Wazungu wanasema Tanzania rushwa imepungua Sana wakati wa Rais Samia kuliko ule wa Magufuli. Watanzania wanasema rushwa inaongezeka. Je, ipi ni ipi?

Wazungu wanasema Tanzania rushwa imepungua Sana wakati wa Rais Samia kuliko ule wa Magufuli. Watanzania wanasema rushwa inaongezeka. Je, ipi ni ipi?

Mwanahabari wa Taifa

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2020
Posts
1,588
Reaction score
956


Mkuu wa mkoa wa Simiyu Mhe David Kafulila akihojiwa na Ayo TV amekuwa na haya ya kusema juu ya kupungua kwa rushwa Tanzania kisayansi,Msikilize

Kafulila anasema,Ripoti ya kimataifa ya kupambana na rushwa inaonesha Tanzania tumetoka nafasi ya 94 mpaka 87 sawa na vietnam & Moroco kati ya nchi 180 zilizofanyiwa utafiti na taasisi ya kitaifa ya Transparency International kwa vigezo 180 na kuziacha nchi za Msumbiji 149, Uganda 142, Kenya 128, malawi110 na Zambia 117

Aidha,Taasisi inayojishughulisha na harakati za kusimamia uwazi na mapambano dhidi ya rushwa na Ufisadi duniani ya " Transparency International " tayari imetoa ripoti yake ya mwaka wa jana,

Taasisi hii iliyofanya kazi ya kuchunguza na kutafiti kiasi cha rushwa na Ufisadi kwenye nchi zipatazo 180 duniani kwa kutumia kipimo cha Corruption Perceptions Index ( CPI ) huku Tanzania nayo ikiwemo mwaka 2020'21.

Ripoti iliyotolewa na taasisi hiyo inayoheshimika zaidi duniani kwa kuwa na taarifa za kweli ya Transparency International inaonesha nchi ya Tanzania rushwa na Ufisadi vimepungua Sana wakati huu wa Rais Samia Suluhu Hassan ambaye ameachia uhuru wa kujieleza kwa wananchi wake,

Mtakumbuka Tanzania ilipata alama 36 kati ya alama 100 zilizotolewa na taasisi hiyo mwaka 2019'20 huku Tanzania tukishika nafasi ya 94 kati ya nchi 180 zilizochunguzwa mwaka huo,

Kwamujibu wa ripoti iliyotolewa mapema mwaka huu Tanzania imepanda kwa nafasi saba ( 7 ) toka ile ya 94/180 mwaka 2019'20 hadi kufikia nafasi ya 87/180 huku ikijizolea alama 39 kati ya alama 100 zilizotolewa,

Hongera Tanzania, Hongera Mama Samia Suluhu Hassan kwani huu ni ushindi mkubwa kwa Taifa,
 
Kuondoka kwa Rushwa hakujawahi kuwa kwa siku moja.

Sipingani na tafiti ila nachowezaa kusema ni kwamba.. Miundo mbinu na namna JPM alivyoendesha nchi matotokeo yake yanaweza kuwa ndio haya yanayosemwa leo.

Utawala wa Samia unaweza kuupima baada ya miaka miwili na kuendelea, kwa sasa watu bado wanamuwaza JPM watu waliotengenezwa na JPM bado wako kwenye mfumo.

Wacha tuone toleo la akina Nape na January itakuwaje baada ya miaka miwili.
 
Waulilze wanaposema RUSHWA wana maana gani? Pengine kwao maana ya rushwa ni ugumu wa kujikwapulia rasilimali zetu.

Which means, kupungua kwa rushwa-hakuna ugumu tena wa kuchota mali za wananchi, ubadhirifu, ufisadi, na madili.
 
Kuondoka kwa Rushwa hakujawahi kuwa kwa siku moja.

Sipingani na tafiti ila nachowezaa kusema ni kwamba.. Miundo mbinu na namna JPM alivyoendesha nchi matotokeo yake yanaweza kuwa ndio haya yanayosemwa leo.
Kuna mtu juzi kati hapa alijinyonga kwenye mkoa wa Kafulila kwa sababu ya kuombwa rushwa. Huo ni mfano hai.

Jamani acheni taarifa za makaratasi zinapotosha sana.

Kama rushwa ingekuwa imepunguwa, hali hiyo ingekuwa ^reflected kwenye maendeleo^~ in JPM's voice.
 
Mimi si mmoja wao lakini ninapinga. 🙂
Uliwahi kuombwa rushwa na ukatoa?

In fact saizi kesi za Wala rushwa ziko nyingi sana Mahakamani na wengine kila siku wanatumbuliwa..

Zama za Jiwe ilikuwa na kucomorokose kwa pesa..

Ni Rais Samia ndio aliwakemea polisi kupokea rushwa ila Mwendazake aliwaruhusu akisema ni vipesa vidogo.
 
Tanzania is a peaceful country in the world.
kamwe huwezi kuifananisha Tanzania na nchi yoyote kwa amani, utulivu na ukarimu.
 
Back
Top Bottom