SHETANI HUKAA NA SHETANI WENZIE.Waliomzunguka sio wacha MUNGU ni mashetani watupu na wafuasi wa bwana Yule..hakuna la maana hapo
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
SHETANI HUKAA NA SHETANI WENZIE.Waliomzunguka sio wacha MUNGU ni mashetani watupu na wafuasi wa bwana Yule..hakuna la maana hapo
Tatizo siyo bwana yule na wala siyo bibi huyu, bali tatizo ni kwamba Katiba tuliyonayo ni mbovu na Sheria zilizopo ni kandamizi, hazifai.Na. M. M. Mwanakijiji
Rais Samia alitaka kupendwa. Rais Samia alitaka kukubalika. Rais Samia alitaka kuoenakana yeye siyo kama yule. Baada ya kuapishwa kufuatia maombolezo ya kifo cha Bw. Yule mara moja watu walianza kusema sasa "wanashusha pumzi". Wapo watu walisherehekea na wakajua kuwa sasa angalau wanaweza kuhema. Hali ya kuwa roho juu kisa bwana yule asiyelala na mwenye kukesha na mafaili hadi chumbani ikashuka. Watu wakaanza kutembea na kuchekeana bila kuogopana.
Upinzani ulishukuru zaidi kwana Bw. Yule aliwabana kweli kweli. Lakini upinzani dhidi yake ulikuwa wazi kabisa na kamili; mgogoro wake na upinzani na dhana ya demokrasia watu waliijua kabla hajaingia madarakani. Hakuwahi kuwa na ahadi za kidemokrasia hata kama aliziimba kidogo. Watu walijua kuwa yeye alichotaka ni "kazi" watu wakakutane kwenye kampeni. Hakutaka kuendekeza siasa za kushindana; walipojaribu kujitutumua vyombo vya dola vya nchi hii vikaingia kumfanya Bw. Yule atawale bila kuzingwazingwa.
Wale wajomba zetu walipojaribu kusema hakuwapepesea macho; na aliwaonesha kweli yeye hawajali kivile pale alipokataa kabisa kwenda kubeba tenga lake kulipeleka huko waliko kuwaomba. Kama aliwaomba aliwataka wao waje kwake ndio awaombe. Tena waje na matenga yao kwanza! Alikataa sana ile hali ya "kujidhalilisha". Sasa Rais Samia alipoingia madarakani siyo tu alitaka kupendwa na watendaji serikali ambao walikuwa roho juu hata kwenda Dubai ilikuwa Mbinde bali alitaka kupendwa na wajomba zetu huko nchi za Magharibi. Rais Samia katika kupendwa huko akaamua kujitenga kimaono na kiutendaji na Bw. Yule.
Bw. Yule alikuwa anafokafoka; mama hakasema yeye hafoki. Huku kijijini Mama akaanza kujulikana kwa "Mama Nahaya Mkayaangilie". Mama hakutaka watu waondoke wamenuna; alijua kuwabembeleza na hata akiwatimua kazi hakutaka wajue ni yeye amechukizwa. Mama akakwepa kabisa kutimua watendaji wabovu papo kwa papo japo anafanya hivyo kimya kimya. Niliandika mahali kuwa Rais Samia ni Simba Mwendapole.
Sasa haya ya juzi ndio yamefunua kuwa jani halitui mbali ya mti na kuwa atapikaye hutapika mbele yake. Mama alijaribu kuwapendeza wapinzani, amejaribu kuwatetea watu wabovu na kwa namna alibariki ulaji wa "urefu wa kamba zao" kumbe wajanja wakala na kamba zenyewe! Mama ambaye alisifiwa kuwa yeye hafokei watu juzi kwenye sherehe za Miaka 60 ya Jeshi la Polisi Mama akajikuta amegeuka kama Bw. Yule.
