Waziri Ummy: CoronaVirus bado ipo, tuendelee kuchukua tahadhari

Waziri Ummy: CoronaVirus bado ipo, tuendelee kuchukua tahadhari

Watu wenye Corona hawaendi hospital maana wananyanyapaliwa. Wengi wako nyumbani wanatumia asili. Ninavyoandika hapa amezikwa shemeji huko Moshi alikufa Corona huko kanda ya ziwa. Jumatano wiki hii anazikwa mwingine huko Marangu na mwili utapelekwa na watu wa afya kutoka Arusha. Mwingine atazikwa Rombo Ijumaa hii mwili utatolewa Moshi. Je serikali inayo taarifa kamili za hali ya ugonjwa nchini? Watanzania tuchukue tahadhari Korona ipo na inaenda kasi sana. Vaa barakoa , kula virurubisho, piga nyungu, epuka mikusantiko. Cha kusikitishaha toka ile tarehe 24 May walipotangaza hali si mbaya wagonjwa wamebaki 9 basi 99% ya watanzania wameyarudia maisha ya kawaida. Life ni kama kawaida vijiweni mpaka daladala hakuna barakoa tena. Soko la Temeke Stereo nilipata hata yale mtanki ya maji ya kunawa hayana maji muda mrefu sana. Nihatari sana hii.
Amezikwa makaburi ya wapi mkuu?Amezikwa lini? Niko maeneo haya.
 
Ni lazima tujiandae kisaikolojia kupokea matokeo ya "herd immunity" ambayo serikali imeona ndiyo njia bora na sahihi ya kukabiliana na hili gonjwa la kutisha na kuambukiza la COVID-19. Tatizo ubaya wake unakuja kutokana na watu wengi kuaminishwa kuwa siyo tena tishio, ama pia lipo kwa kiwango cha chini sana hapa nchini.
 
Kweli koona kwishiney, kuna wahudumu wawili wa kibaha nimewaona wamerudi kwenye vituo vyao
 
Hivi inawezekana ikawa tumetumia mbinu gani kulishinda hili janga hivi, Kwa mbinu yoyote tuliyotumia kwanini tusi share na ulimwengu ili kunusuru dunia na hili janga

Sent using Jamii Forums mobile app

Dawa ya Corona ipo Tanzania, tatizo wazungu hawathamini dawa zetu wacha wafe kama inzi.

 
Ulimwengu walidharau sana.Wasipotubu kwa dhihaka zao kipindi kile taifa letu linamlilia Mungu,sasa si waendelee kutumia hizo mbinu za kisayansi walizosema sisi tumeziacha.Hii kitu itawasumbua sana.wacha sisi tuendelee kupiga kazi.Watanzania pigeni kazi kipindi cha kutajirika ndiyo hiki.majirani watakuwa na njaa.mitaji yao itakuwa imekata by the time wanapata akili
Tuombe Tena ili tuondoe umaskini
 
Ni lazima tujiandae kisaikolojia kupokea matokeo ya "herd immunity" ambayo serikali imeona ndiyo njia bora na sahihi ya kukabiliana na hili gonjwa la kutisha na kuambukiza la COVID-19. Tatizo ubaya wake unakuja kutokana na watu wengi kuaminishwa kuwa siyo tena tishio, ama pia lipo kwa kiwango cha chini sana hapa nchini.
Herd immunity inatia shaka kwani kule China na Itally kuna watu waliumwa halafu wakapona na wakapata maambukizi tena.Hapo inaleta mashaka kuwa huenda mtu aliyepona hajajengewa kinga ya kutosha, hivyo njia hii ya kinga ya kundi haina uhakika.
 
Waambieni madereva wa ambulance wawe wanazima ving'ora!

Maana si kwa kupisha huku.
Bila shaka ving'ora vya ambulance vilikuwepo hata kabla ya janga hili la CORONA kuikumba nchi yetu. Hiyo idadi iliyotajwa ni wagonjwa waliopo mahospitali, na hospitalini ndipo tunapopatia takwimu ya wagonjwa wa corona, waliopo majumbani na mitaani hatuna mpango nao, watakapokuja hospitali tutatoa taarifa zao, ndiyo maana akasema tuwe makini, corona ipo na tuendelee kuchukua tahadhari.
 
Amezikwa makaburi ya wapi mkuu?Amezikwa lini? Niko maeneo haya.
Fuatilia kifo cha Wakili Jack Mrema ndiyo alifia kanda ya Ziwa huko Bukoba. Mwingine ni huko Marangu Jumatano hiii mwili ikitokea Arusha na mwingine ni Rombo makaburi ya Watawa Huruma Convent mwili ukitokea Moshi mjini.
 
Back
Top Bottom