Waziri Ummy nashauri ukae na wataalamu wa afya kabla ya tamko la bei ya huduma za afya

Waziri Ummy nashauri ukae na wataalamu wa afya kabla ya tamko la bei ya huduma za afya

jingalao

JF-Expert Member
Joined
Oct 12, 2011
Posts
36,197
Reaction score
29,717
Nampongeza Waziri wa Afya kwa kupata updates mbalimbali za sekta unayoisimamia kwa wakati na hivyo kuwa responsive.

Nikijikita katika mada,

Mimi ni muumini wa sustainable health system financing yaani sekta ya afya inahitaji njia endelevu ya rasilimali fedha ili iweze kuleta tija. Mfumo wa afya nchini kama ilivyo nchi nyingi maskini bado inategemea uhisani wa marekani na mataifa mengine, hii ni hatari kwa usalama na ustawi wa Taifa. Yaani siku tukimchukiza Marekani, Uingereza au Japan tunarudi miaka 50 nyuma, hili ni jambo hatari.

Bado bajeti ya sekta ya afya ni changa mno yaani haijafikia 15% ya GDP Kama ilivyowahi kuazimiwa huko Abuja. Hivyo sekta ya afya inaidai serikali deni la kufulfill hiyo asilimia ili angalau kutoa huduma.

Bado Serikali haitoi ruzuku stahiki sawia na hitajika kwenye huduma za afya ukilinganisha na sekta nyingine mfano Elimu. Ukihitaji mifano fanya mapitio ya uwekezaji katika huduma za afya vs huduma nyingine (fanya rejea kwenye bajeti ya huduma za jamii bungeni kwa miaka 10).

Sekta ya afya imejitahidi kuja na bunifu mbalimbali ili kuwezesha upatikanaji wa rasilimali fedha ili iinuke,
hapo utaona in recent 7 years or so kumekuwa na mabadiliko chanya.

Nikiri kuwepo kundi la wahuni na wafanyabiashara walioanza kujitokeza kwenye sekta ya afya wenye nia ya kubadili sekta hii kutoka katika utoaji huduma na kuwa bisashara (hii ni kwenye sekta binafsi na mashirika ya dini sio public). Kamwe sikubaliani na dhana hii ya wahuni kwani imeprove failure hata Marekani.
HIVYO NI LAZIMA WADHIBITIWE!

Lipo jambo la kisera ambalo Wizara ya Afya inalikwepa kwepa na kuishia kuja na matamko ya taharuki.
Jambo hili niliwahi kulisemea humu humu jamvini, na niliwahi kuliulizia katika moja ya midahalo ya wagombea urais miaka kadhaa imepita. Jambo hilo sio lingine bali ni bima ya afya kwa wote. Mh. Rais Samia Suluhu Hassan wakati anaingia madarakani na alipokuwa anawaapisha mawaziri wake awamu ya awali kabisa aliwaagiza Wizara ya Afya kuja na Sera ya Bima ya Afya kwa wote. Alisisitiza swala hilo lichakatwe na kufikia mwisho lakini hadi sasa hakuna draft yoyote iliyowasilishwa bungeni badala yake tunaona purukushani za majukwaani. HII SIO SAWA.

Consultation fee ni sehemu muhimu ya ada za kumuona ,kumsikia na kupata ushauri wa daktari (sio kumuona daktari tu). Unapoingia chumba cha daktari yapo mengi yanayofanyika kabla ya kwenda kwenye vipimo n.k.

MAONI
Sekta ya afya imevamiwa na ngwini wengi sana, na ngwini hawa waemkuwa wasemaji sana huku uwezo wao ukiwa mdogo.

Kuna tatizo la wasaidizi wa madaktari, yaani ukianzia wauguzi, wafamasia, wateknolojia wa maabara nk, ambao baada ya kupewa fursa wameanza kupeleka umbea kwa viongozi badala ya kutoa ushauri kuntu.

Pia naamini madhila mengi ambayo umeyatolea ufafanuzi yanatokana na sekta binafsi na mashirika ya dini. Basi ni muhimu kurusha jiwe katika eneo husika na sio kwa public sector. Rationing ya bei ianzie sekta binafsi.

Mhe. Waziri tumia vyanzo sahihi kupata genuine challanges na solutions katika sekta ya afya. Nashauri ukipata fursa au ukiamua kutengeneza fursa hebu waite waganga wafawidhi wa zahanati, vituo vya afya na hospitali (ngazi ya msingi) upate maoni yao ili kuja na Sera bora.​

KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA!
 
