#COVID19 Waziri wa Afya: Watu 408 wamebainika kuwa na Corona , 284 wakiwa katika mashine za oksijeni

#COVID19 Waziri wa Afya: Watu 408 wamebainika kuwa na Corona , 284 wakiwa katika mashine za oksijeni

Corona ipo. Will mbili hizi nimeshuhudia misiba misiba miwili ya watu waliokufa kwa matatizo ya mapafu..tuchukua tahadhari
 
Mkwele lazima asepe na hii korona 3 maana alifurahia sana kifo cha jembe
Namuomba mungu na shetani hii covidi iondoke na wasaliti wa hii nchi
 
1625980499690.png
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Dorothy Gwajima amesema hadi kufikia Julai 8, 2021 jumla watu 408 walibainika kuwa na ugonjwa wa corona huku 284 wakitumia mitungi ya oksijeni.

Dk Gwajima ametoa taarifa hiyo leo Jumamosi Julai 10, 2021 wakati akitoa elimu ya kujikinga na ugonjwa huo kwenye mnada wa Msalato jijini Dodoma.

Kwa upande wa Mkoa wa Dodoma, Waziri huyo amesema hadi kufikia Julai 8, 2012, jumla ya watu 26 waligundulika kuwa na ugonjwa huo huku 22 wakiwa katika mitungi ya oksijeni.

Wakati huo huo, Dk Gwajima na kamati ya ulinzi na usalama ikiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Anthony Mtaka wametembea umbali wa kilometa nne lengo likiwa ni kuhamasisha jamii kuvaa barakoa ili kujikinga na maambukizi.
 
Upuuzi mtupu,,,hivi tukifunguwa kusafiri nje ya inchi,,,
serikali itapata faida gani?

Sijawahi kuona serikali isiyopenda raia wake kama serikali hii ya Tanzania..

Inchi nyingi za uarabuni zimekuwa zikikimbilia mabaharia wa kitanzania.
Baada ya wahindi na waphilipino kuzuiwa kuingia uarabuni.
Kwa kesi za maambukizi kuwa nyingi.
Na Tanzania kuonekana hakuna corona.

Sasa hayo maigizo yenu ya kutaka pesa kwa mabeberu mnataka tufungiwe mabaharia wa Tanzania tuonekane tunaumwa..

Hovyo kabisa,,
Mnasema watu wanaumwa corona mbona hamsitishi msongamano wa watu?

Mbona bado mmefunguwa vitu vinavyoleta msongamano na maambukizi?

Ni lini mmepima watu na kujuwa wanaumwa ni kadhaa?

Wacheni maigizo yasio na tija.
 
Wagonjwa 408 ni wachache sana ni sawa na asilimia 0.000742 ya watanzania wote. Wakifika asilimia moja mnijulishe nianze Kuvaa barakoa.

Chukua tahadhari mapema usisubiri Hadi yakufike karibu yako...

Elimisha wa karibu yako kwamba ugonjwa upo usifanye mzaha na c19 wimbi la Sasa ni hatari zaidi...
 
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Dorothy Gwajima amesema hadi kufikia Julai 8, 2021 jumla watu 408 walibainika kuwa na ugonjwa wa corona huku 284 wakitumia mitungi ya oksijeni.

Dk Gwajima ametoa taarifa hiyo leo Jumamosi Julai 10, 2021 wakati akitoa elimu ya kujikinga na ugonjwa huo kwenye mnada wa Msalato jijini Dodoma.

Kwa upande wa Mkoa wa Dodoma, Waziri huyo amesema hadi kufikia Julai 8, 2012, jumla ya watu 26 waligundulika kuwa na ugonjwa huo huku 22 wakiwa katika mitungi ya oksijeni.

Wakati huo huo, Dk Gwajima na kamati ya ulinzi na usalama ikiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Anthony Mtaka wametembea umbali wa kilometa nne lengo likiwa ni kuhamasisha jamii kuvaa barakoa ili kujikinga na maambukizi.
=====

Ni wakati sasa wa Wananchi na asasi na taasisi mbalimbali za kiserikali na zisizo za kiserikali kushirikiana na serikali katika kutekeleza na kuhamasisha maelekezo ya wataalamu wa afya juu ya hatua za kukabiliana na ugonjwa huu.

View attachment 1848604 View attachment 1848605
Hizi data ZA kupikwa ila mwanzo mzuri
 
Huyu mama ni muongo kuliko Prof. Muhongo. Hapa nilipo Kuna watu 9 wamefariki Leo Kwa COVID-19. Hospital zimejaa wagonjwa. Mbona hakutaja waliokufa? Hiyo idadi ni kutoka mkoa au wilaya gani Tanzania?
Duh! kwani mkuu unafikiri hata hao wanatajwa kufa kwa covid ni kwamba kweli wote vyanzo vya vifo vyao ni covid? wewe unaweza kufa na mipresha yako huko ila ukipimwa na kukutwa na virusi vya corona teyari kifo chako kinahesabika ni cha covid.
 
Ndio nini sasa hiki ? hao 408 wamegundulika lini ? Na Wapi ? Katika kutambua ukubwa wa tatizo tunatakiwa tuambiwe eneo na kipindi cha muda walipogundulika vinginevyo tunaona ni janja janja tu !
Hii ndio TZ
 
Huyu mama ni PhD Kwa kusomea au ni Dr wa binadamu? Data alizo zitoa Leo ni maajabu ya data
Hivi kwanini lawama hapewi Rais mama samia katika hili kama ambavyo alivyokuwa anapewa lawama Magufuli? Rais mwenyewe kanyamaza kimya kwa maana haoni kinachofanywa na waziri wake ila sisi ndio tunamlaumu waziri na kumuacha Mama samia.
 
Back
Top Bottom