Waziri Simbachawene jiuzulu, una-underperfom. Ajali zitamaliza Watanzania

Waziri Simbachawene jiuzulu, una-underperfom. Ajali zitamaliza Watanzania

Jukumu la kwanza la usalama ni wewe Abiria unatakiwa kulichukua .

Kuna wakati nilisafiri kutoka dodoma kuja Dar abiria mwema akapiga simu polisi chalinze kuwa dereva anaendesha Mwendo kasi pasipo tahadhari polisi wakasimamisha basi likaenda kituoni , abiria wote walimtetea dreva yule abiria akaonekana hana hoja basi likaruhusiwa.

Mimi mwenye nilimuamuru dereva aendeshe basi kwa tahadhari tukitokea Mwanza kuja Dar nikidai haki yangu ya kuendeshwa kwa kufuata sheria za barabarani baada ya dereva kutaka kutuangusha Ilibidi basi lisimame abiria wakamtetea dereva.
Kweli kabisa

Na hilo kila siku wanaambiwa,abiria ukiona dereva ana kimbiza mwendo wa kasi mseme

Ova
 
Habari za asubuhi wana JamiiForums

Kwa maslahi ya taifa naona tujadili hili swala. Naona halizungumzwi mahali popote ukiachilia matatizo mengi tuliyonayo kama taifa kwa sasa.

Kumezuka tatizo la ajali za kila mahala takribani ajali 4-5 kwa siku zinaripotiwa kwenye mitandao ya kijamii zikihusisha vyombo vya usafiri wa abiria kama Mabasi yaendayo mikoani.

Pamoja na kuwa usafiri na usimamizi wake uko chini ya Wizara ya mambo ndani hatuoni hatua yoyote inayochukuliwa na Waziri mwenye dhamana Mh Simbachawene. Sio tu kuchukua hatua bali hata kulizungumzia tu yuko kimya.

Kwa maoni yangu na jinsi navyoona ripoti hizi naweza kusema baada ya vifo vya corona Ajali tanzania inashika namba mbili.

Tusifanye siasa kwenye maisha ya watu. Mh Rais anakopa pesa kila siku zije nchini kusaidia watanzania sasa kama watanzania wanateketea kwa ajli kila siku huku wengi wakiachwa na ulemavu wa kudumu itakuwa haina maana.

Utendaji wa Mh Simbachaweni uko chini ya kiwango kuliko hata wa Kangi Lugola.
Waziri mwenye dhamana mmemsikia?
 
Kweli kabisa

Na hilo kila siku wanaambiwa,abiria ukiona dereva ana kimbiza mwendo wa kasi mseme

Ova
The moment amekimbiza mwendo kasi kabla hujamsema dereva tayari ajali ishatokea.
 
Back
Top Bottom