Waziri Ulega akipiga mkwara na Kingereza cha ugoko

Waziri Ulega akipiga mkwara na Kingereza cha ugoko

Kwa aibu niliyojiskia leo baada ya kusikiza Kiingereza cha Waziri Ulega akizungumza na Wakandarasi Wachina wanaojenga barabara ya mwendokasi huko Mwenge leo nakuomba tu Msemaji wa Serikali zungumza na Waandishi wa habari na waombe tu wasirushe zilr clips za Waziri wetu akizungumza kiingereza.

Kwa kifupi tu Waziri wetu kaharibu mbaya. Ile clip ikienda viral ni aibu sana 😅. Kile kiingereza kitatuaibisha sana kama Taifa. Ni broken isiyovumilika.

Mwisho jamani nafasi za Uwaziri ni kubwa sana. Hawa ni watu wanao negotiate deals kwa faida ya nchi. Wanaosimama kwenye international platforms kuwakilisha nchi. Jamaniii tuteue watu wenye uwezo hata wa kuzungumza hizi lugha kubwa za kigeni kama kiingereza kwa ufasaha.

Poleni Tanzania. Ni aibu
Kwanini asiongee kiswahili fasaha, halafu mkalimani akafanya kazi yake?

Mbona wachina wanapenda kuongea na wageni kwa kutumia lugha yao?
Kwanini tunakinyanyapaa kukiongea kiswahili?

Siwezi kumlaumu ama kumcheka Waziri kutokana na mfumo mbovu wa ufundishaji wa lugha ya kingereza nchini Tz.
 
Kwa aibu niliyojiskia leo baada ya kusikiza Kiingereza cha Waziri Ulega akizungumza na Wakandarasi Wachina wanaojenga barabara ya mwendokasi huko Mwenge leo nakuomba tu Msemaji wa Serikali zungumza na Waandishi wa habari na waombe tu wasirushe zilr clips za Waziri wetu akizungumza kiingereza.

Kwa kifupi tu Waziri wetu kaharibu mbaya. Ile clip ikienda viral ni aibu sana 😅. Kile kiingereza kitatuaibisha sana kama Taifa. Ni broken isiyovumilika.

Mwisho jamani nafasi za Uwaziri ni kubwa sana. Hawa ni watu wanao negotiate deals kwa faida ya nchi. Wanaosimama kwenye international platforms kuwakilisha nchi. Jamaniii tuteue watu wenye uwezo hata wa kuzungumza hizi lugha kubwa za kigeni kama kiingereza kwa ufasaha.

Poleni Tanzania. Ni aibu
Tuwekee na clip ya kingereza walicho ongea wachina hapo
 
Mwisho jamani nafasi za Uwaziri ni kubwa sana. Hawa ni watu wanao negotiate deals kwa faida ya nchi. Wanaosimama kwenye international platforms kuwakilisha nchi. Jamaniii tuteue watu wenye uwezo hata wa kuzungumza hizi lugha kubwa za kigeni kama kiingereza kwa ufasaha.
Kwahiyo unataka watu wateuliwe kwa kigezo cha lugha ya kingereza na sio uwezo wao kwenye utendaji?

Anyway, wawe wanatembea na wakalimani ili mambo yasiwe mengi.
 
Wewe mwenyewe unakiweza kingereza au ni wale wale wenye kupenda kucheka lugha za watu?.

Unaweza ukawa unaongea kingereza cha mfalme George wa UK halafu unachunga ng'ombe wa Babu zako kijijini kwenu, unaweza ukawa hujui kingereza vizuri lakini ukawa tajiri mwenye kufanya biashara kubwa za kidunia.
Hata kumbe huna uelewa wa hoja ya mleta uzi.
Kwa watu kama mawaziri lazima tuwe na watu ambao wapo vizuri kichwani, ukijumlisha na lugha ya kiingereza kwani ndio wanaoingia mikataba kwa niaba ya wizara na nchi.

Kipimo cha mafanikio sio utajiri.
Kila mmoja ana kipimo chake cha mafanikio kulingana na mtazamo wake kuhusu mafanikio.
 
Kwani kiingereza ni intelligence ya mtu au ni lugha tu kama kiswahili, mbona wa Japan wengi hawajui kiingereza..........hizo ndo comment za watanzania walio shindwa kumudu lugha ya kiinaereza.
Kulinganisha japan na tanzania sio sahihi mkuu, sisi tanzania huko serikalini english ni lugha walioamua kuikumbatia katika sehemu mbalimbali. Hivo tukiwaona viongozi wanavochemka sisi tunafurahi
 
Wewe unaejua kingereza unamzidi 🥶uwezo wako kung'amua mambo ni mdogo sana
 
Back
Top Bottom