Yaani, kama hotuba ile ingetolewa kwa sauti ya Bw. Yule kuna watu wangebeba mashada ya maua na kumwambia mama kumbe umerudi! Sasa alivyojitenga vyote vile, na juhudi zote za 4R zimekuwa sasa ni juhudi za 4K - Kugeukana, Kukimbizana, Kutoleana Macho na Kupigana Mikwara! Alijaribu kujitenga na habari za Bw. Yule; lakini sasa karudi tena karudi na naona na tenga analipiga mkwara. Tunakoelekea jina la Bw. Yule litaanza kuimbwa mbele zake kama alama za kumuunga mkono.
Tofauti yake na Nchimbi ni hii;Mama mbona wasiwasi wake tu?
Alikuwa nayo nafasi ya kusimama katika haki na akaungwa mkono na walio wengi.
Nchimbi mbona anaongea lugha nzuri na anaeleweka?Kwani angeongea kama Nchimbi shida ilikuwa wapi?
Asingekubaliana na teka teka nani angekuwa na taabu naye?
Tatizo lake kulewa madaraka akisikia katiba mpya anaona urais wake 2025 unakuja kwenda na maji.
Laiti angejikita kwenye kujenga legacy yake kuliko 2025 mbona alikuwa na yote ya kupata?
Alipo sasa na ajiangalie asije akaanguka.
Kwani yaliisha je na yule mwamba aliyeambiwa mgombea shuruti awe mwanamke?
Ni kweli… kama hii nchi hatukutakiwa kupewa uhuru kabisa, tulitakiwa tuendelee kutawaliwa na wakoloni.Mtu mweusi huwa hapewi uhuru hata siku moja
Kazi ya Mungu ata Hangaya ndiyo anaandaliwa hivyo asiposhituka na kujiuzuru.Hilo lako kweli ni wazo muflis, kabisa tena.
Kazi ya Mungu haina makosa.
= Unabadilisha.Kazi ya Mungu ata Hangaya ndiyo anaandaliwa hivyo asiposhituka na kujiuzuru.
Unabadirisha Wakurugenzi wa TISS kama Wakuu wa Wilaya!🤣🤣🤣.
Ile hotuba ya juzi ni michezo anayochezewa;na atachezeshwa lege mpaka afurahi yaani.
Mwambieni vyombo vya usalama na ulinzi vina taratibu zake haviingiliwi,ameyatimba, mwambieni akae pembeni kwa usalama wake!!
Wazo lako lingekuwa na maana kama ungesema serikali ifute mfumo wa demokrasia ya vyama vingi. Vinginevyo, ni ujinga mkubwa kusema arudishe siasa za kuwashughulikia wapinzani. Kama hawatakiwi, kwa nini mruhusu wawepo kisheria, in the first place?Nilikuwa wa kwanza kusema Mama arudishe siasa za kuwashughulikia Wapinzani bila kuingiza mambo hayo kwenye uchumi.
Mifano Iko Mingi sana kuanzia Uganda,Rwanda,Egypt,China nk.
Bwana wako yule alikuwa haelewi yeye akaleta chuki zake Hadi kwenye Uchumi,Hali ikawa mbaya wawekezaji wakakimbia, account zikaanza kufungwa ,watu kubambikiwa Kodi Kwa sababu pesa imepungua na Biashara kukaba kiasi kwamba vilio vya vyuma kukaza vilitamalaki.
Rais awashughulikie Wanasiasa uchwara na vibaraka wote ila silete siasa za ujamaa hapa.
Mwisho kama unaembeba habebeki unategemea uendelee kumbeba? Una mdamp tuu unasonga mbele mwenyewe.
Hujaelewa ujumbe...Kwahiyo ni kwamba unaunga mkono mauaji na jinsi Magufuli alivyowafanyia waliompinga ndio unaona ni njia sahihi akitumia Samia pia?
Hakika ...hata kwenye andiko la MM kwa jicho la Tatu ...la sisi wachache unaliona tatizo!Samia si tatizo letu.
Samia ni dalili tu ya tatizo letu.
Na kila tunavyo focus kwenye dalili ya tatizo na kuacha kuangalia tatizo lenyewe, tunazidisha tatizo.
