Waziri Ummy, Usipotoshwe maamuzi yako kuhusu ADDO na wafamasia mtawaumiza Watanzania

Umejenga hoja vizuri sana. Unatengeneza vipi dawa bila kujua magonjwa kwa kina? Nafikiri huu mjadala utasaidia kuweka standards na kuondoa huu mkanganyiko.
Yani anataka utengeneze dawa za Migrainw alafu anakuja kuliaa huku Mfamasia hajui magonjwaaa sasa hizo dawa zinatengenezwa na mtu asiejua ugonjwa????
 
Kwenye hiyo App hata walevi nao watakuwa na Parkinsonisim[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
Hahaaaaaa. Nadhani app ni Kwa ajili ya kuonesha dalili, Kisha mtu aende hospital kwa vipimo zaidi. App inasoma namna sehemu ya nyonga inavyoenda juu na chini.
 
Kazi mojawapo ya Mfamasia ni Drug design and development, au kazi ndogo tu ya Compounding

Muulize MD kama ana ABC eneo hili ili ujue kama kweli anaweza kufanya kila jukumu la mfamasia
Kuna daktari alimuandikia mtoto captopril 0.13mg tds 1/12..lakini alikuwa hajui dose hii itapatikanaje ikiwa kidonge kina 25mg..jasho lilimtoka...akaja pharmacy kuuliza akajibiwa tuachie hiyo ni kazi yetu.

Wanaume wakaingia kufanya compounding..wakapiga kitu cha dilution (c1v1=c2v2) wakapata hiyo dose ya 0.13mg kwa kutengeneza syrup...kitu kidogo tu fasta,lakini hawawezi,how wataweza kufanya kazi zote za wataalamu wa dawa?

Sasa huyu jamaa anayesema daktari anaweza kufanya kazi ya Pharmacist sijui anadhani ni pale kusoma prescription na kutoa dawa au..kitu ambacho hata mfamasia hafanyi amewaachia technicians na assistants.
 
Maana yake tumesome medical store peke ake ?

Hii sio sahihi "Kumsaidia nesi na doctor kutunza dawa store na kuzisambaza"
 
Umetoa maoni mazuri sana daktari ila mimi nafikiri ADDO ndio suluhisho ila sasa hii ADDO isiwe certification bali iwe ni kozi maalum ambayo inasomewa chuo kwa ajili ya kufanya kazi katika haya maduka ya dawa muhimu ni iwe na cimbination ya Diagnosis pamoja na dispensing.Na ifundishwe kwa ithibati inayoeleweka kwa ngazi ya Certificate,Diploma na Degree.
 
sawa mkuu nimelisha ubongo kitu asbh hii.
 
Hata mim nimeshangaa sana...kwamba njee ya hospital daktari hajui dawa!!!!

Mim nitibiwena daktari na sio pharmacist
 
Hapa naona grandiosity kati ya wafamasia na madaktari..mfamasia anajiona yeye ndo anaweza kutoa dawa na kutibu kwakua ana basic knowledge ya physiology,bio chem etc na Dr anajiona anaweza kuwa mafamasia kwakua ana basic knowledge ya pharmacology kadhalika nurses na watu wa maabara …mfamasia anaamini anajua magonjwa yoote na anajua dawa zoote wkt ni utopolo tu..Dr anadhan anajua dawa zoote(from adv eff ,interactions etc kuliko mfamasia nao ni utopolo tu..kuna forum flan huko telegram kulikua na mtifuano mkali sana kati nurses na Dr maana nurses wanaona wanajua everything na Dr nao wanadai nurses sio issue wanaweza kufanya kaz kama ma Dr na ma nesi pia aisee ilikua issue..
My take..kujua anatomy,physiology haikufanyi ww kuwa Dr maana hata radiographer wanasoma hayo masomo na pia kusoma basic pharmacology hakukufanyi wewe kua pharmacist maana hata nurses wanasoma pharmacology..kila mmoja akae kwenye nafasi yake Dr ona mgonjwa fanya vpimo na toa dawa..watu wa madawa watoe dawa kama kuna contradiction wawasilinae kupata muafaka maana jopo la ma Dr wanaweza kukaa kwenye clinical meeting zao hasa za specific departments ambapo wakaamua mgonjwa X aanze dawa flan so kama mfamasia anaona kuna walakin aonane na wahusika kwa clarification na sio kusema Sitoi daqa kwakua dawa x na Z zina interact au dawa hii ni contraindicated kwa mgonjwa huyu u never know labda walikaa waka outweigh risk ya ugonjwa over side effects za dawa so kukaa pamoja mkaangalia namna ya kumsaidia mgonjwa ndo la msingi..kwa ufupi mfamsia si Dr hata kama anajua BAADHI ya diagnosis ya magonjwa kwa maana hawez kujua kila kiu kamwe hahaha au sio mzee wa famasi unaweza kufanya reduction ya colles # kwakua unajua anatomy..!na Dr si mfamasia kwakua hawez kujua kila kitu kuhusu madawa maana kila mtu kaingia deep kwenye masomo yake..EVERY MEDICAL PERSONNEL WANNA BE A DOCTOR [emoji1788]
 
