Waziri wa Kilimo, zao la bangi ni muhimu sana kwa maendeleo ya haraka

Waziri wa Kilimo, zao la bangi ni muhimu sana kwa maendeleo ya haraka

Umesema vyema sana.

Kilimo cha bangi ni faida tupu.

1. Tanzania tukilima bangi ajira zitaongezeka kuanzia kwenye ulimaji wenyewe, uandaaji, watu watakaokuwa wanafanya research. Maelfu ya watu na familia zao watatoka kwenye umasikini wakipato.

2. Serikali ikiruhusu inapata kodi, makusanyo ya kodi yanaongezeka.

3. Mazao yanayotokana na bangi yatatumika viwandani. Kama alivyosema mwanzisha uzi, bangi inatumika kutengemeza nguo, vijaa vya ujenzi, mafuta kuanzia ya magari hadi kupaka kwenye ngozi yako. Hii ni pesa kwa watanzamia tutumie fursa hii.

4. Bangi ni dawa. Kama tukiruhusu kilimo cha bangi hiyo maana yake vituo vyetu vya utafiti wa dawa za binadamu vitaendelea kufanya utafiti na dawa nzuri zitatengenezwa kutibu watu wetu kuliko kutimia millions kununua bidhaa hiyohiyo kutoka nje. Tusiwe vipofu, tufungue macho tuone.

5. Kilimo cha bangi kinasaidia tourism kukua. Watu watatembelea mashamba yetu na vituo vyetu vya utafiti toka kote duniani kuja kujifunza.
 
Mheshimiwa Hussein Bashe, natumai na Rais wetu mama Samia Suluhu Hasan na washauri wake wengine utawafikia ujumbe huu.

Zao la bangi za aina tofauti (different varieties of hemp) linastawi vizuri sana Tanzania. Ni wakati muafaka, tena tumechelewa sana, kuanzisha zao la bangi kwa faida. Zao la bangi linaweza kututowa kwenye umasikini kwa haraka sana.

Baadhi ya faida zinazotokana na zao la bangi ni pamoja na:

Dawa aina mbali mbali, zinazotumika hivi sasa mahpspitalini na dawa mbadala.

Pia bangi inawe kutengeza karatasi, inaweza kutengeza mbao, inaweza kutengeza, "vigae" vya kuezekea, inaweza kutengeza bodi za gari ambazo ni bora kuliko za mabati.

Licha ya hayo, inaweza kutengeneza virutubisho mbali mbali vya aya ya binadam, wanyama na mimea. Pamoja na madawa ya kuzuia wadudu wa mimea.

Pia bangi inaweza kutengeza mafuta ya kutumika kwenye magari ambayo ni bora kuliko ethano na methanol.

Kinachotakiwa kufanywa ni kuanza na aina moja au mbili ya bidhaa muhimu na kufunguliwa kituo maalum cha utafito na kuzalisha mbegu bpora kwa biashara.

hatuna haja ya kutegemea mataifa ya nje kwenye hili, tunaweza kuzalisha mali ghafi zetu wenyewe na kuwauzia nje bidhaa zinazotokana na bangi. Ni kujipanga tu.

Nafahamu Bashe utaweza hili kwa ufanisi mkubwa ukilivalia njuga. Weka legacy kijana kupitia bangi.

Nafahamu wengi wakisikia "bangi" akili zao zinakwenda katika kilevi cha bangi. Kilevi cha bangi ni matumizi duni ya bangi, ingawa na yenyewe inaweza kufanyiwa tafiti ika[atikana mbegu isiyo na madhara na ikauzwa kihalali kuliko hivi sasa tunaletewa mbegu za kutia watu wazimu, mpaka skanka limejaa sasa hivi linaumiza vijana.

Tuondokane na ujinga na kufata watu, tumepata elimu ili ituukomboe siyo tuendelee kuwa wajinga wa kuburuzwa kama misukule, wanachotaka mabwana wakuba ndiyo tukifate, ni wakati Tanzania tukajifanyia yetu wenyewe na hao wakubwa tuwaimbishe nyimbo tunazotaka sisi. Rasilimali tunazo, kwanini watuendeshe na mali zetu?

Uchumi tuna tunaukalaia kwa kudanganywa na nchi za magharibi ili tuendelee kuwa watumwa wao daima.

Naamini ndani ya miaka ya kuruhusu zao la bangi na tafiti zake za kina, hatutako[pa tena nje, sisi tutakuwa wakopeshaji.