Halafu MM anatushawishi tumkumbuke😭 labda tulinganishe!Magufuli alikuwa-
1. Alizuia shughuli halali za vyama vya siasa hususan mikutano na maandamano
2. Alikuwa ameitisha Mahakama iamue kwa kuipendelea Serikali
3. Aliliteka Bunge likawa kama kitengo cha Ikulu
4. Alinyang'anya fedha za wafanyabiashara na kuwatupa rumande bila makosa
5. Alikuwa MWONGO sana kwa kuwa alijuwa Watanzania ni wajinga. Alidai anajenga miradi kwa fedha za ndani kumbe anakopa kwenye mabenki ya nje
6. Alidhibiti uhuru wa maoni na kuvitisha kuvifungia vyombo huru vya habari ambavyo vingeripoti kinyume na matakwa yake
7. Aliiba uchaguzi wote wa 2020 na kutuachia wabunge aliowateua yeye
Huna akili wewe.Ni ngumu kumwepuka bwana yule. Njia aliyoichagua amegundua haimfikishi salama.
Any way ngumu sana kuaapply "demokrasia" kwa mtu mweusi halafu utegemee matokeo chanya. Njia ya bwana yule ndiyo demokrasia sahihi kwa mwafrika hii ya mzungu ni sahihi kwao
Tanzania hakuna siasa za Vyama vingi ni maigizo.Wazo lako lingekuwa na maana kama ungesema serikali ifute mfumo wa demokrasia ya vyama vingi. Vinginevyo, ni ujinga mkubwa kusema arudishe siasa za kuwashughulikia wapinzani. Kama hawatakiwi, kwa nini mruhusu wawepo kisheria, in the first place?
Sikuelewa Magufuli alipoweka lengo la “kumaliza” upinzani kufikia 2020. Kama ilikuwa ni kwa kubadili sheria na katiba au kuondoa mawazo ya upinzani vichwani mwa watanzania wote!? Mawazo ya ajabu sana haya.
Halafu ni vigezo vipi vinavyopima wanasiasa uchwara na vibaraka? Na ni nani huyo mwenye mamlaka ya kupima na kuamua mambo hayo (regulator)?
Vigezo ni simple tuu,angalia Wapinzani wakibanwa Huwa wanapeleka wapi Malalakiko Yao? Je ni Kwa Umma? Jibu ni hapana ni Kwa Mabeberu na familia na Mapato ya shughuli zao za siasa zinafadhiliwa na Mabeberu ,so Hawa ni watu hatari Kwa mstakabali wa Nchi.
Nijuavyo nchi inatakiwa kuendeshwa kwa AKILI na MAARIFA kwa sheria, kanuni na taratibu na si kwa HISIA za misimu.
Sifa za kuwa Kiongozi ni zipi huko kwenu ambazo ziko tuned?Huyu wako hata ungemfunga mgongoni kwako uwe unampa maelekezo unayodhani ni mazuri kwenu, bado nyote mtaanguka tu; kwa sababu akili zenu haziko 'tuned' kuwa viongozi.
Sasa anagalia kwa mfano haya uliyo andika hapa, na wewe mwenyewe umetoa hoja iliyo nyooka. Hata hujui 'ujamaa' ni nini, wala ubepari nao hujui unahusu nini!
Unaloweza kufanya ni kutapika tu uliyo jifunza vitabuni miaka kadhaa iliyopita wakati vita baridi ingali inaendelea!
Muda si mrefu watanzania watapewa fursa nyingine adhimu ya kujionea tena kwamba haina makosa.Hilo lako kweli ni wazo muflis, kabisa tena.
Kazi ya Mungu haina makosa.
alisema mtanikumbuka wao wakakazana kufanya asikumbukwe kwa kuonyesha mabaya yake na sasa sio muda mrefu watamkumbuka kwa mazuriNa. M. M. Mwanakijiji
Rais Samia alitaka kupendwa. Rais Samia alitaka kukubalika. Rais Samia alitaka kuoenakana yeye siyo kama yule. Baada ya kuapishwa kufuatia maombolezo ya kifo cha Bw. Yule mara moja watu walianza kusema sasa "wanashusha pumzi". Wapo watu walisherehekea na wakajua kuwa sasa angalau wanaweza kuhema. Hali ya kuwa roho juu kisa bwana yule asiyelala na mwenye kukesha na mafaili hadi chumbani ikashuka. Watu wakaanza kutembea na kuchekeana bila kuogopana.
