Waziri wa Mambo ya Ndani, Eng. Masauni fuatilia pesa za makusanyo ya Wiki ya Nenda kwa Usalama. Zimepigwa?

Waziri wa Mambo ya Ndani, Eng. Masauni fuatilia pesa za makusanyo ya Wiki ya Nenda kwa Usalama. Zimepigwa?

Don Moen

JF-Expert Member
Joined
Nov 12, 2020
Posts
1,636
Reaction score
3,142
WAZIRI ENG. MASAUNI

Naomba nikurudishe nyuma kidogo, miaka miwili nyuma ukiwa naibu waziri wa mambo ya ndani, ukiwa kama mwenyeketi wa usalama barabarani uliagiza kila mkoa ukusanye fedha za WIKI YA NENDA KWA USALAMA ambazo hutozwa kuanzia tsh 3,000 hadi 5,000
kwa kulingana na ukubwa wa gari husika.

Baada ya makusanyo hayo ulielekeza kila Mkoa ununue magari kwa ajili ya kusaidia utendaji wa kazi katika ofisi za ma RTO wa mikoa.

Katika maagizo yako hayo karibu mikoa yote ilijitahidi kukusanya kwa uaminifu na kutekeleza agizo lako kuwa walinunua magari kulingana na makusanyo ambapo mikoa iliyokusanya kidogo ilijitahidi kunua hata Noah.

Pamoja na mikoa mingine kutii agizo lako hilo. lakini Mikoa ya kipolisi ya Kinondoni, Ilala na Temeke haikutekeleza agizo lako hilo matokeo yake kuna tetesi kuwa Ofisi ya Kanda ilikusanya pesa zote na zikaishia mikononi mwa wajanja wachache.

Hivyo lengo la agizo lako halikutimizwa. Ili kuupata ukweli wa hili ni kazi rahisi tu ni kuwaita hao ma RTO watakueleza walipoelekeza hizo pesa.

Katika hili unayo nafasi nzuri ya kulifuatilia hili kwani sasa wewe ni Waziri kamili na hili lilikuwa agizo lako mwemyewe.

Mikoa hiyo ya kipolisi kwa ujumla haikosi kuwa na magari yasiyopungua 500,000 na ukizidisha kwa bei ya wastani ya 3,000x500,000=1,500,000,000. Hii ni pesa nyingi zingeweza kulisaidia jeshi la polisi. Naomba nisiwataje wahusika bali jaribu kufuatilia mwenyewe ndani ya muda mfupi utakua na majibu.

Mungu abariki utendaji wako.
 
Wenye bigari tunavyokamuliwa kila uchao na bado zinapigwa wakuu?
 
Zinapigwaje wakati mtoaji ni mmoja, sidhani kama wapigaji ni polisi labda wakipiga walizoletewa kwa ajiri ya shughuli flan lkn sio makusanyo.
 
Zinapigwaje wakati mtoaji ni mmoja, sidhani kama wapigaji ni polisi labda wakipiga walizoletewa kwa ajiri ya shughuli flan lkn sio makusanyo.
Mbona uzi uko wazi?
Hizi hazikusanywi kwa mashine bali unapokwenda kulipia stika ya nenda kwa usalama unampatia mkusanyaji mkononi
 
Bwashee hao waliozikula kwani hawakula kwa urefu wa kamba zao? Au walijirefushia kamba zao kwa kuunganisha na vipande vya kamba za wengine?

Naamini mh waziri atafuatilia.
Haha hii nafikiri ilikuwa enzi ya kayafa
 
Inaonekana wewe ni traffic mziko umekupita kushoto mkuu, kila mtu ale kwa urefu wa kamba ake
 
Bwashee hao waliozikula kwani hawakula kwa urefu wa kamba zao? Au walijirefushia kamba zao kwa kuunganisha na vipande vya kamba za wengine?

Naamini mh waziri atafuatilia.
Mkuu sijaleta uzi huu kwa fitina kwa kubahatisha bali najua fika chain nzima ya utafunaji na waliofaidi zaidi ni wawili mkuu wa kanda na mkulu wa mkuu wa kitengo.

Hadi ilikotumika katika uwekezaji binafsi.
Nikifunguka kwenye uzi mods wata ufuta kwa kigezo cha kuthibitisha.

Nikithibitisha waziwazi lazima identity yangu itatambuliwa mara moja.
 
Zinakusanywa bila control number? hapo lazima utengenezee watu ulaji na serikali kukosa mapato....
 
Back
Top Bottom