Dah sektahii ya Afya ni muhimu sana hatutakiwi kuichezeachezea
 
Mtoa mada, iwapo maelezo Yako yatakosa vigezo vifuatavyo basi maelezo Yako yatakosa uhalali:

Je, ni kweli ukisemacho?
Je, ni mambo mazuri?
Je, hayo maelezo yana umhimu?
 
Mtoa mada, iwapo maelezo Yako yatakosa vigezo vifuatavyo basi maelezo Yako yatakosa uhalali:

Je, ni kweli ukisemacho?
Je, ni mambo mazuri?
Je, hayo maelezo yana umhimu?
Subiri wengine wamalize kuchangia tutathmini
 
Hospital za Umma consultation fee ya Kazi hasa? Wanalipwa salary kwa Kodi ya umma kwa ajili gani hasa?

Na hiyo fee si inaenda Serikalini au kwa daktari binafsi? Kama inaenda Serikalini kuna shida gani serikali kuipiga chini kama ilivyofanya kwenye ada ya Elimu?

Mwisho swala la Bima ya Afya litakuja,ni kuandaa mfuko maalumu wenye chanzo maalumu cha fedha na Mchango wa Wananchi..

Mathalani tunaweza weka tozo hizi za Simu nk ndio zikafanya Kazi ya Bima.
 
Hospital za Umma consultation fee ya Kazi hasa? Wanalipwa salary kwa Kodi ya umma kwa ajili gani hasa?

Na hiyo fee si inaenda Serikalini au kwa daktari binafsi? Kama inaenda Serikalini kuna shida gani serikali kuipiga chini kama ilivyofanya kwenye ada ya Elimu?

Mwisho swala la Bima ya Afya litakuja,ni kuandaa mfuko maalumu wenye chanzo maalumu cha fedha na Mchango wa Wananchi..

Mathalani tunaweza weka tozo hizi za Simu nk ndio zikafanya Kazi ya Bima.
Tuna options mbili tu
1-Kulipia huduma za Afya kama nyinginezo(Tulipe cash kwa gharama za juu au bima kwa wote kwa gharama za kushare )

2-Huduma bure kwa hisani ya Serikali ya Tanzania.

HIZI NDIO OPTIONS ZA KISERA OTHETWISE TUTADANGANYANA TU
 
KUNA TATIZO LA WASAIDIZI WA MADAKTARI YAANI UKIANZIA WAUGUZI,WAFAMASIA,WATEKNOLOJOA WA MAABARA N.K AMBAO BAADA YA KUPEWA FURSA WAMEANZA KUPELEKA UMBEA KWA VIONGOZI BADALA YA KUTOA USHAURI KUNTU.

Tangu lini hizo kada zimekuwa wasaidizi wa madaktari, hizo ni independent kada na wala daktari hana mamlaka yoyote kwao.

Shida hamtaki usawa kwenye hii sekta, inabidi mkubali nyakati zimebadilika, hatuko enzi za kupelekeshana tena. Yani nyie kuambiwa consultation fee itolewe ndiyo imekuwa nongwa?[emoji23]

Mama Samia ana nia nzuri na watanzania, hivi kwa nini mtu alipie pesa kumuona mtu fulani ambaye ameajiriwa na serikali na analipwa mshahara? Kwa kigezo kipi yani.


Wake up, dont sleep, dont sleep, we are approaching next era my friend[emoji2733]
 
Tangu lini hizo kada zimekuwa wasaidizi wa madaktari, hizo ni independent kada na wala daktari hana mamlaka yoyote kwao.

Shida hamtaki usawa kwenye hii sekta, inabidi mkubali nyakati zimebadilika, hatuko enzi za kupelekeshana tena. Yani nyie kuambiwa consultation fee itolewe ndiyo imekuwa nongwa?[emoji23]

Mama Samia ana nia nzuri na watanzania, hivi kwa nini mtu alipie pesa kumuona mtu fulani ambaye ameajiriwa na serikali na analipwa mshahara? Kwa kigezo kipi yani.


Wake up, dont sleep, dont sleep, we are approaching next era my friend[emoji2733]
Kada zote hizo zimeletwa na kada hiyo muhimu ,hiyo ni fact....daktari anayajua yote ya waliobakia ...hutaki soma
 
Hospital za Umma consultation fee ya Kazi hasa? Wanalipwa salary kwa Kodi ya umma kwa ajili gani hasa?

Na hiyo fee si inaenda Serikalini au kwa daktari binafsi? Kama inaenda Serikalini kuna shida gani serikali kuipiga chini kama ilivyofanya kwenye ada ya Elimu?

Mwisho swala la Bima ya Afya litakuja,ni kuandaa mfuko maalumu wenye chanzo maalumu cha fedha na Mchango wa Wananchi..

