Waziri Ummy, Usipotoshwe maamuzi yako kuhusu ADDO na wafamasia mtawaumiza Watanzania

Nime mwelewa vizuri sana Waziri lichukue hili. Lifanyie kazi.
 
Daktari ana prescribe dawa
 
Kwakweli mpaka ulipofikia huu mjadala sijauelewa vizuri kutokana na kukosa background ya mfumo wetu wa utoaji dawa hospitalini, kwenye pharmacies na nini hasa kinachogombewa humu.

Hoja nyingi zinazobishaniwa humu kijijini kwetu mfumo wake ni tofauti inaonekana.

Ni hivi kwa mfumo wa kijijini kwetu dawa anaandika Dokta kupitia ushahidi wa vipimo kila kitu huku ni evidence based; so hakuna mtu mwingine mwenye uwezo wa kuandika dawa nje ya hospitali ata kama ni dokta.

Dawa zozote ambazo zinahitaji mixing kama antibiotics fluids and other drips hiyo kazi inafanywa na nurse, kitu kingine nurse kwa kuwa yupo na mgonjwa muda mrefu kupitia uzoefu wake anauwezo wa kuchua clinical decision bila ya Dr hali ya mgonjwa inapobadilika na kunahitajika intervention za dharura.

Nurse pia anafahamu pathophysiology za magonjwa ya ward anayofanya kazi akiona dawa aliyopendekeza Dr ailingani na hali ya mgonjwa anaweza shauri tofauti there is always a senior nurse to consult kila ward ndio in charge ambae ataamua.

Kama kuna dawa za kupewa kutumia nyumbani ndio mgonjwa unaenda kuchukua pharamacy kwa prescription ya Dokta.

Otherwise kazi za pharmacy zinasimamiwa na pharmacists not anyone else; na kwenye medicine kwa taratibu zake kama kuna mtu ameajiriwa kuuza dawa au kutoa huduma yoyote ata ya kumwangalia mgonjwa (care assistant) kama ajasomea maswala afya lazima apewe basic training ya kazi kulingana na majukumu yake vinginevyo aruhusiwi you are not allowed to delegate duties to anyone who is not trained to perform them in a health system nadhani ndio msingi wa ADDO huko pharmarcy.

Sasa kwenye huu mjadala I am lost sijui hata wanabishania nini tena if anything nilichojifunza mfumo wa wetu wa everyday operation za hospitali unatatizo unahitaji wataalamu kuangalia upya; kila mtu mjuaji.

Sidhani ata kama hospitali zetu zina utaratibu wa ku record medical errors na sababu zake kama ni uzembe (negligence) mtu anachukuliwa hatua za kisheria au hata kama wana record any other critical incidents na kuzichunguza ili baadae watu wachukiwe hatua if it’s deemed negligence. Sio kila mara hayo makosa yanapotokea lazima mtu aadhibiwe mengine ni innocent mistakes.

Sasa huu mjadala umejaa majigambo ambayo hayana tija kwa watumiaji wa huduma ya afya ni professional rivalry inayohatarisha quality ya utoaji wa huduma na usalama wa wateja na inaonyesha there is so much medical error iwapo hakuna ushirikiano na kila mtu mjuaji.
 
Halafu mbona maduka ya dawa za mifugo na mimea hawaihaji cheti cha ADDO!? Au dawa zao hazisomewi na wafamasia!?
 
Daktari ana prescribe dawa
Kwa hiyo akifanya hivyo haitoshi?
Kinachofuata baada ya hapo kuna watu wengine wanachukua wajibu wao juu ya mgonjwa aliye'prescribiwa' dawa. Kwa nini hili liwe gumu kueleweka?
 
1. Sehemu ya kupewa dawa inaitwa PHARMACY. Pharmacist ndiyo amequalify kufanya kazi hapo. Clue ipo kwenye jina

2. Mambo mengi anayosoma Daktari mfamasia pia anasoma.
Physiology(jinsi mwili unafanya kazi)

Microbiology(bakteri na virusi)

Parasitology(Minyoo na parasites
wengine),

Biochemistry(chemistry ya viumbe hai)

Epidemiology(Kusambaa kwa magonjwa)
Biostastatistic(Takwimu za afya)

Anatomy(muundo wa mwili) na Pathology(magonjwa yanavyokuwa) anasoma haya kwa kiasi.

