Phillipo Bukililo
JF-Expert Member
- Dec 29, 2015
- 18,487
- 13,611
Jumatatu Majaliwa anakwenda MSD akiongozana na Hamduni wa TAKUKURU na Mkuu wa Polisi, huo ni mfano mmoja tu wa madudu yetu watanzania.Ninalitambua hilo mkuu,ninajiamini mimi ni mtenda kazi ila nchi yetu wanaofaidi ni watu wajanja ndani ya CCM&System zao.Hawana ubunifu ndiyo maana nchi imekuwa omba omba wa misaada duniani pamoja na raslimali ilizonazo.
Watanzania ni wachapa kazi na watiifu mno ndiyo maana kuna watawala wanaostarehe kufuru kwa jasho letu.Ukitaka kuwafahamu waroho hao wa madaraka watajie madai ya Katiba mpya au hitaji la tume huru ya uchaguzi usikie wanavyong'aka.
Ni wazuri mno kwa kujenga hoja za kujitetea lakini wabovu sana kulinganisha na Wakenya au Waganda.