Mathalani tunaweza weka tozo hizi za Simu nk ndio zikafanya Kazi ya Bima.

Nitazungumzia kitu kimoja hapa. Umefikiria kama bei gharama ya sahani ya wali ingekuwa inahumuisha kodi ya gesi, kodi ya mchele, mshahara wa mpishi, bei ya sahani, kijiko na bakuli?? Je ingekuwa na bei gani?

Wanachojaribi kufanya ni kupunguza tozo katika cost points zinazofuatia kama maabara, madawa, kulala na kadhali. Je unaona ni sawa kama mtu anayefanya x-ray ndio angekuwa akilipia huduma hiyo akifidia na maabara, kitanda nk sehemu ambazo anaweza kuwa hakufika??

Ni kumwona daktari pekee ndio kila mtu atapita na hivyo ni sahihi hiyo kuwa point of sale!! Au unataka mtu aende kumwona daktari halafu awe amepewa hata ushauri baada ya kugundulika hana maradhi, bure???
 
Mleta mada kada za afya zote zinafanya kazi kwa kushirikiana sio kumsaidia daktari.

Naungana na wewe kuhusu kuwa na financing sustainability katika secta ya afya.

Kuhusu bima ya afya kwa wote serikali iwe makini sana mzigo huo ni mkubwa sana kwa uchumi wetu..

Kumbuka pia ina mzigo mkubwa sana wa elimu bure.

#MaendeleoHayanaChama
 
Kwenye consultation fee, kama wanaona haina umuhimu, basi wawatafute clinical officers au nurses wawe wanatoa matibabu.
 
Nape akae ajifunze kwa wenzake namna bora ya kuwa kiongozi na mtumishi bora wa umma.
 
Nitazungumzia kitu kimoja hapa. Umefikiria kama bei gharama ya sahani ya wali ingekuwa inahumuisha kodi ya gesi, kodi ya mchele, mshahara wa mpishi, bei ya sahani, kijiko na bakuli?? Je ingekuwa na bei gani?

Wanachojaribi kufanya ni kupunguza tozo katika cost points zinazofuatia kama maabara, madawa, kulala na kadhali. Je unaona ni sawa kama mtu anayefanya x-ray ndio angekuwa akilipia huduma hiyo akifidia na maabara, kitanda nk sehemu ambazo anaweza kuwa hakufika??

Ni kumwona daktari pekee ndio kila mtu atapita na hivyo ni sahihi hiyo kuwa point of sale!! Au unataka mtu aende kumwona daktari halafu awe amepewa hata ushauri baada ya kugundulika hana maradhi, bure???
Hizo gharama za x ray,kitanda,nk tunalipia kama kawaida..

Hoja inabakia pale pale,tulipoe consultation fee ya Kazi gani? Salary ni ya Kazi ipi kama sio kununua huo itaalamu wao?
 
Kuna baadhi ya wizara Waziri husika anapaswa kuwa mwenye taaluma na weledi wa taaluma husika badala ya kuokota na kumuweka yeyote.

Hii inapaswa kuwekwa kwenye Katiba kabisa.
 
Hata CEOs wa taasisi nyingine za Umma wanapaswa kutokana na Uzoefu wa operations za shughuli za kwenye taasisi husika na sio kuleta wageni na kuwafanya ma-CEOs inachelesesha utendaji kazi wenye tija.

Inabidi atumie muda mrefu kuanza ku-get familiarized na kujifunza kisha kuelewa organ structure, malengo, kuweka mikakati, mpaka kujaribu kuanza kuelewa miaka 2-3 imekatika! [emoji848][emoji848]

Kweli tuko siriasi kuwaletea maendeleo waTZ ?
 
Kada zote hizo zimeletwa na kada hiyo muhimu ,hiyo ni fact....daktari anayajua yote ya waliobakia ...hutaki soma
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Yeah I knew unazunguka tuu, na bado mtazidi kuteseka na hizo grandiosity zenu mpaka mfe.

Mtake msitake hizo ni independent profesions na zina miongozo yao ya uendeshaji.
 
Ila wakati wa korona hatukusema walipwe au waslipwe consultation naomba mungu isitokee tena
 
Nampongeza Waziri wa Afya kwa kupata updates mbalimbali za sekta unayoisimamia kwa wakati na hivyo kuwa responsive.

Nikijikita katika mada,

Mimi ni muumini wa sustainable health system financing yaani sekta ya afya inahitaji njia endelevu ya rasilimali fedha ili iweze kuleta tija. Mfumo wa afya nchini kama ilivyo nchi nyingi maskini bado inategemea uhisani wa marekani na mataifa mengine, hii ni hatari kwa usalama na ustawi wa Taifa. Yaani siku tukimchukiza Marekani, Uingereza au Japan tunarudi miaka 50 nyuma, hili ni jambo hatari.