Mambo haya yanamuwezesha kufahamu magonjwa na mwili wa binadamu unavyofanya kazi.

Pharmacology(jinsi dawa inavyofanya kazi mwilini). Hili anosoma kuliko daktari

3. Anasoma pia. Chemistry ya madawa, madawa ya mitishamba, jinsi ya kutengeneza dawa, jinsi ya kutunza dawa, jinsi ya kutoa dawa, na clinical pharmacology(jinsi dawa zinavyotumika hospitalini, magonjwa yanavyokuwa na matibabu yake).

So kabla ya kubishana tunapaswa kwanza kufahamu huyu mfamasia ana maarifa ya namna gani. Sijaona madaktari wengi kwenye huu uzi, wanajua jinsi ambavyo huyo Prof yupo wrong.
 
Madaktari wa bongo faka sana na wanatakiwa wawe regulated to the maximum, sitasahau kuna Dr mmoja tena Prof alinipa diagnosis fake ya kipumbavu na nusu inimalize kwa ajiri ya madawa niliyopewa kutibu ugonjwa ambao ulikuwa fake, sitasahau hilo
 
Sijui wanazungumzia mfamasia wa level gani mbona kwenye maduka ya madawa wanaogawa dawa na kuelekeza namna ya kuzitumia utakuta ni watu wa kawaida kabisa tena wengine walifaulu kwa kiwango cha chini Elimu ya kidato cha nne?

Kama daktari ndo anapendekeza dawa gani mgonjwa atumie Ili kutibu tatizo na mfamacia kazi yake ni kutoa dawa zilizopendekezwa na daktari sasa hapo Nani ni Nani?

Wafamasia mnataka kujifanya mko juu kuliko daktari huo ni uongo! Daktari anaweza kufanya kazi bila mfamasia ila mfamasia hawezi kufanya kazi kama daktari hayupo
 
Sijui wanazungumzia mfamasia wa level gani mbona kwenye maduka ya madawa wanaogawa dawa na kuelekeza namna ya kuzitumia utakuta ni watu wa kawaida kabisa tena wengine walifaulu kwa kiwango cha chini Elimu ya kidato cha nne?...
Wewe na we akili yako imedumaa..hoja hapa kila mtu asimamie taaluma yake..madaktari wa bongo wengi ni njaa tupu..wamekalia kupoka kila fursa ndani ya kada ya afya..hasa zile zenye harakati ya pesa.

#MaendeleoHayanaChama
 
Wewe na we akili yako imedumaa..hoja hapa kila mtu asimamie taaluma yake..madaktari wa bongo wengi ni njaa tupu..wamekalia kupoka kila fursa ndani ya kada ya afya..hasa zile zenye harakati ya pesa.

#MaendeleoHayanaChama
Kama mtu ameaomea pre nursing au nursing tena ya mwaka mmoja halafu anaweza kugawa dawa na kumuelekeza mtumiaji je kwa MD itakuwa ajabu? Kwani hata Hawa wafamasia wa kibongo wana Nini kama si kugawa dawa tu? Wamegundua au kutengeneza dawa gani? Kujifanya wakubwa wakati hata panado hawawezi kutengeneza !!! Wafamasia wa kibongo ni wagawa dawa tu hakuna jingine wanalijua
 
Wewe unaweka uongo kwa sababu hujui kama ulivyojieleza hapa mwenyewe.

"Wafamasia mnataka kujifanya mko juu kuliko daktari...," Huu ni uongo. Umeona wapi famasia akitaka kuwa juu kuliko daktari? Daktari anayo kazi yake inayofahamika kisheria kabisa, na Famasia anayo kazi yake inayofahamika kisheria kabisa. Wote wamehitimu katika maeneo yao yanayowahusu. Mfamasia hawezi kwenda kudai kazi anazofanya daktari, sasa wewe kwa kutojua kwako, daktari anapotafuta kufanya kazi zinazomhusu Famasia, kwa vile hujui uwezo wa hawa wawili katika nyanja zao, hapo unachanganyikiwa na kuanza kuropoka kama ulivyofanya hapa.

