Waziri wa fedha ingilia kati sakata la uboreshaji wa mashine za EFD, kamishna wa TRA ataleta balaa kubwa

Waziri wa fedha ingilia kati sakata la uboreshaji wa mashine za EFD, kamishna wa TRA ataleta balaa kubwa

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Muda uliotolewa wa kuboresha Mashine za EFD wa mwezi mmoja (kuanzia desemba 7 hadi Januari 7) hautoshi, kwa sababu mawakala wanaofanya kazi hiyo wamezidiwa na kazi hiyo kutokana na wingi wa mashine hizo na tayari wameomba kuongezewa muda wa kufanya marekebisho hayo ya ghafla yaliyosababishwa na TRA wenyewe kutokana na sababu zisizofahamika.

Tayari Kamishna wa TRA amekataa kuongeza muda na ameahidi kuwaadhibu wafanyabiashara walioshindwa kuboresha machine zao za EFD kwa muda uliopangwa , hapa analenga kuwakamua pesa wafanyabiashara ambao tayari wana hali mbaya kutokana na kuzorota kwa biashara nchini.

Sasa kwa hali hii kamishna haondoi Tatizo bali anaharibu zaidi, ikumbukwe kwamba wafanyabiashara wenye EFD hawajakataa kuboresha mashine zao bali mawakala wenye dhamana hiyo wameshindwa kumaliza kazi kwa wakati, wako ambao mashine zao ziko kwa mawakala mpaka sasa zikisubiri foleni ya kuboreshwa, sasa kamishna anapokataa kuongeza muda halisaidii Taifa bali ataleta mkanganyiko zaidi.

Namuomba Waziri wa fedha aingilie kati jambo hili ili kuokoa biashara za watu kwa Manufaa ya Taifa.
 
Busara Inatakiwa Kutumika Vinginevyo Suala La Mkomoeni Halitaleta Afya Kwa Ustawi Wa Tanzania. Iwapo Ni kweli Mawakala Wamelewa. Unatoa Vp Adhabu Kwa Mfanyabiashara!

Hapendwi Mtu, Inapendwa Pesa!

Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania
😀😁😂🤣😃😄😅😄😃🤣😂😁
 
Hili jambo wanaliona labda ni dogo lakini kuna manung'uniko makubwa ndani ya mioyo ya wafanya biashara kwa sababu jambo hili lingepewa muda lifanyike vizuri. Nenda pale ' web technologies ' pale Fire, Kariakoo kuna msongamano mkubwa sana usio wa lazima ambao hata unaweza kuleta madhara mengine na hasa kutokana na hali ilivyo huko duniani kwa sababu hatuwezi kujua nani kaja jana au juzi na huko alikutana na watu gani.

Kwa sababu kodi inalipwa na imekuwa ikilipwa ni swala la kufanya 'upgrading' tu,basi lipewe muda lifanyike kwa ufasaha bila madhara au manung'uniko na kuanza kuisema vibaya serikali kwa sababu tunajua lengo ni zuri kutokana na hili zoezi. Tunaomba hata ikibidi Rais alisikie hili na kulitolea tamko ili muda wa zoezi hili uongezwe.
 
Hili jambo wanaliona labda ni dogo lakini kuna manung'uniko makubwa ndani ya mioyo ya wafanya biashara kwa sababu jambo hili lingepewa muda lifanyike vizuri. Nenda pale ' web technologies ' pale Fire, Kariakoo kuna msongamano mkubwa sana usio wa lazima ambao hata unaweza kuleta madhara mengine na hasa kutokana na hali ilivyo huko duniani kwa sababu hatuwezi kujua nani kaja jana au juzi na huko alikutana na watu gani.

Kwa sababu kodi inalipwa na imekuwa ikilipwa ni swala la kufanya 'upgrading' tu,basi lipewe muda lifanyike kwa ufasaha bila madhara au manung'uniko na kuanza kuisema vibaya serikali kwa sababu tunajua lengo ni zuri kutokana na hili zoezi. Tunaomba hata ikibidi Rais alisikie hili na kulitolea tamko ili muda wa zoezi hili uongezwe.
Inasikitisha sana na inaleta aibu kubwa sana.
 
Busara Inatakiwa Kutumika Vinginevyo Suala La Mkomoeni Halitaleta Afya Kwa Ustawi Wa Tanzania. Iwapo Ni Kweli Mawakala Wamelewa
Unatoa Vp Adhabu Kwa Mfanyabiashara!!!


Hapendwi Mtu, Inapendwa Pesa!!
Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania
😀😁😂🤣😃😄😅😄😃🤣😂😁
Je nchi hii haitaki wafanyabiashara ?
 
Mashine hazipo na bado hazijaingia Dar .Watu wengi wamelipia ila bado mzigo haujafika sasa hapo kosa ni la mfanyabiashara ?
 
Hapo Sasa Hivi Tunasema Kitaalam
Miruzi Mingi Humpoteza Mbwa!!
Wazigua Wao Wangesema Funda Na Mruzi Havikwivana!!

Wanatakiwa Viongozi Wakae Meza Ya Duara
Waone Hali Halisi Siyo Kuamua Tu Vyovyote
Inasikitisha sana
 
Wakitaka kuua nchi waendelee na mpango wao huu
Umasikini wa Watanzania ndio faida kwa CCM. Si rahisi kwa CCM kuwa maarufu kwa Tanzania ya watu wenye uwezo wa kula mara tatu kwa siku na kupeleka watoto wao shule.

Tanzania masikini ndio mtaji mkubwa wa CCM, na ndio maana mpaka leo wakulima hoi kabisa. Sasa bado mmoja - Mfanya biashara ndio aliyebaki na kiburi. Naye ataisoma namba tu. Mi 5 tena.
 
Kitengo cha elimu sijui kina feli wapi sijaona hata demo ya nini TRA wanahitaji efd za awali na hiyo wanayo hitaji, nimepokea sms toka meneja wangu japo haina details kujua nini haswa wanahitaji. TRA fanyeni demo tumeni mitandaoni na katika tv tujue nini haswa kinahitajika.
 
Back
Top Bottom