Waziri wa Afya Ummy Mwalimu akiongea na viongozi wa dini, amesema kuwa kwa sasa hali ya ugonjwa wa Korona nchini imebadirika kutoka kuletewa ugonjwa na watu kutoka nje imegeuka kuwa hali ya kuambukizana sisi wenyewe kwa wenyewe.
Wakati huo Waziri Ummy ameonya kuwa ndani ya muda mfupi ujao maambukizi yatageuka kuwa maambukizi ya jumuia(Community Transmission), akawataka watanzania wajiandae kwa hali hiyo.
MY TAKE:
Tuliwaambia mapema kabisa, Fungeni hii mipaka ya nchi mtatuletea janga, lakini tukaendelea kujivutavuta sasa tunakwenda kwenye hali ngumu sana
Tumeona juzi hapa mtu katoka Dubai tarehe 24 March kashuka Dar, kisha tukasikia kaenda mwanza tarehe 29 March alipopimwa na kukutwa na Korona, huyu mtu ilikuwaje hakuwekwa karantini?
Kwa hiyo ina maana Kwenye Karantini hatukuwa serious na pia kwenye kufunga borders hatukuwa serious, sasa matokeo yake huenda tukaingia kwenye hali ngumu
Kiufupi serikali haiwezi kukwepa lawama hali ikigeuka na kuwa mbaya nchini.
Saa hivi hao wachina tuliokuwa tukiwapokea kwa bashasha pale KIA kipindi wapo kwenye hali ngumu sasa hivi wamefuta residence permit na viza za foreigners walio nje ya mipaka ya nchi yao na wanawasumbuasumbua foreigners walio nchini mwao kwa sasa kwa kuwabagua na kuwafanyia kila aina ya ubaguzi kuwa eti ndo wanawapelekea New cases, Wanawanyima hoteli, kuingia kwenye supermarkets,Weusi wakipanda mabasi wachina wanashuka. Sasa najiuliza Je sisi wema wetu wa kufungua mipaka kipindi kile umetuletea nini zaidi ya kuhatarisha maisha ya watu wetu?
Msikilize Ummy Mwalimu hapa akiongea
View attachment 1413820