Waziri Ulega apendekeza Watu binafsi kutumia barabara za Mwendokasi kwa kulipia

Waziri Ulega apendekeza Watu binafsi kutumia barabara za Mwendokasi kwa kulipia

ChoiceVariable

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2017
Posts
66,537
Reaction score
75,687
Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega amewataka wataalamu wa sekta ya ujenzi kubuni mbinu za kupunguza foleni mijini na kuongeza mapato ya Serikali kupitia barabara za mwendokasi huku akipendekeza zitumiwe na magari binafsi kwa kulipia.

Akizungumza leo Alhamisi Februari 13, 2025 mkoani kwenye Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo mkoani Singida, Ulega alipendekeza mfumo wa kulipia kwa magari binafsi ili kutumia njia za Mabasi Yaendayo Haraka (BRT) wakati wa msongamano mkubwa.

"Kwa nini barabara moja ibaki tupu kwa muda mrefu wakati magari mengine yamekwama kwenye foleni? Nchi nyingine zinatumia mfumo wa kulipia ili kuepuka foleni, tunaweza kufanya hivyo hapa pia," amesema Ulega.

Aidha, Ulega amesisitiza juu ya umuhimu wa kuzingatia thamani ya fedha katika usimamizi wa miradi ya barabara, madaraja, na viwanja vya ndege, huku akiagiza Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads) kusimamia miradi ya dharura yenye thamani ya Sh868.56 bilioni.

Mkutano huo pia umejadili bajeti ya wizara kwa mwaka wa fedha 2025/26 kabla ya kuwasilishwa bungeni


 
My Take
Binafsi naona ni pendekezo zuri ambalo kitakuwa chanzo Cha Mapato na pia kusaidia kumrudisha hela za Mkopo.

Serikali ilizongatie 👇👇

View: https://www.instagram.com/p/DGBOTPrNpWS/?igsh=dXN1d2p2cGx0Y291

Huyo ni mwendawazimu kweli kweli, hivi anajua malengo ya mwendokasi ni yapi? Kwahiyo mabasi yapambane tena na foleni? Hiyo itakuwa ni mwendokasi sasa?

Mabasi ya mwendokasi yanaitwa mwendokasi sio sababu yanaenda speed kubwa, la hasha, bali yanaitwa hivyo sababu yanapita njia isiyo na foleni, hivyo yanafika haraka.., na lengo ni watu waache magari binafsi nyumbani yanayokaa foleni na badala yake watumie usafiri wa umma usio na foleni. Sasa ukiruhusu gari binafsi zipite kwa kulipia , mwisho wa siku mwendokasi nayo itakuwa na foleni kama barabara ya kawaida, na kuharibu malengo yote ya mradi. sasa utaahira kama huu kweli mtu anapendekeza kabisa bila aibu.., jamani, hizi taka taka za namna hii zinapataje uwaziri.., how?!!!
 
Public service huduma muhimu hazihitaji malipo. Don't create classes. This is something government should avoid to do
Tatizo lako la kutosafiri duniani ndilo hili
Unaonyesha ushamba wako .Barabara za serikali za kulipia ziko nyingi tu duniani huko

Daraja tu la kigamboni la kulipia na ni la setikali kama hutaki kulipia unapita barabara ya mbagala kwenda kigamboni
 
Tatizo lako la kutosafiri duniani ndilo hili
Unaonyesha ushamba wako .Barabara za serikali za kulipia ziko nyingi tu duniani huko

Daraja tu la kigamboni la kulipia na ni la setikali kama hutaki kulipia unapita barabara ya mbagala kwenda kigamboni
Sio za mwendo kasi hizi za hapa mjini. Nashukuru kwa kuniita mshamba
 
Back
Top Bottom