ChoiceVariable
JF-Expert Member
- May 23, 2017
- 66,537
- 75,687
Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega amewataka wataalamu wa sekta ya ujenzi kubuni mbinu za kupunguza foleni mijini na kuongeza mapato ya Serikali kupitia barabara za mwendokasi huku akipendekeza zitumiwe na magari binafsi kwa kulipia.
Akizungumza leo Alhamisi Februari 13, 2025 mkoani kwenye Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo mkoani Singida, Ulega alipendekeza mfumo wa kulipia kwa magari binafsi ili kutumia njia za Mabasi Yaendayo Haraka (BRT) wakati wa msongamano mkubwa.
"Kwa nini barabara moja ibaki tupu kwa muda mrefu wakati magari mengine yamekwama kwenye foleni? Nchi nyingine zinatumia mfumo wa kulipia ili kuepuka foleni, tunaweza kufanya hivyo hapa pia," amesema Ulega.
Aidha, Ulega amesisitiza juu ya umuhimu wa kuzingatia thamani ya fedha katika usimamizi wa miradi ya barabara, madaraja, na viwanja vya ndege, huku akiagiza Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads) kusimamia miradi ya dharura yenye thamani ya Sh868.56 bilioni.
Mkutano huo pia umejadili bajeti ya wizara kwa mwaka wa fedha 2025/26 kabla ya kuwasilishwa bungeni
Akizungumza leo Alhamisi Februari 13, 2025 mkoani kwenye Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo mkoani Singida, Ulega alipendekeza mfumo wa kulipia kwa magari binafsi ili kutumia njia za Mabasi Yaendayo Haraka (BRT) wakati wa msongamano mkubwa.
"Kwa nini barabara moja ibaki tupu kwa muda mrefu wakati magari mengine yamekwama kwenye foleni? Nchi nyingine zinatumia mfumo wa kulipia ili kuepuka foleni, tunaweza kufanya hivyo hapa pia," amesema Ulega.
Aidha, Ulega amesisitiza juu ya umuhimu wa kuzingatia thamani ya fedha katika usimamizi wa miradi ya barabara, madaraja, na viwanja vya ndege, huku akiagiza Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads) kusimamia miradi ya dharura yenye thamani ya Sh868.56 bilioni.
Mkutano huo pia umejadili bajeti ya wizara kwa mwaka wa fedha 2025/26 kabla ya kuwasilishwa bungeni