Wazo Muflisi: Alijaribu Kujitenga lakini Anarudi Bila Tenga...

Wazo Muflisi: Alijaribu Kujitenga lakini Anarudi Bila Tenga...

Ndio maana Kuna wakati unawaza mambo yasiwezekana mfano Bora nchi wakabidhiwe consultants waendeshe. Tuwe na Rais kama mfalme Kwa maana ya Alana tu ya mamlaka ya taifa.

Hao jamaa wakamate Kila kitu. Kuanzia kukusanya Kodi, kusimamia uendeshaji wa miradi na mambo yote Kwa mujibu wa dira na malengo ya taifa.

Kurekebisha hili tatizo kwenye jamii itatuchukua muda sana, na hasa Kwa vile hatuanfalii chanzo Cha tatizo, tutaangalia matokeo ya tatizo.
EEEEEeeeeNNNnnnHEEEeee. 'The Monk', Bhwanah!

Nadharia hiyo ya 'consultants' nilisha igusia sana humu kutokana na viongozi wetu hawa kudhani kuwa sisi wenyewe (waTanzania) hatuna uwezo wa kufanya lolote la maana katika maendeleo ya nchi yetu na kwa hiyo wao wakiamini kila jambo wapewe watu toka nje kuja kuliendesha. Huwa nashindwa kujua kwa nini viongozi hao hao wao hawajijumuishi katika hao waTanzania wengine; kwa maana kwamba nafasi zao huwa hawafikirii kamwe zitafutiwe watu toka nje kuja kuzisimamia.
Swala la 'consultants' sina tatizo nalo kabisa, nisilo kubaliana nalo ni fikra za kudhani waTanzania hawawezi kufanya vizuri katika nyanja hizo hizo tunazo watafuta 'consultants'. Mbaya zaidi ni hapo hawa viongozi wetu wanapofikiri kuwa hata uwezo wa kujifunza mambo tusiyo yajuwa kwa sasa, sisi waTanzania hatuna. Fikra za namna hii zinaua moyo wa taifa, na kulifanya liwe tegemezi miaka yote.

Kwa maoni yangu, kinacho takiwa kwa nchi yoyote , ni kwa wananchi wake kujiamini kwamba wanaweza kufanya kinachoweza kufanywa na binaadam mwingine yeyote katika kuleta maendeleo yetu. Viongozi wanatakiwa wawe mstari wa mbele kusukuma moyo huo wa uthubutu wa wananchi, siyo kuwakatisha tamaa.

Tatizo ni moja tu. Kukosekana kwa viongozi wenye uamini huo na kuweka taratibu za kusimamia juhudi hizo ziwe na ufanisi.
 
Nimesema hili zaidi ya mara Elfu,Elimu ya Tanzania inatengeneza wapiga kura wajinga,watoto wajinga,wazazi wajinga,viongozi wajinga...walimu wajinga,future itakuaje bright??hata rais awe smart kiasi gani,waliomzunguka??anao watawala??..
...Rais mjinga....😁
 
EEEEEeeeeNNNnnnHEEEeee. 'The Monk', Bhwanah!

Nadharia hiyo ya 'consultants' nilisha igusia sana humu kutokana na viongozi wetu hawa kudhani kuwa sisi wenyewe (waTanzania) hatuna uwezo wa kufanya lolote la maana katika maendeleo ya nchi yetu na kwa hiyo wao wakiamini kila jambo wapewe watu toka nje kuja kuliendesha. Huwa nashindwa kujua kwa nini viongozi hao hao wao hawajijumuishi katika hao waTanzania wengine; kwa maana kwamba nafasi zao huwa hawafikirii kamwe zitafutiwe watu toka nje kuja kuzisimamia.
Swala la 'consultants' sina tatizo nalo kabisa, nisilo kubaliana nalo ni fikra za kudhani waTanzania hawawezi kufanya vizuri katika nyanja hizo hizo tunazo watafuta 'consultants'. Mbaya zaidi ni hapo hawa viongozi wetu wanapofikiri kuwa hata uwezo wa kujifunza mambo tusiyo yajuwa kwa sasa, sisi waTanzania hatuna. Fikra za namna hii zinaua moyo wa taifa, na kulifanya liwe tegemezi miaka yote.

Kwa maoni yangu, kinacho takiwa kwa nchi yoyote , ni kwa wananchi wake kujiamini kwamba wanaweza kufanya kinachoweza kufanywa na binaadam mwingine yeyote katika kuleta maendeleo yetu. Viongozi wanatakiwa wawe mstari wa mbele kusukuma moyo huo wa uthubutu wa wananchi, siyo kuwakatisha tamaa.

Tatizo ni moja tu. Kukosekana kwa viongozi wenye uamini huo na kuweka taratibu za kusimamia juhudi hizo ziwe na ufanisi.

Nakuelewa sana Mkuu, huenda nikawa nimetumia neno "consultant" isivyopaswa kulingana na hoja iliyopo mezani lakini nnachotaka kusema, tubinafsidhe uendeshaji wa nchi, ipelekwe kama kampuni. Hapo zingatia sijasema kampuni iwe ya nje au ya ndani.
 
Nakuelewa sana Mkuu, huenda nikawa nimetumia neno "consultant" isivyopaswa kulingana na hoja iliyopo mezani lakini nnachotaka kusema, tubinafsidhe uendeshaji wa nchi, ipelekwe kama kampuni. Hapo zingatia sijasema kampuni iwe ya nje au ya ndani.
Yaani serikali iwe "Kampuni/ifanye kazi zake kama Kampuni"? Rais awe CEO wa kampuni hiyo! Mawaziri na watumishi wengineo serikalini wawe ni watumishi wa Kampuni.

Sioni tatizo na muundo huo, isipokuwa inapokuja kwa 'consultants' hao kuwa ni watu kutoka nje. Nchi (sovereign) ina mambo mengi sana yanayo hitaji wa 'consultant' hao kuwa wa ndani. Tuli wahi kuwa na wakoloni hapa; sijui kama kuna uwezekano tena wa kutaka kuwaleta wengine, hata kama jukumu lao ni la kusimamia shughuli za kiserikali tu bila maswala mengineyo.

Maana ya yote haya, ni kwamba hata jeshi, polisi na vyombo vingine vyote itabidi tutafute watu wa kuviendesha kwa ufanisi!

Mimi naamini kitu kimoja tu siku hizi: kwamba waTanzania wanao uwezo, na wapo tayari kufanya mambo yao kwa ufanisi mkubwa; bila ya ufusadi, wizi, ulaghai wa aina yoyote ile, iwapo tutabahatika kumpata kiongozi/viongozi wanaotaka iwe hivyo.

WaTanzania siyo wavivu, siyo wapiga soga na kutotekeleza kazi zao maofisini ipasavyo, n.k., n.k.,. Kunatakiwa pawe na viongozi watakao weka mfumo, taratibu za kufanya mambo yetu kwa weledi. Wanchi wakiliona hili, watafuata mstari, na hakuna kuchekeana tena wakati mali ya umma inateketezwa, au kazi ofisini zinafanywa kama ni utashi tu wa mtu kuzifanya.

Sisi hatuna tofauti yoyote na wachina, wakorea Kusini, wajapan na wengi wengineo. Tofauti yetu pekee ni kwamba hatuna viongozi wenye maono ya kutuelekeza katika mlengo huo wa wengine.
 
Back
Top Bottom