Bado bajeti ya sekta ya afya ni changa mno yaani haijafikia 15% ya GDP Kama ilivyowahi kuazimiwa huko Abuja. Hivyo sekta ya afya inaidai serikali deni la kufulfill hiyo asilimia ili angalau kutoa huduma.

Bado Serikali haitoi ruzuku stahiki sawia na hitajika kwenye huduma za afya ukilinganisha na sekta nyingine mfano Elimu. Ukihitaji mifano fanya mapitio ya uwekezaji katika huduma za afya vs huduma nyingine (fanya rejea kwenye bajeti ya huduma za jamii bungeni kwa miaka 10).

Sekta ya afya imejitahidi kuja na bunifu mbalimbali ili kuwezesha upatikanaji wa rasilimali fedha ili iinuke,
hapo utaona in recent 7 years or so kumekuwa na mabadiliko chanya.

Nikiri kuwepo kundi la wahuni na wafanyabiashara walioanza kujitokeza kwenye sekta ya afya wenye nia ya kubadili sekta hii kutoka katika utoaji huduma na kuwa bisashara (hii ni kwenye sekta binafsi na mashirika ya dini sio public). Kamwe sikubaliani na dhana hii ya wahuni kwani imeprove failure hata Marekani.
HIVYO NI LAZIMA WADHIBITIWE!

Lipo jambo la kisera ambalo Wizara ya Afya inalikwepa kwepa na kuishia kuja na matamko ya taharuki.
Jambo hili niliwahi kulisemea humu humu jamvini, na niliwahi kuliulizia katika moja ya midahalo ya wagombea urais miaka kadhaa imepita. Jambo hilo sio lingine bali ni bima ya afya kwa wote. Mh. Rais Samia Suluhu Hassan wakati anaingia madarakani na alipokuwa anawaapisha mawaziri wake awamu ya awali kabisa aliwaagiza Wizara ya Afya kuja na Sera ya Bima ya Afya kwa wote. Alisisitiza swala hilo lichakatwe na kufikia mwisho lakini hadi sasa hakuna draft yoyote iliyowasilishwa bungeni badala yake tunaona purukushani za majukwaani. HII SIO SAWA.

Consultation fee ni sehemu muhimu ya ada za kumuona ,kumsikia na kupata ushauri wa daktari (sio kumuona daktari tu). Unapoingia chumba cha daktari yapo mengi yanayofanyika kabla ya kwenda kwenye vipimo n.k.

MAONI
Sekta ya afya imevamiwa na ngwini wengi sana, na ngwini hawa waemkuwa wasemaji sana huku uwezo wao ukiwa mdogo.

Kuna tatizo la wasaidizi wa madaktari, yaani ukianzia wauguzi, wafamasia, wateknolojia wa maabara nk, ambao baada ya kupewa fursa wameanza kupeleka umbea kwa viongozi badala ya kutoa ushauri kuntu.

Pia naamini madhila mengi ambayo umeyatolea ufafanuzi yanatokana na sekta binafsi na mashirika ya dini. Basi ni muhimu kurusha jiwe katika eneo husika na sio kwa public sector. Rationing ya bei ianzie sekta binafsi.

Mhe. Waziri tumia vyanzo sahihi kupata genuine challanges na solutions katika sekta ya afya. Nashauri ukipata fursa au ukiamua kutengeneza fursa hebu waite waganga wafawidhi wa zahanati, vituo vya afya na hospitali (ngazi ya msingi) upate maoni yao ili kuja na Sera bora.​

KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA!
Unampongeza kwa lipo .watu waliosoma kipindi cha ujamaa wanashida sana
 
Kuna baadhi ya wizara Waziri husika anapaswa kuwa mwenye taaluma na weledi wa taaluma husika badala ya kuokota na kumuweka yeyote.

Hii inapaswa kuwekwa kwenye Katiba kabisa.
True hata mimi naona huyu mama kwenye hii secta anapwaya sana anataka kuendesha NHIF kijamaa ,na matamko mbali mbali
 
Kada zote hizo zimeletwa na kada hiyo muhimu ,hiyo ni fact....daktari anayajua yote ya waliobakia ...hutaki soma
Hapa unayumba mzee, hakuna kada muhimu juu ya nyingine. Kama umesoma na hukufundishwa au hujui kwa nini Kuna separation ya majukumu katika kada hizi basi wewe ni jipu.

Sent from my TECNO BA2 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom