Waziri wa Kilimo, zao la bangi ni muhimu sana kwa maendeleo ya haraka

Waziri wa Kilimo, zao la bangi ni muhimu sana kwa maendeleo ya haraka

FaizaFoxy

Platinum Member
Joined
Apr 13, 2011
Posts
100,246
Reaction score
123,145
Mheshimiwa Hussein Bashe, natumai na Rais wetu mama Samia Suluhu Hasan na washauri wake wengine utawafikia ujumbe huu.

Zao la bangi za aina tofauti tofauti (different varieties of hemp) linastawi vizuri sana Tanzania. Ni wakati muafaka, tena tumechelewa sana, kuanzisha zao la bangi kwa faida. Zao la bangi linaweza kututowa kwenye umasikini kwa haraka sana.

Baadhi ya faida zinazotokana na zao la bangi ni pamoja na:

Dawa aina mbali mbali, zinazotumika hivi sasa mahospitalini na dawa mbadala.

Pia bangi inaweza kutengeza karatasi, inaweza kutengeza mbao, inaweza kutengeza, "vigae" vya kuezekea, "boards" mbali mbali za kujengea na kuundia fanicha, inaweza kutengeza bodi za magari ambazo ni bora kuliko za mabati.

Licha ya hayo, inaweza kutengeneza virutubisho mbali mbali vya kutumika na binadam, wanyama na mimea. Pamoja na madawa ya kuzuia wadudu wa mimea.

Pia bangi inaweza kutengeneza mafuta ya kutumika kwenye magari ambayo ni bora kuliko ethanol na methanol.

Kinachotakiwa kufanywa ni kuanza na aina moja au mbili ya bidhaa muhimu na kufunguliwa kituo maalum cha utafiti na kuzalisha mbegu bora kwa biashara.

hatuna haja ya kutegemea mataifa ya nje kwenye hili, tunaweza kuzalisha mali ghafi zetu wenyewe na kuwauzia nje bidhaa zinazotokana na bangi. Ni kujipanga tu.

Nafahamu Bashe utaweza hili kwa ufanisi mkubwa ukilivalia njuga. Weka legacy kijana kupitia bangi.

Nafahamu wengi wakisikia "bangi" akili zao zinakwenda katika kilevi cha bangi. Kilevi cha bangi ni matumizi duni ya bangi, ingawa na yenyewe inaweza kufanyiwa tafiti ikapatikana mbegu isiyo na madhara na ikauzwa kihalali kuliko hivi sasa tunaletewa mbegu za kutia watu wazimu. Mpaka skanka limejaa sasa hivi linaumiza vijana.

Tuondokane na ujinga na kufata watu wa magharibi. Tumepata elimu ili itukombowe siyo tuendelee kuwa wajinga wa kuburuzwa kama misukule, wanachotaka mabwana wakubwa ndiyo tukifate, ni wakati Tanzania tukajifanyia yetu wenyewe na hao wakubwa tuwaimbishe nyimbo tunazotaka sisi. Rasilimali tunazo, kwanini watuendeshe na mali zetu?

Uchumi tunao lakini tunaukalia, Nyerere. Kwa kudanganywa tu na nchi za magharibi tutaendelee kuwa watumwa wao daima.

Naamini ndani ya miaka mitatu ya kuruhusu zao la bangi na tafiti zake za kina, hatutakopa tena nje, sisi tutakuwa wakopeshaji.

Nawasilisha.

Pia, soma: Dodoma: Serikali kuanzisha kiwanda cha mafuta ya bangi
 
Tuanzishe na Bodii ya zaoo la bangi;,??

Siamini kwenye "bodi" naamini kwenye vituo vya tafiti.

Kituo cha tafiti kinaweza kuzofanya kazi za bodi na zaidi, kitaalam kabisa.

Tena namshauri Bashe, wachana na mambo ya bodi, anzisha vituo vya utafiti vitavyokuwa direct facilitators zinazosimamiwa na wizara zako.

Tuwe na "Research and development" za uhakika, badala ya bodi za wapigaji.
 
Endapo serikali itaona fursa katika kilimo hicho, basi ni vyema wakaanza na kutoa elimu kwa wananchi kwasababu bado wengi wanaamini bangi ni hatari na hawataki hata kuisikia.
Hilo sahihi kabisa, tulijazwa ujinga na wamagharibi wakalipiga marufuku zao muhimu sana lenye faida kwa faida zao tu.