Every medical personnel wants to be a doctor?...Stop this nonsense aisee.
 
Kwa binadamu tuna MD

Kwa mifugo tuna Veterinary Doctor wazee wa SUA bachelor of veterinary medicine

Pharmacist kwenye mifugo siwaoni in field zaidi ya kwenye viwanda vya dawa za mifugo

Bado siwezi kupewa prescription na pharmacist Bora anipe nurse kama MD hayupo
 
Busara ingekuelekeza kujibu hoja badala ya kumshambulia kibinafsi. Nakushauri shambulia hoja yake kwa kuonesha yalipo mapungufu ya hoja yake bila kutafuta namna ya kumshusha hadhi yake.
 
Mna uhakika ili andiko limetoka kwa Prof?
 
Umeandika vizuri ila mwishoni hapo Umeharibuu not everbody want to be a Dr but Dr want to be everybody...[emoji3][emoji3]
 
Ndugu madaktari,

Tunaacknowledge changamoto mnayopitia hasa kwenye suala la ajira na maslahi ukizingatia ongezeko kubwa la wahitimu wenye shahada ya udaktari ukilinganisha na fursa za ajira zilizopo.

Kitu kinachoendelea sasa hivi ni harakati za makusudi za kada husika kujikwamua kutoka katika lindi la unemployment. Tunaelewa wenzenu wafamasia wanapata fursa adhimu ya kusimamia utolewaji wa huduma za kifamasia kwenye mafamasi hivyo huwasaidia hata kama hawana ajira rasmi.

Hivyo basi, vita yenu imejikita katika kuwapoka/kuwanyang'anya fursa wenzenu badala ya kufikiria namna ya kucreate ya kwenu kulingana na taaluma yenu. Nitatoa mifano michache;-
  1. Kwanini tusiangalie fursa zilizopo kwenye hizi outlest za kutolea huduma za afya kama zahanati na polyclinics tukawainfluence watunga sheria na tukaweka sheria itakayohakikisha sisi ndio tunasimamia hizi facilities?
  2. Kwanini tusijikite kwenye kuhakikisha hizi shule za kutolea elimu ya utabibu kwa lower cadres zinahitaji some kind of monitoring or supervision na hii iwe by us?
In view of the above, nadhani ndugu zangu madaktari, ifike wakati muhamishe target ya kusolve hili suala lenu kutoka kuwanyang'anya wafamasia fursa yao kwenda kwenye kutengeneza fursa yenu wenyewe.

Nawasilisha kwa mjadala.
 
Safi sana umesaidia kujibu hoja kisomi zaid
 
Kuna daktari alimuandikia mtoto captopril 0.13mg tds 1/12..lakini alikuwa hajui dose hii itapatikanaje ikiwa kidonge kina 25mg..jasho lilimtoka...akaja pharmacy kuuliza akajibiwa tuachie hiyo ni kazi yetu.
Hahahhaaa, I wish ningemuona na kale kajasho kake kimbamba
Wanaume wakaingia kufanya compounding..wakapiga kitu cha dilution (c1v1=c2v2) wakapata hiyo dose ya 0.13mg kwa kutengeneza syrup.
Wanataka kudandia majukumu, hili dogo tu hawaliwezi
Sasa huyu jamaa anayesema daktari anaweza kufanya kazi ya Pharmacist sijui anadhani ni pale kusoma prescription na kutoa dawa au..kitu ambacho hata mfamasia hafanyi amewaachia technicians na assistants.

