokuzwa na NGO's lukuki zilizo jazana Ngorongoro kuwa hao waliletwa hapo na Wakoloni mwishoni mwa miaka ya hamsini tuu, na sio kweli kuwa hiyo ni ardhi yao ya miaka na mikaka kwani miaka hiyo walikuwa njiani toka Sudan.
What a stupid minister that we have.
 
Ame, wanaotaka Jamii ya Wafugaji wa Kimasai waendelee kuishi bila haki ya kumiliki ardhi, bila haki ya kuishi kwenye nyumba bora, bila kuendesha vyombo vya moto, waeleze bayana kuwa wako tayari kuhamia huko Ngotongoro, wao na wake zao au waume wao na watoto wao. Kinyume cha hapo, wajiitao Watetezi ni Wanafiki
Haki kama wanahitaji si wangeomba? Tangu lini kiatu usichokivaa ukajua kinaumiza wapi? Mnafiki nani kati ya wanaojidai wanawatafutia haki wakati wao wenyewe wanaona wanapokwa haki yao?
 
Hali ya kumuabudu Magufuli kwa hawa wafuasi wake kama Nebuchadinezzer lazima tuukomeshe. Magufuli alivunja umoja wa kitaifa kwa vitendo vyake viovu. Alisema kabisa "siwezi kupeleka miradi ya maendeleo kwenye maeneo ambayo wananchi wamechagua upinzani"
Wewe ng'ombe mwache Rais wetu Magufuli ameshamaliza kazi yake na sasa anapumzika huko kwa Mwenyezi Mungu. Tunajua wewe ni fisadi kubwa hapa TZ ulinyooshwa wakati wa Magufuli hata sasa hivi utaendelea kunyooshwa tu pamoja na kujipendekeza kwa Mama Samia!
 
Wewe ng'ombe mwache Rais wetu Magufuli ameshamaliza kazi yake na sasa anapumzika huko kwa Mwenyezi Mungu. Tunajua wewe ni fisadi kubwa hapa TZ ulinyooshwa wakati wa Magufuli hata sasa hivi utaendelea kunyooshwa tu pamoja na kujipendekeza kwa Mama Samia!
Magufuli hawezi kupumzika, ataendelea kuungua tu na moto wa jehanam.
 
Back
Top Bottom