Wametujaza ujinga kwa muda mrefu sana, ni wakati muafata tuwe huru kwa fikra na mawazo yetu.
 
Mheshimiwa Hussein Bashe, natumai na Rais wetu mama Samia Suluhu Hasan na washauri wake wengine utawafikia ujumbe huu.

Zao la bangi za aina tofauti (different varieties of hemp) linastawi vizuri sana Tanzania. Ni wakati muafaka, tena tumechelewa sana, kuanzisha zao la bangi kwa faida. Zao la bangi linaweza kututowa kwenye umasikini kwa haraka sana.

Baadhi ya faida zinazotokana na zao la bangi ni pamoja na:

Dawa aina mbali mbali, zinazotumika hivi sasa mahpspitalini na dawa mbadala.

Pia bangi inawe kutengeza karatasi, inaweza kutengeza mbao, inaweza kutengeza, "vigae" vya kuezekea, inaweza kutengeza bodi za gari ambazo ni bora kuliko za mabati.

Licha ya hayo, inaweza kutengeneza virutubisho mbali mbali vya aya ya binadam, wanyama na mimea. Pamoja na madawa ya kuzuia wadudu wa mimea.

Pia bangi inaweza kutengeza mafuta ya kutumika kwenye magari ambayo ni bora kuliko ethano na methanol.

Kinachotakiwa kufanywa ni kuanza na aina moja au mbili ya bidhaa muhimu na kufunguliwa kituo maalum cha utafito na kuzalisha mbegu bpora kwa biashara.

hatuna haja ya kutegemea mataifa ya nje kwenye hili, tunaweza kuzalisha mali ghafi zetu wenyewe na kuwauzia nje bidhaa zinazotokana na bangi. Ni kujipanga tu.

Nafahamu Bashe utaweza hili kwa ufanisi mkubwa ukilivalia njuga. Weka legacy kijana kupitia bangi.

Nafahamu wengi wakisikia "bangi" akili zao zinakwenda katika kilevi cha bangi. Kilevi cha bangi ni matumizi duni ya bangi, ingawa na yenyewe inaweza kufanyiwa tafiti ika[atikana mbegu isiyo na madhara na ikauzwa kihalali kuliko hivi sasa tunaletewa mbegu za kutia watu wazimu, mpaka skanka limejaa sasa hivi linaumiza vijana.

Tuondokane na ujinga na kufata watu, tumepata elimu ili ituukomboe siyo tuendelee kuwa wajinga wa kuburuzwa kama misukule, wanachotaka mabwana wakuba ndiyo tukifate, ni wakati Tanzania tukajifanyia yetu wenyewe na hao wakubwa tuwaimbishe nyimbo tunazotaka sisi. Rasilimali tunazo, kwanini watuendeshe na mali zetu?

Uchumi tuna tunaukalaia kwa kudanganywa na nchi za magharibi ili tuendelee kuwa watumwa wao daima.

Naamini ndani ya miaka ya kuruhusu zao la bangi na tafiti zake za kina, hatutako[pa tena nje, sisi tutakuwa wakopeshaji.

Nawasilisha.
professor wajackoyah: bangi heee
 
Hilo sahihi kabisa, tulijazwa ujinga na wamagharibi wakalipiga marufuku zao muhimu sana lenye faida kwa faida zao tu.

Wametujaza ujinga kwa muda mrefu sana, ni wakati muafata tuwe huru kwa fikra na mawazo yetu.
Sahihi kabisa, Pia wakulima wapewe vibali maalum sio kila mtu awe na uwezo wa kulima Bangi
 
Mkoa kama Arusha , wakilima huisafirisha Kenya ( njia za panya)...ikifika Kenya inasafirishwa kwenda Ethiopia (kwa njia za panya)

Ethiopia inasafirishwa kwenda Asia na nyingine inapelekwa kwenye viwanda vikubwa Canada ...

Rwanda walishaona fursa sana kwa Canada ..wana viwanda vingi vya kuprocess bangi hasa kwa matibabu ya cancer au wenye maumivu makali mwilini ..
 
Back
Top Bottom