Hao unaowaona wakigawa dawa kwenye maduka ya dawa, wote wanafanya kazi chini ya uangalizi wa Famasia. Ni lazima wawe chini ya uangalizi huo, ndivyo sheria inavyosema, na ndivyo taaluma ya Famasia inavyoelekeza.

Sasa basi, kama unataka daktari naye akagawe dawa, kama unadhani anaweza kufanya hivyo kama hao unaowaona watu wa kawaida kabisa ndani ya Pharmacy, basi tukubaliane, daktari wako afanye kazi hiyo chini ya usimamizi wa Famasia, maana ndivyo sheria inavyoelekeza duniani kote inapohusiana na madawa. Daktari kazi yake haihusu shughuli za madawa. Shughuli za madawa ni za Famasia. Hiyo ni taaluma nyingine, tofauti kabisa na taaluma ya udaktari, pamoja na kwamba wote wanahudumia mgonjwa, kila mmoja kwa ujuzi wake, mambo aliyoyasomea.

Sasa sijui kama utanielewa, lakini naomba usome kwa akili inayotaka kujifunza na kujua. Usisome kwa akili ambayo tayari umeielekeza katika ujuaji, kama ulivyofanya hapo juu.
 
"80% ya wapharmacia huko S.Africa alipo Professor kazi yao kubwa ni kugundua na kutengeneza dawa viwandani na hao 20% hufanya kazi hospitali (kuwasaidia ma nesi na ma MD kutunza na kusambaza dawa)" kwa madai ya Prof Koboko

"Mpharmacia hasomi kuhusu magonjwa na wadudu" kwa madai ya Professor

Hivi huko viwandani wanatengeneza vipi dawa kwaajili ya kutibu magonjwa ikiwa hawajasoma hayo magonjwa ?
;Utajuaje MECHANISM ya dawa bila kujua kisababishi/wadudu unakidhibiti vipi (?

:
 
Umefanya vizuri kutoa ufafanuzi kuhusu maduka haya ya "Dawa Muhimu."

Na kwa bahati mbaya sana, Koboko yeye katumia fursa ya udhaifu wa maduka haya kulaumu/kushutumu fani ya Famasia, jambo ambalo sasa naona halina uhusiano kabisa na maduka haya.

Lakini katika maelezo yako, inaonekana dhahiri kwamba pamekuwepo na udhaifu katika usimamizi na uendeshaji wa maduka haya. Kama yanageuzwa kufanya kazi nyingine ambazo hazikupangiwa kufanyika humo, inakuwaje chombo kinachosimamia haya maduka kisiwe na uwezo wa kuyafuta/ kuyasimamisha kufanya kazi kwa makosa yaliyofanyika? Pharmacy ikifanya ujinga huu, itaachwa iendelee kufanya kazi?

Kwa hiyo basi, inaonekana matatizo yanaanzia kwa chombo kilichopewa dhamana ya kusimamia shughuli za maduka haya; kuhakikisha kwamba hayakiuki taratibu yaliyopewa na shughuli yaliyopangiwa kuzitekeleza.

Baraza la Famasia wamejikokea wenyewe moto utakaowaunguza.
 
"80% ya wapharmacia huko S.Africa alipo Professor kazi yao kubwa ni kugundua na kutengeneza dawa viwandani na hao 20% hufanya kazi hospitali (kuwasaidia ma nesi na ma MD kutunza na kusambaza dawa)" kwa madai ya Prof Koboko...
Anyanganywe huu uprofesa wake wa mchongo...andiko hili limemuacha uchi sana.
 
Kwako Mh. Waziri wa Afya wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Ndugu Ummy Mwalimu.

Kwanza pole kwa kazi nzito unayoifanya yakusimamia wizara nyeti na ngumu yenye wataalam wengi wenye weledi, kadhia, hamu na kamu katika kuleta maendeleo chanya hususan katika sector ya Afya.

Mh. Waziri mimi ninayeandika makala hii ni mtaaluma wa fani zote mbili ambazo huleta mvutano usio na tija katika taifa letu, nina Diploma in Pharmaceutical science na Bachelor of medicine and surgery zote kutoka Oslo School of medicine nchini Norway.

Nasikitika kusema kwamba hali ya utendaji kazi katika sector ya afya inaharibiwa na watu wenye academical fallacy and abuse, watu hawa hujiona kuwa vyeti wanavyomiliki vinawapa dhima yakubeba dunia nzima katika mifuko yao wanayoweka shilingi, hali hii huleta utengano na hali ya kudharauliana katika taaluma walizopo, hii haipo tu katika kada ya afya bali katika fani zote zinazohisika na utendaji kazi kwa kutumia taaluma.

Nimesikitishwa na mtu anayejiita professor huku akijitwika vyeo kama mmed and PhD, akisahau kuwa anaaibisha wataaluma nguli katika sekta ya afya wenye wadhifa kama huu mathalani Prof. Sarungi ambaye amefanya mambo mengi mazuri katika wizara ya Afya.

Nilipojaribu kuingia katika mtandao wetu wa medical council of Tanganyika kumtafuta mwanataaluma huyu sikuweza kupata taharifa zake katika database ya baraza letu, ndipo nilipojua kuwa huyu ni kijana wa hovyo ambaye atakuja kuingia kwenye kundi la wataaluma wenye academical fallacy and ignorance kwa spidi ya 4g, kwa uelewa wake mdogo wakuchanganua mambo nimeona kabisa huyu ni mwanafunzi tena wa mwaka wa kwanza semester ya Kwanza Aliyegusa gusa human anatomy and physiology na kuanza kuona ameshamaliza taaluma nzima ya afya, ambaye hajui hata umuhimu wa team work katika kumuhudumia mgonjwa hospitalini.

Akishindwa hata kujua kuna kitu kinaitwa University prospectus ambacho kingemsaidi kujua anachokisoma mtaaluma mwingine kina mwingiliano gani na yeye, anashindwa hata kutambua kuwa hata wafanyakazi wa hospital wasio na utaalam wa tiba hupewa mafunzo juu ya magonjwa, dalili zake na namna ya kujikinga awapo katika mazingira yake ya kazi, leo hii anatoka kijana mmoja wa hovyo nakuandika kuwa mwanataaluma aliyefunzwa kwa miaka 5 hajui magonjwa na dalili zake? Hii ni hatari sana na academical fallacy ni ugonjwa unaotafuna wengi.

Katika pitapita zangu nikakutana na andiko la ndugu Yoshua nguyahambi aliyejishusha kuwa darasa la saba B ilihali kwa aliyoeleza inahakisi yeye ni mtaaluma anayejua anachokifanya napenda kuchangisha andiko lake na uzi wangu ili kuweza kusediment ujumbe wangu kama ifuatayo;

Yoshua Nguyahambi, Darasa la Saba B

Ndugu zangu nawasalimu kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Nimeisoma kwa makini Makala ndefu ya mtu anayejiita Prof. Patrick Koboko, nashawishika kukiri wazi kwamba Profesa (Kama anavyojiita) amefanya upotoshaji wa makusudi kwa mhe. Waziri wa Afya na Umma wa watanzania kuhusu Addo na taaluma ya ufamasia.

Kwanza, katika makala yake amedai kazi ya mfamasia ni Kutunza na kuifadhi dawa, kusambaza maeneo yenye uhitaji pamoja na kutengeneza dawa viwandani na siyo kutoa dawa moja kwa moja kwa mgonjwa, ameenda mbele zaidi na kusema kazi ya mfamasia siyo drug administration eti hii ni kazi ya watu wengine, ameendelea kudai kwamba mfamasia hajasomea magonjwa wala wadudu wanaosababisha maradhi na hajasomea dalili za magonjwa, huu ni upotoshaji wa kijinga na makusudi kabisa uliofanywa na mtu wa ngazi ya uprofesa, angekuwa kwenye nchi za wenzetu angeshaitwa na kunyang'anywa uprofesa mara moja!

Hivi katika akili ya kawaida tu ya la saba B, kama yangu, mtu anaweza kukutengezea dawa kiwandani kama alivyodai anayejiita profesa, bila kujua issue za drug administration, epidemology, Anatomy, Physiology, Parasitology, Pathology, Medical semiology, medical toxicology, microbiology, biochemistry, Parasitology? Yaani mtu akutengenezee Paracetamol na asijue namna ya kuitoa kwa mgonjwa? Anasahau kabisa wao (wafamasia) watengenezaji wa dawa ndio wanawaandalia leflet zinazoonyesha namna dawa inavyopaswa kutumika, athari zake, n.k. Profesa wakati unaandaa makala hii ulikuwa wapi? Au ulikuwa na hangover ya K-vant?. Wakati mwingine tunapoamua kuandika makala sensitive na zinazogusa moja kwa moja Umma wa watanzania tusisukumwe na jicho la wivu, husda na kijino pembe kwa taaluma za wengine.

Profesa Patrick Koboko MD, MMED,PhD(kama anavyojiita) amenifanya mimi darasa la saba B nirudi kuangalia tena Prospectus ya vyuo vinavyotoa course za ufamasia, kuangalia je madai yake aliyoyatoa kuhusu wa wafamasia yana ukweli? Ni halali? Mathalan ukisoma prospectus ya chuo kikuu cha Muhimbili ya 2019/2020 – 2020/2021 ukurasa wa 75, kuna maneno yasomeka hivi, nanukuu "Pharmacy education embraces the search, development, formulation, analysis, storage and distribution of products for maintenance and restoration of good health as well as provision of information and guidance on proper use of medicines."

Sio kazi yangu darasa la saba B kumtafsiria maneno hayo, lakini ni wazi kuwa wafamasia ndio wanataaluma pekee wanaondaliwa sio tu kwajili ya yale aliyosema, wafamasia wanapaswa kuyafanya lakini pia kwajili ya kulea na kutoa taarifa sahihi za matumizi sahihi ya dawa, Prof. Koboko (kama anavyojiita) alipaswa alijue hili mapema hata kabla hajafikiria kuandika makala yake.

Kwahiyo kama darasa la saba B nampa home work profesa Koboko (kama anavyojiita) aende aipitie tena Prospectus ya Muhimbili na vyuo vingine vinavyo offer digrii ya ufamasia, aangalie vizuri kwa kulinganisha na hizo taaluma nyingine ni wapi kwenye Prospectus hizo mfamasia haandaliwi kutoa dawa kwa mgonjwa?

Litakuwa kosa kubwa la karne kama usimamizi wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi vitaondolewa kwenye mikono ya wafamasia kwa maana ya Baraza la famasi, kwasababu ya ushauri wa ki husda na kijino pembe ulitolewa na huyo anayeitwa Profesa, kwa sababu kwa mfumo wa elimu ya Tanzania ni wafamasia pekee ndio wameandaliwa kwa jukumu hilo. Profesa kama anavyojiita alipaswa kulifahamu hili.

KUHUSU ADDO.

Arudi aangalie vizuri kwanini wizara ya afya iliamua kuanzisha mafunzo hayo, ingawa ni kweli kuna mapungufu lkn haiondoi nia njema ya Serikali kupitia wizara ya Afya iliyoamua kuanzisha mafunzo hayo, ambapo awali yalikuwa chini ya TFDA sasa hivi TMDA, na baadae uratibu wake ukahamishiwa baraza la famasi kwasababu wao ndio wadau & walezi sahihi wa mambo yote yanahusiana na dawa, vifaa tiba na vitendanishi

Upo ushahidi wa wazi kabisa wa baadhi ya maduka haya ya dawa muhimu ambayo wanataaluma wenzetu (wasio wafamasia) wameyageuza kuwa Zahanati bubu kinyume kabisa kanuni zinazoruhusu uanzishaji wa maduka ya dawa muhimu unavyotaka, na ndicho anachojaribu kushauri Profesa (kama anavyojiita) kuwa maduka haya yageuzwe kuwa zahanati bubu kwa kupewa matabibu na Manesi bila kufundishwa chochote kuhusu malengo ya uanzishwaji ya maduka haya, kama nilivyosema awali litakuwa kosa kubwa la karne kuupokea ushauri huo bila kuzingatia ukweli niliouanisha kwenye makala yangu" mwisho wa andiko la Yoshua.

Ni rahi yangu kwa madaktari wote nchini kutambua, kuheshimu na kuthamini uwepo wa kila mmoja wetu katika sekta ya Afya, sisi hatuna authority yeyote yakushusha, kutweza na kubagaza taaluma zingine, nichelee kusema kwamba kwa sasa kipindi ambacho niko masomoni (Resident 2) wafamasia wamekuwa msaada mkubwa kwangu especially katika kufahamu dawa za aina mbalimbali hata zile ambazo haziko katika scope ya masomo yangu, ndugu hawa wako honest sana na wengi hupenda kurejea katika maandiko "books or publication" incase akihisi kitu hana uhakika nacho hali ambayo ni tofauti kwetu sisi madaktari ambapo uhusi kufanya hivyo ni kujishusha thamani na kuonekana HUJUI, nimepractice nchini Sweden na nakiri kusema hali ni tofauti Sana ukilinganisha na nchini kwangu, sikuwahi kusikia mvutano wakitaaluma katika nchi yoyote huku ulaya wala marekani na wao ndio chachu ya mifumo hii ya afya, sembuse sisi tuliopokea kama mapokeo..ni Aibu lakini ndio uhalisia.

Mwisho kabisa nachukua fursa hii kuwataka radhi wafamasia wote waliokerwa na andiko lile, niwatie moyo kufanya kazi kwa weledi kutokana na maadili ya kazi yenu, mchango wenu ni wamuhimu katika sekta ya afya, mnatusahihisha na mengi sana especially drug interactions and drug overdose kwa hili siwezi ficha mnatusaidia sana.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki taaluma ya Afya nchi Tanzania.

Doctor junior
Resident in internal medicine.
 
Dawa zao hazisomewi na wafamasia.
Mfamasia ana idea pia kuhusu dawa za mifugo , maana dawa nyingi zinafanana tofauti ni pharmacokinetics parameters ndio zinakuwa tofauti kidogo , sijajua kwenye mitaala ya kitanzania kwa wenzetu huwa wanasoma pia veterinary pharmacology semester 1 au 2.
 
Pharmacist (mfamasia) ni Degree holder

Pharmaceutical Technician (Fundi dawa sanifu) Huyu Ni Diploma

Pharmaceutical Assistant (Fundi dawa sanifu msaidizi) Huyu ni Certificate

Dispenser (Huyu Ni mtoa dawa ila yupo chini ya Fundi dawa sanifu msaidizi)

Hao unaowaona wanakupa dawa kwenye pharmacy si phao labda ubahatike kukutana nae, pharmacist Kazi yake ni kusimamia shughuli zote za uendeshaji pharmacy na kuangalia competent ya hao wanaotoa huduma kwenye pharmacy Kwa wagonjwa....

Pharmacist ndio msimamizi mkuu wa pharmacy yeyote ndo maana Cheti chake hutumika kusajili pharmacy

Note: Wabongo tumezoea kila anaetoa dawa tunamuita mfamasia, au ukienda hospitalini kila alievaa Koti Muna Muita Dokta ila sivyo hivyo....

Nawasilisha hoja
 
Da
WAZIRI UMMY MWALIMU, USIPOTOSHWE NA WAFAMASIA KUHUSU ADDO, MTAANGAMIZA AFYA ZA WATANZANIA.

Na Prof Patrick Koboko(MD,MMED,PhD)

Salaam Mhe Waziri!
Daktari upo wapi?
Kunywa chochote nitalipa.
Naunga mkono hoja.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…