FaizaFoxy
Platinum Member
- Apr 13, 2011
- 100,246
- 123,145
Mheshimiwa Hussein Bashe, natumai na Rais wetu mama Samia Suluhu Hasan na washauri wake wengine utawafikia ujumbe huu.
Zao la bangi za aina tofauti tofauti (different varieties of hemp) linastawi vizuri sana Tanzania. Ni wakati muafaka, tena tumechelewa sana, kuanzisha zao la bangi kwa faida. Zao la bangi linaweza kututowa kwenye umasikini kwa haraka sana.
Baadhi ya faida zinazotokana na zao la bangi ni pamoja na:
Dawa aina mbali mbali, zinazotumika hivi sasa mahospitalini na dawa mbadala.
Pia bangi inaweza kutengeza karatasi, inaweza kutengeza mbao, inaweza kutengeza, "vigae" vya kuezekea, "boards" mbali mbali za kujengea na kuundia fanicha, inaweza kutengeza bodi za magari ambazo ni bora kuliko za mabati.
Licha ya hayo, inaweza kutengeneza virutubisho mbali mbali vya kutumika na binadam, wanyama na mimea. Pamoja na madawa ya kuzuia wadudu wa mimea.
Pia bangi inaweza kutengeneza mafuta ya kutumika kwenye magari ambayo ni bora kuliko ethanol na methanol.
Kinachotakiwa kufanywa ni kuanza na aina moja au mbili ya bidhaa muhimu na kufunguliwa kituo maalum cha utafiti na kuzalisha mbegu bora kwa biashara.
hatuna haja ya kutegemea mataifa ya nje kwenye hili, tunaweza kuzalisha mali ghafi zetu wenyewe na kuwauzia nje bidhaa zinazotokana na bangi. Ni kujipanga tu.
Nafahamu Bashe utaweza hili kwa ufanisi mkubwa ukilivalia njuga. Weka legacy kijana kupitia bangi.
Nafahamu wengi wakisikia "bangi" akili zao zinakwenda katika kilevi cha bangi. Kilevi cha bangi ni matumizi duni ya bangi, ingawa na yenyewe inaweza kufanyiwa tafiti ikapatikana mbegu isiyo na madhara na ikauzwa kihalali kuliko hivi sasa tunaletewa mbegu za kutia watu wazimu. Mpaka skanka limejaa sasa hivi linaumiza vijana.
Tuondokane na ujinga na kufata watu wa magharibi. Tumepata elimu ili itukombowe siyo tuendelee kuwa wajinga wa kuburuzwa kama misukule, wanachotaka mabwana wakubwa ndiyo tukifate, ni wakati Tanzania tukajifanyia yetu wenyewe na hao wakubwa tuwaimbishe nyimbo tunazotaka sisi. Rasilimali tunazo, kwanini watuendeshe na mali zetu?
Uchumi tunao lakini tunaukalia, Nyerere. Kwa kudanganywa tu na nchi za magharibi tutaendelee kuwa watumwa wao daima.
Naamini ndani ya miaka mitatu ya kuruhusu zao la bangi na tafiti zake za kina, hatutakopa tena nje, sisi tutakuwa wakopeshaji.
Nawasilisha.
Pia, soma: Dodoma: Serikali kuanzisha kiwanda cha mafuta ya bangi
Zao la bangi za aina tofauti tofauti (different varieties of hemp) linastawi vizuri sana Tanzania. Ni wakati muafaka, tena tumechelewa sana, kuanzisha zao la bangi kwa faida. Zao la bangi linaweza kututowa kwenye umasikini kwa haraka sana.
Baadhi ya faida zinazotokana na zao la bangi ni pamoja na:
Dawa aina mbali mbali, zinazotumika hivi sasa mahospitalini na dawa mbadala.
Pia bangi inaweza kutengeza karatasi, inaweza kutengeza mbao, inaweza kutengeza, "vigae" vya kuezekea, "boards" mbali mbali za kujengea na kuundia fanicha, inaweza kutengeza bodi za magari ambazo ni bora kuliko za mabati.
Licha ya hayo, inaweza kutengeneza virutubisho mbali mbali vya kutumika na binadam, wanyama na mimea. Pamoja na madawa ya kuzuia wadudu wa mimea.
Pia bangi inaweza kutengeneza mafuta ya kutumika kwenye magari ambayo ni bora kuliko ethanol na methanol.
Kinachotakiwa kufanywa ni kuanza na aina moja au mbili ya bidhaa muhimu na kufunguliwa kituo maalum cha utafiti na kuzalisha mbegu bora kwa biashara.
hatuna haja ya kutegemea mataifa ya nje kwenye hili, tunaweza kuzalisha mali ghafi zetu wenyewe na kuwauzia nje bidhaa zinazotokana na bangi. Ni kujipanga tu.
Nafahamu Bashe utaweza hili kwa ufanisi mkubwa ukilivalia njuga. Weka legacy kijana kupitia bangi.
Nafahamu wengi wakisikia "bangi" akili zao zinakwenda katika kilevi cha bangi. Kilevi cha bangi ni matumizi duni ya bangi, ingawa na yenyewe inaweza kufanyiwa tafiti ikapatikana mbegu isiyo na madhara na ikauzwa kihalali kuliko hivi sasa tunaletewa mbegu za kutia watu wazimu. Mpaka skanka limejaa sasa hivi linaumiza vijana.
Tuondokane na ujinga na kufata watu wa magharibi. Tumepata elimu ili itukombowe siyo tuendelee kuwa wajinga wa kuburuzwa kama misukule, wanachotaka mabwana wakubwa ndiyo tukifate, ni wakati Tanzania tukajifanyia yetu wenyewe na hao wakubwa tuwaimbishe nyimbo tunazotaka sisi. Rasilimali tunazo, kwanini watuendeshe na mali zetu?
Uchumi tunao lakini tunaukalia, Nyerere. Kwa kudanganywa tu na nchi za magharibi tutaendelee kuwa watumwa wao daima.
Naamini ndani ya miaka mitatu ya kuruhusu zao la bangi na tafiti zake za kina, hatutakopa tena nje, sisi tutakuwa wakopeshaji.
Nawasilisha.
Pia, soma: Dodoma: Serikali kuanzisha kiwanda cha mafuta ya bangi