WCB, Diamond na Rayvanny watozwa Tsh milioni 9 kutokana na maudhui mabovu ya wimbo 'Mwanza'

WCB, Diamond na Rayvanny watozwa Tsh milioni 9 kutokana na maudhui mabovu ya wimbo 'Mwanza'

Huyu Ngereza ameingia Mkenge kutoka kwa watu wanaoichukia WCB, sasa hivi kila Nyimbo ikitoka WCB, Kuna memba wanaanzisha uzi kuomba ufungiwe naona safari hii wamefanikiwa.. Kuanzi wimbo Rich Mavoko na Diamond, ukaja Haleluya, ukaja African beauty, ule kaimba na Rick Ross nk
 
Shika adabu yako tunazungumzia wimbo wa mwanza
Ishike adabu yako kwanza ,na sisi tutazishika zetu kunguru wewe, hivi slipomtaja amberruty kusema usije shikwa ukapelekwa central ..hapo anakemea au anahamasisha ,huo mtaro utafukuliwa wako maana una tabia zileee za konki konki
 
Download completed, saved.... Want to PLAY...? BASATA wacheshi tu acha wavune posho kiulaini.
 
Jaribu kuwa serious basi,akafanyie mziki nje ya nchi ? Angeweza tu kama mashairi yake pamoja na lugha ingekuwa inajulikana ,hivi unapoimba nyege,nyege ,nyegezi unakuwa unaimanisha nini?
anamaanisha Nyegezi
 
WCB , Diamond na Rayvanny wametozwa tsh milioni 9 kutokana na maudhui mabovu ya wimbo 'Mwanza'

BASATA imewatoza faini ya Tsh. Milioni 3 kila mmoja Mwanamuziki Diamond Platnumz, Mwanamuziki Rayvanny na Lebo nzima ya Wasafi Classic

Aidha, Wasanii hao wamepewa maelekezo wauondoe wimbo huo 'YouTube' vinginevyo wa mamlaka waliyonayo BASATA watafungiwa kufanya shughuli za sanaa

Vile vile BASATA imesisitiza kuwa mtu yeyote, kwa sehemu yoyote au chombo chochote kisiutumie wimbo huo kwa sababu haufai kwa matumizi yoyote yale
Basata wana njaa tu
 
Back
Top Bottom