Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu: Wagonjwa 37 wamethibitishwa kupona virusi vya Corona na wameruhusiwa kwenda nyumbani

Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu: Wagonjwa 37 wamethibitishwa kupona virusi vya Corona na wameruhusiwa kwenda nyumbani

Kwanini wengi mnatamani idadi kubwa itangazwe ya wenye maambukizi na waliokufa kama siyo roho ya uchawi inawasumbua

♡♤Life belongs to all who struggle for it♤♡♧
Magufuli alisema wamepona 100 mbona waziri kasema wamepona 37 na sio 100!! Tumuamini nani kati yao?
 
Kwahiyo ni 137 waliopona?
Jamani Rais alisema walishapona zaidi ya Miamoja ndio maana akaomba watangazwe wanaopona kuanzia sasa, Aliomba watangazwe hao waliopita ndio basi haiwezekani kuwachanganya,nyie ndio walewale mtakaoanza kuuliza maswali yakijinga kuwa hao watu wameponaje kwa muda mfupi 137?na ndio maana hawajachanganywa kuondoa hayo maswali
 
Tofauti na nchi nyingine, sisi tutakuwa tunatangaziwa idadi ya waliopona tu.
Idadi ya cases mpya na tumepima wangapi hiyo tuachie nchi nyingine, sio kila kitu tuige.
Kwa strategy hii mpya, tatizo limekwisha.
 
Waziri wa Afya Ummy Mwalimu amesema wagonjwa 37 wa corona wamepona na kuruhusiwa na sasa waliopona wamefikia 48, wagonjwa hao ni kati ya 108 waliothibitika kuwa na corona ila kwa sasa hawana dalili, wengine 71 wanasubiri vipimo vya mwisho na wataruhusiwa.
Nilijua tu maagizo ya jiwe yataaanza kutekelezwa haraka hatutaasikia number kubwa ya waagonjwa tena.Jaman tumekwisha kwa hili jiwe
 
Back
Top Bottom