Upinzani ulishukuru zaidi kwana Bw. Yule aliwabana kweli kweli. Lakini upinzani dhidi yake ulikuwa wazi kabisa na kamili; mgogoro wake na upinzani na dhana ya demokrasia watu waliijua kabla hajaingia madarakani. Hakuwahi kuwa na ahadi za kidemokrasia hata kama aliziimba kidogo. Watu walijua kuwa yeye alichotaka ni "kazi" watu wakakutane kwenye kampeni. Hakutaka kuendekeza siasa za kushindana; walipojaribu kujitutumua vyombo vya dola vya nchi hii vikaingia kumfanya Bw. Yule atawale bila kuzingwazingwa.
Wale wajomba zetu walipojaribu kusema hakuwapepesea macho; na aliwaonesha kweli yeye hawajali kivile pale alipokataa kabisa kwenda kubeba tenga lake kulipeleka huko waliko kuwaomba. Kama aliwaomba aliwataka wao waje kwake ndio awaombe. Tena waje na matenga yao kwanza! Alikataa sana ile hali ya "kujidhalilisha". Sasa Rais Samia alipoingia madarakani siyo tu alitaka kupendwa na watendaji serikali ambao walikuwa roho juu hata kwenda Dubai ilikuwa Mbinde bali alitaka kupendwa na wajomba zetu huko nchi za Magharibi. Rais Samia katika kupendwa huko akaamua kujitenga kimaono na kiutendaji na Bw. Yule.
Bw. Yule alikuwa anafokafoka; mama hakasema yeye hafoki. Huku kijijini Mama akaanza kujulikana kwa "Mama Nahaya Mkayaangilie". Mama hakutaka watu waondoke wamenuna; alijua kuwabembeleza na hata akiwatimua kazi hakutaka wajue ni yeye amechukizwa. Mama akakwepa kabisa kutimua watendaji wabovu papo kwa papo japo anafanya hivyo kimya kimya. Niliandika mahali kuwa Rais Samia ni Simba Mwendapole.
Sasa haya ya juzi ndio yamefunua kuwa jani halitui mbali ya mti na kuwa atapikaye hutapika mbele yake. Mama alijaribu kuwapendeza wapinzani, amejaribu kuwatetea watu wabovu na kwa namna alibariki ulaji wa "urefu wa kamba zao" kumbe wajanja wakala na kamba zenyewe! Mama ambaye alisifiwa kuwa yeye hafokei watu juzi kwenye sherehe za Miaka 60 ya Jeshi la Polisi Mama akajikuta amegeuka kama Bw. Yule.
Yaani, kama hotuba ile ingetolewa kwa sauti ya Bw. Yule kuna watu wangebeba mashada ya maua na kumwambia mama kumbe umerudi! Sasa alivyojitenga vyote vile, na juhudi zote za 4R zimekuwa sasa ni juhudi za 4K - Kugeukana, Kukimbizana, Kutoleana Macho na Kupigana Mikwara! Alijaribu kujitenga na habari za Bw. Yule; lakini sasa karudi tena karudi na naona na tenga analipiga mkwara. Tunakoelekea jina la Bw. Yule litaanza kuimbwa mbele zake kama alama za kumuunga mkono.
Tatizo karibu wote tunamuangalia rais kama ugonjwa, wakati rais ni dalili ya ugonjwa tu.
Ugonjwa upo katika jamii yote.
Mtoto anavyolelewa tu ni tatizo, sasa unategemea huyu mtoto akija kuwa rais ataongoza nchi vizuri?
Mama ni chinjachinjaTofauti na yule, huyu mcha Mungu
Umemsikiliza Jenerali Ulimwengu?Tatizo karibu wote tunamuangalia rais kama ugonjwa, wakati rais ni dalili ya ugonjwa tu.
Ugonjwa upo katika jamii yote.
Mtoto anavyolelewa tu ni tatizo, sasa unategemea huyu mtoto akija kuwa rais ataongoza nchi vizuri?