Hicho ndicho wanachofikiria tena wanaleta hoja eti ADDO amepata mafunzo kidogo halafu anaruhusiwa kutoa dawa ila wao pamoja na kutibu wanakatazwa kutoa dawa.

Utoaji unaopigiwa chapuo hapa ni kudispense hasa kwenye Community Pharmacy.

Madaktari wanachoumia sana wala sio ishu ya ADDO, hiki ni kivuli tu cha wao kuongea. Kinachowaumiza ni mamlaka aliyonayo Mfamasia katika biashara ya Dawa(Business of Pharmacist) ambapo wao hawana, huu ni wivu tu.
 

Ipo hivi ndugu yangu...Miongozo hadi sasa kwenye upande wa Community Pharmacy na DLDM..........Community Pharmacy inahitaji Pharmaceutical Personels tuu. Lakini DLDM ndo serikali ilitoa fursa kwa other medical personels kukabiliana na upungugu mfano; Daktari,Tabibu,Muuguzi kama anataka kuhusika kwenye DLDM basi lazima asome short course ya ADDO.Na sio kwamba mtu yeyote asie na background ya afya anasoma ADDO.!!... kama mtu baki anataka kumiliki basi atapewa mafunzo ya Umiliki wa ADDO...na kuajiri mtaalam wa afya mwenye addo au mwenye kozi za Pharmacy level ya Diploma hadi Certificate.

Swali lako sasa..:::Kwani Daktari anashindwa??...kwanza inabidi ujue hakuna kazi ngumu Duniani ni suala la kuelekezwa ,kuzoea na kufanya...na ndio maana mtu yeyote akifundishwa kuchoma Sindano anachoma vizuri tuu..Mind you kuna Madaktari walitumbuliwa walikuwa wamegushi vyeti....lakini kwan kazi walikuwa hawafanyi??? Ukizoea(Experience) kazi yeyote unafanya
Suala linakuja kwenye UFANISI....(jicho la kitaalam)...unavyohudumu ni je kwa asilimia kubwa ni sahihi?? Hakuna changamoto zozote zinaweza kujitokeza??Jambo gani lifanyike na lisifanyike kipindi Mgonjwa anaanza kutumia dawa??..hapa ndio Utaona gap la kitaaluma lililopo...reasoning why iwe hivi na sio hivi......!! Tatizo pia ni kwamba Layman au mtu asie na ujuzi ataona rahisi tuu kuandika 2 ×3 kakariri....kumbe inaweza ikawa hata 3 × 2...!! Hii kureason ndo suala linabaki kwa wafamasia..kuna watu wa organ failure,huwez hudumia mtu perfect na mwenye tatizo katika Namna sawa sababu na ufanisi wa mwili sio sawa.....!! Why dawa hii usinywe maziwa dawa hii unywe..why dawa hii usipige pombe dawa hii baada ya muda fualn unywe....why dawa hii na hii Hapana..""Na huo ndio Ufanisi wa kazi sasa"" ndo unaleta Specialization...na kusema kila mtu afanye alichosoma kwa usahihi...Nurse hawez kuwa daktari,Mfamasia hawezi kuwa daktari, mtaalam wa maabara hawez kuwa daktari and Vice Versa....sababu hasa ""Reasoning yao tofauti""
 
Wafamasia hawana shida, wanafanya majukumu yao bila kuingilia ya wengine. Tatizo ni hawa madaktari kujifanya wanajua kila kitu cha kada nyingine na kutaka kuingilia majukumu yasiyo yao.

Utakuta Daktari anamuandikia mgonjwa dawa kwa kiasi fulani cha dose lakini hajui namna hiyo dose inaweza kutengenezwa endapo dawa iliyopo ina dose kubwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…