Nawasilisha.
Naunga hoja kwa mikono yote miwili 100% :DESKCHAN:. Kinachotakiwa kuboreshwa ni:-
1. Kui-review sheria kandamizi iliyopo sasa(Sio kuifuta) na kutoa elimu stahiki juu ya matumizi yake sahihi na watumiaji waelimshwe kwa kina madhara ya kuitumia hovyo hususan vijana.
2. Kuzitambua (Identify)aina zilizopo hapa Tz na kuzichuja/kuzipambanua ili kutenga aina iliyo bora zaidi na yenye uhitaji mkubwa kwenye soko. Hakuna maana ya eti mapolisi na wengineo kukimbizana na watumiaji au wakulima wa zao hili kwani ni upotevu usio wa lazma wa raslimali watu, muda na fedha za Serikali kwa jambo ambalo KAMWE hawatokaa wafaulu.
USHAURI:
1. Serikali ikubali kubadilisha mtizamo Hasi (Negative perception) dhidi ya zao hilo na kuanza kuliona kama ni zao potential kwa faida ya nchi yetu kiuchumi.
2. Serikali na Wataalam-kilimo na Watafiti waliopo wakae na kupanga mpango- mkakati (Strategic plan) wa namna ya kuliendeleza zao hilo.
3. Serikali iwe flexible, isikaze shingo (Rigidity) na iwasikilize wanaoshauri kwa nia njema.
BTW:
Kongole mtoa mada :HYPERCLAPHD:
 
Ni kubadili tu mtazamo. Bangi na Gongo ni bidhaa ambazo zikihalalishwa zinaweza kuchangia pato la Taifa. Tazama, tangu zimepigwa vita mbona ndiyo zinashamiri..!!!
 
Bravo kabisa madame FaizaFoxy yaani leo ndio siku iliyosisimua mishipa yangu kwa kuona kumbe uko timamu kiakili kuliko wanavyojaribu kukuchukulia poa humu ndani,

Bangi ina faida chanya asilimia 99%
Ila mapunguani hua wanaangalia hiyo 1%
yenye hasara
Tukitoka kwenye huo ujinga tutajikuta tunafanya mambo yenye Tija sana
Bangi ikiruhusiwa tu hakyanani kule Maskani Lupembe Njombe watatoka mabillionare wa kufa mtu maana inakubali ardhi ya kule hatari!
 
Mheshimiwa Hussein Bashe, natumai na Rais wetu mama Samia Suluhu Hasan na washauri wake wengine utawafikia ujumbe huu.

Zao la bangi za aina tofauti tofauti (different varieties of hemp) linastawi vizuri sana Tanzania. Ni wakati muafaka, tena tumechelewa sana, kuanzisha zao la bangi kwa faida. Zao la bangi linaweza kututowa kwenye umasikini kwa haraka sana.

Baadhi ya faida zinazotokana na zao la bangi ni pamoja na:

Dawa aina mbali mbali, zinazotumika hivi sasa mahospitalini na dawa mbadala.

Pia bangi inaweza kutengeza karatasi, inaweza kutengeza mbao, inaweza kutengeza, "vigae" vya kuezekea, "boards" mbali mbali za kujengea na kuundia fanicha, inaweza kutengeza bodi za magari ambazo ni bora kuliko za mabati.

Licha ya hayo, inaweza kutengeneza virutubisho mbali mbali vya kutumika na binadam, wanyama na mimea. Pamoja na madawa ya kuzuia wadudu wa mimea.

Pia bangi inaweza kutengeneza mafuta ya kutumika kwenye magari ambayo ni bora kuliko ethanol na methanol.

Kinachotakiwa kufanywa ni kuanza na aina moja au mbili ya bidhaa muhimu na kufunguliwa kituo maalum cha utafiti na kuzalisha mbegu bora kwa biashara.

hatuna haja ya kutegemea mataifa ya nje kwenye hili, tunaweza kuzalisha mali ghafi zetu wenyewe na kuwauzia nje bidhaa zinazotokana na bangi. Ni kujipanga tu.

Nafahamu Bashe utaweza hili kwa ufanisi mkubwa ukilivalia njuga. Weka legacy kijana kupitia bangi.

Nafahamu wengi wakisikia "bangi" akili zao zinakwenda katika kilevi cha bangi. Kilevi cha bangi ni matumizi duni ya bangi, ingawa na yenyewe inaweza kufanyiwa tafiti ikapatikana mbegu isiyo na madhara na ikauzwa kihalali kuliko hivi sasa tunaletewa mbegu za kutia watu wazimu. Mpaka skanka limejaa sasa hivi linaumiza vijana.

Tuondokane na ujinga na kufata watu wa magharibi. Tumepata elimu ili itukombowe siyo tuendelee kuwa wajinga wa kuburuzwa kama misukule, wanachotaka mabwana wakubwa ndiyo tukifate, ni wakati Tanzania tukajifanyia yetu wenyewe na hao wakubwa tuwaimbishe nyimbo tunazotaka sisi. Rasilimali tunazo, kwanini watuendeshe na mali zetu?

Uchumi tunao lakini tunaukalia, Nyerere. Kwa kudanganywa tu na nchi za magharibi tutaendelee kuwa watumwa wao daima.

Naamini ndani ya miaka mitatu ya kuruhusu zao la bangi na tafiti zake za kina, hatutakopa tena nje, sisi tutakuwa wakopeshaji.

Nawasilisha.
Wacha we,,Faiza mi 5 tena
 
Ingependeza ungetupa Somo, kwa nchi zilizoruhusu zimeongeza kiasi gani kwenye pato la taifa?

