Weka hapa Tiba asilia ulizowahi kutumia na zikakusaidia, mimi zangu hizi hapa

Weka hapa Tiba asilia ulizowahi kutumia na zikakusaidia, mimi zangu hizi hapa

Muhimu: Uzi huu hauhusishi matatizo ya nguvu za kiume, tayari kuna uzi wake maalum jukwaa la mapenzi

Huu ni uzi spesho wa mirejesho yetu tuliowahi kutumia tiba asili na zikatusaidia, yaani sisi ndio tuwe mashuhuda sio kukopi ma kupesti humu.

1. Nilikuwa nakula samaki ghafla kimfupa kikanikomea kwenye koo, nilijaribu kukohoa kwa nguvu lakini wapi, kuna rafiki yangu alikuwa mtu wa kanda ya ziwa akanipikia ugali mgumu, niliambiwa nipige tonge zile kubwa bila mboga yoyote, Tonge la kwanza tu mfupa ukateremka nikabaki nashangaa na nilimshukuru sana, nilikuwa nimepanga niende hospitali ila rafiki alinisaidia.

2. Funza kwenye kidole anaesababisha kidole kivimbe na maumivu makali, maumivu yalikuwa makali sana, nilienda hospitalini wakaniambia kucha itolewe, niliwaambia hakuna tatizo ntakuja, ulifikiri nilienda !! nikiwa natafta njia mbadala nikaambiwa na dada flan kaishi bush utotoni kwamba dawa ni kuvaa ndulele / turatura / ndura / nyanya pori, yaani unaichuma unaikata juu na chini iwe kama pete alafu unaivaa iishie ile sehemu yenye mdudu, ule utomvu ni sumu kwa mdudu yule, yaani ukiivaaa atahangaika sana mpaka afe ila nawe mda huo chamoto utakiona, akifa maumivu yanaisha na kidole kinakuwa na usaha, unakitoboa huhisi maumivu yoyote yale, unakamua usaha wote.

3. Kwikwi - hii dawa yake ni kunywa maji, ama upate uwoga mfano utishiwe umeiba kitu, kuna nyingine ni sugu sijajua wanatibu vipi.
Safi sana bonge la topic daah sijui uluwazaje mwamba kuja na hii ishu
 
Chukua karafuu kijiko 1 cha chakula. Chemsha kwa maji lita 1 kisha unakunywa kikombe kama cha kahawa 1 Kila SIKU kwa SIKU 7. Au mils 20 yaani vile vipimio vya dawa ya Maji ( Syrup) Viwili kutwa mara 1
Shukrani
ntarudi kwa mrejesho
 
Dawa hii alinieleza mentor wangu japo sijawahi itumia Kwa mtu.
Atafutwe nguruwe aliyezaa akamuliwa maziwa yake kidogo TU kama 10ml weka ktk kichupa .
Mnywaji wa pombe achanganyiwe matone kadhaa ktk bia au pombe anayoipenda sana, ikifanyika Kwa siri ni Bora zaidi.Kisha atakunywa na hii ni dozi ya maramoja ,once and forever.
Akirudia tena kunywa pombe huyo ni mwamba.
Atatapika nusu kufa?
 
Paka mavi ya ng'ombe yale mabichi yalitolewa na ng'ombe muda mfupi tu eneo husika kisha vaa kitu cha kuzuia kama kofia zile za kike lala asubuhi koga endelea na kazi zako utaona mabadiliko
Sema kweli mkuu? Hivi ni vile vya kuzaliwa au kipara chochote?
 
Hii dawa haina madhara kwenye mwili ila itaweza kukuletea msongo wa mawazo.

Anyway ukinywa hii dawa utafanya kitendo ambacho hutaamini wewe ndiyo ulifanya.

Madhalani, kuna mama mmoja ndugu alitamani kuona Mume wake anaacha pombe, aliinunua na kumpa mume wake, kilichotokea mumewe alitembea uchi wa mnyama toka bar mpaka nyumbani huku akisindikzwa na watoto wa mtaani.

Baada ya hapo kilichotokea ni historia, mzee alicha pombe na sasa anasali swala tano.
Mama mbavu zangu mie🤣😂😂😂
 
Anayejua dawa ya kuzuia damu kutoka puani
Sio tiba asilia
Kuna mtu nilishamuona ana shida ya damu puani akachoma hii

images-3.jpeg
 
Eucalyptus[Mlingoti haswa ule mweupe] - naitumia mara kwa mara kutibu kikohozi.

Unachemsha majani yake unapiga ⅓kikombe kutwa mara3.
 
Tumeric. Binzari. Manjano.
Inatibu kidonda
 
Nahitaji mtu anisadie ndugu yangu aiache pombe Jamani nisaidieni
Mchanganyie maziwa ya nguruwe kwenye pombe. Angalizo Hy pombe iwe bia na SI vinginevyo. Hakikisha umeandaa uji mwepesi wamoto... maana atatapika na kuharisha unaweza ukafikiri anakufa. Hiyo harufu atakayoisikia kwenye pombe🤣🤣🤣 Kila akigusa pombe atatapika hvy ataamua kuachana nayo tu.
 
Hii dawa haina madhara kwenye mwili ila itaweza kukuletea msongo wa mawazo.

Anyway ukinywa hii dawa utafanya kitendo ambacho hutaamini wewe ndiyo ulifanya.

Madhalani, kuna mama mmoja ndugu alitamani kuona Mume wake anaacha pombe, aliinunua na kumpa mume wake, kilichotokea mumewe alitembea uchi wa mnyama toka bar mpaka nyumbani huku akisindikzwa na watoto wa mtaani.

Baada ya hapo kilichotokea ni historia, mzee alicha pombe na sasa anasali swala tano.
Kuna jamaa mmoja wa mtaani kwetu akipiga adhana bar mke na ndugu wote wakamtenga, 🤣🤣🤣 sasa hv hataki kusikia pombe, nahisi alipewa Hy dawa
 
Back
Top Bottom