Jumatano ni mbali sanaLazima tuvunje rekodi ya Afrika Mashariki, kuna sehemu tumekosea, Hii kasi ni ya kipekee, na sioni kama kuna Tahadhari kubwa saana ya kuiepuka, hadi imefikia waumini wameanza kuamua wenyewe kwa wenyewe kuzuia wenzao wakae majumbani, hivyo basi kifuatacho kufikia Jumatano ijayo tutakuwa tunaongoza Afrika Mashariki...nategemea Juma tatu au Jumanne kuwepo kwa tamko gumu kuliko yote kutoka Serikali, hebu tujiulize, ni wapi tumekosea hadi kufikia huku tuelekeako?
Sent using Jamii Forums mobile app
Waliokufa si watu?
"corona ipo tuchukue tahadhari"
Lile jitu la EquadorLazima tuvunje rekodi ya Afrika Mashariki, kuna sehemu tumekosea, Hii kasi ni ya kipekee, na sioni kama kuna Tahadhari kubwa saana ya kuiepuka, hadi imefikia waumini wameanza kuamua wenyewe kwa wenyewe kuzuia wenzao wakae majumbani, hivyo basi kifuatacho kufikia Jumatano ijayo tutakuwa tunaongoza Afrika Mashariki...nategemea Juma tatu au Jumanne kuwepo kwa tamko gumu kuliko yote kutoka Serikali, hebu tujiulize, ni wapi tumekosea hadi kufikia huku tuelekeako?
Sent using Jamii Forums mobile app
Tuseme InShaAllahNinachofurahi wagonjwa hawafi wengi wanapona
Corona itaisha Ndani ya muda mfupi
Sent using Jamii Forums mobile app
Corona haina lumumba Wala ufipa ikipiga ina piga tu chukua tahadhari mwenyewe fuata mashariti na taratibu za kujikinga ukiona vp jifungie na familia yako ndani kulaumu hovyo hovyo sio kinga ya Corona hao hao unao watumikia wanachukua tahadhari na familia zaoEndeleeni kuficha ugonjwa. Wakiupata watu kadhaa hapo Lumumba mtatia akili.
Anadhani Kinga ya Corona Ni kulaumu hovyo hovyo mwache akeshe jf akilaumu Corona haichagui huyu Ni lumumba au huyu ufipaHivi huu ugonjwa unafichika?
Hapo unapokaa kuna mgonjwa yetote? Au umeshuhudia mtu yeyote akisema ana ndugu yake anaumwa corona?
Sent using Jamii Forums mobile app
Siasa ipi walio ileta hebu oredhesha hapa tujue hizo siasa walizo ziletaAtakapoanza kuugua waziri ndio mtajua hii sio movie ya kibongo
Mmejawa na kiburi na uongo mwingi kwa sababu ya mtu mmoja hivi
Ummy sijui utawaambia nini WaTz tukianza kwanza tumeanza kuzikana
Covid-19 Tz ipo kila mahali
Mnaleta siasa kwenye uhai wa watu
Uzuri huyu virus hana uchaguzi ni wote kwa wote
Wakusanya watu akina bashite na wengineo muanze kujiandaa
Punguzeni viburi
Si uende na wewe kijijini kwenu au huna kwenuAlafu yeye akakimbia kijijini kwao
Waziri wa Afya Ummy Mwalimu akiongea na viongozi wa dini, amesema kuwa kwa sasa hali ya ugonjwa wa Korona nchini imebadirika kutoka kuletewa ugonjwa na watu kutoka nje imegeuka kuwa hali ya kuambukizana sisi wenyewe kwa wenyewe.
Wakati huo Waziri Ummy ameonya kuwa ndani ya muda mfupi ujao maambukizi yatageuka kuwa maambukizi ya jumuia(Community Transmission), akawataka watanzania wajiandae kwa hali hiyo.
MY TAKE:
Tuliwaambia mapema kabisa, Fungeni hii mipaka ya nchi mtatuletea janga, lakini tukaendelea kujivutavuta sasa tunakwenda kwenye hali ngumu sana
Tumeona juzi hapa mtu katoka Dubai tarehe 24 March kashuka Dar, kisha tukasikia kaenda mwanza tarehe 29 March alipopimwa na kukutwa na Korona, huyu mtu ilikuwaje hakuwekwa karantini?
Kwa hiyo ina maana Kwenye Karantini hatukuwa serious na pia kwenye kufunga borders hatukuwa serious, sasa matokeo yake huenda tukaingia kwenye hali ngumu
Kiufupi serikali haiwezi kukwepa lawama hali ikigeuka na kuwa mbaya nchini.
Saa hivi hao wachina tuliokuwa tukiwapokea kwa bashasha pale KIA kipindi wapo kwenye hali ngumu sasa hivi wamefuta residence permit na viza za foreigners walio nje ya mipaka ya nchi yao na wanawasumbuasumbua foreigners walio nchini mwao kwa sasa kwa kuwabagua na kuwafanyia kila aina ya ubaguzi kuwa eti ndo wanawapelekea New cases, Wanawanyima hoteli, kuingia kwenye supermarkets,Weusi wakipanda mabasi wachina wanashuka. Sasa najiuliza Je sisi wema wetu wa kufungua mipaka kipindi kile umetuletea nini zaidi ya kuhatarisha maisha ya watu wetu?
Msikilize Ummy Mwalimu hapa akiongea
View attachment 1413820
hao unao watumikia wanachukua tahadhari na familia zao