Hata bungeni kuna wabunge walizungumzia, Hivyo uko sahihi. Hasahasa ilimwe kwa ajili ya Export tu
 
BANGI! UTAZIBITI VP UVUTAJI WAKE? C VIJANA WOTE WATAKUWA MATAHIRA
Siasa tu hizo,,,,mbona pombe pia kuna baadhi ya watu hawaiwezi ila ipo inauzwa na athari zake zote za kiafya , bangi pia ingeruhusiwa kama pombe tu wanao iweza waendelee na wasio iweza waendelee na mengine
 
Maoni ya juu ya bandiko la Binti foxy

Ccm wanajua fika bangi ikahalalishwa basi vijana watakuwa na uthubutu na akiri fika ya kuwachomoa madarakani!!

Wavuta bangi wote hayupo muoga muoga wote Huwa wanajiamini kupindukia ukivuta bangi ikakuaa fresh hata gari la police unaliona nikasisimizi tu.

Ndio maana pale Kenyata bomu la chozi hidakwa jujuu na kirudishwa Kwa speed Ile Ile na sometimes watu hugeuka kuwa Ronald linazimwa kabla halijautua chini!!

Angalia pale Jamaica hakuna mvuta bange Ambae unaweza mpeleka lesi hivihiv tu hayupo labda awe kichaaa

Nini kifanyike naungana na Mzuri wangu FaizaFoxy kuwa Kuna mbegu nyingi nzuri na zisizo na madhara Kwa wavutaji.

Wote tunajua tumbuko Ina madhara lukuki
Pombe Zina madhara na hata soda lkn wapo walio chagua kutumia na wengine kutokutumia!!

Serkali sikieni hili wazo la kishimba aliwahi sema tumechelewa sana.
 
Ni kubadili tu mtazamo. Bangi na Gongo ni bidhaa ambazo zikihalalishwa zinaweza kuchangia pato la Taifa. Tazama, tangu zimepigwa vita mbona ndiyo zinashamiri..!!!
Ni kweli. Tatizo kubwa ni kwa viongozi na Wataalam (Tekanalojia na Maadili) kutokutambua na kukubali au kuzichunguza kwa undani baadhi ya Sheria kuona kama zimepitwa na wakati au ziliwekwa kimkakati enzi hizo kwa malengo ya kudhibiti ukuaji wa kiuchumi (ni vita)wa maendeleo ya Taifa na Watu wake na kuzifanyia marekebisho.
 
Ni kubadili tu mtazamo. Bangi na Gongo ni bidhaa ambazo zikihalalishwa zinaweza kuchangia pato la Taifa. Tazama, tangu zimepigwa vita mbona ndiyo zinashamiri..!!!
Gongo imesomesha mtoto wa shangazi saivi ni askari Huwa anaulizwa akija nyumbani vipi Huwa unawakamata ? Anakubali Huwa tunakamata muda huo walevi wa gongo wamejikojolea wapo hapo hapo nyumbani
 
Wewe unavuta?
Pombe unakunywa?
Sigara kawaida unavuta?
Ugoro unavuta?

Hata wakiruhusu cocaine iuzwe Bado kama hutumii hutumii tu Kuna walokole pamoja na kwamba Imani Yao inakata kunywa nyagi ila wanakunywa tu ni maamzi. Ahsantee
BANGI! UTAZIBITI VP UVUTAJI WAKE? C VIJANA WOTE WATAKUWA MATAHIRA
 
Gongo imesomesha mtoto wa shangazi saivi ni askari Huwa anaulizwa akija nyumbani vipi Huwa unawakamata ? Anakubali Huwa tunakamata muda walevi wa gongo wamejikojolea wapo hapo hapo nyumbani
Mi nakumbuka mzee mmoja alifungwa gerezani kwa kesi ya gongo. Siku ameachiliwa nikamuuliza, "Utakwenda kufanya kazi ya gongo tena?". Alinijibu kwa ujasiri kuwa hawezi kuacha kazi hiyo kwa sababu imemuwezesha kusomesha watoto wake, amefungua bucha mbili za nyama na ana nyumba za kupangisha. Alijinasibu kuwa biashara ya gongo kwake ni zaidi ya mgodi (madini), maana kule ni pata potea. Hiyo ilikuwa mwaka 1999 jijini Arusha.
 
Ingependeza ungetupa Somo, kwa nchi zilizoruhusu zimeongeza kiasi gani kwenye pato la taifa?

Hata bungeni kuna wabunge walizungumzia, Hivyo uko sahihi. Hasahasa ilimwe kwa ajili ya Export tu
Naomba hapa Hasahasa ilimwe kwa ajili ya Export tu parekebishwe kuwa kwa matumizi sahihi kwani hata ss waTz tunahitaji kuwa na vi wanda vyetu wenyewe vya kuichakata bangi kupata madawa yaliyomo ndani yake badala ya kuyaagiza madawa yatokanaya na bangi huko tulikoiuza tena kwa bei poa halafu bei ya madawa yatokanayo na bangi yetu wanatuuzia kwa bei mbaya.
 
Back
Top Bottom