Wekeza Milioni 7 upate Milioni 20 ndani ya miezi 6

Wekeza Milioni 7 upate Milioni 20 ndani ya miezi 6

Nimenunua gunia 20 za debe sita kwa 6000@ natest zali ikinipendeza nitaendelea nayo mwakani
Matumizi yake
1 .gunia tupu 20=12000
2.usafiri 2000= 40000
3.mpunga gunia 20*36000= 720000
4. Gharama ndogo ndogo = 50000

JUMLA 822000
TUKUTANE JANUARY
Kwa hiyo hizi utazitunza hadi january mkuu ? Au utaongeza ?
Kadirio la faida litakuaje?
 
Salamaleko,

Shalom. Kama tunavojua kipindi hiki kwa maeneo ya vijijini ni kipindi cha kuvuna mazao na kuna niliko mimi kwa sasa debe la mahindi lina 7000 na debe la mpunga lina 5000. Maana yake gunia la debe sita la mpunga ni 30000. Na gunia la mahindi la debe sita linasoma 42,000.

Kama una mtaji wa kununua mpunga kwa kipindi cha mavuno basi una uhakika wa kuingiza mil 20 kwa mtaji wa mil 6 kwa muda wa miezi 5 (UHAKIKA)

MCHANGANUO
Gunia la mpunga 30,000 unanunua gunia 200 jumla inakuja 6,000,000 kwenye million 7 inakua imebaki million 1 kwa ajili ya kukava gharama za ukusanyaji na mambo mengine madogo madogo.

Huu tupo mwezi wa 5 ikifika mwezi wa 10/11/12 gunia la mpunga linafika 100,000l= kutoka 30k ya sasa.

Sasa una gunia 200 stoo zidisha 100,000 kwa kila gunia mzigo utasoma 20,000,000/= ukitoa mil 7 uliyowekeza UNABAKI NA 13,000,000/=KAMA FAIDA KWA MIEZI SITA (6) WOOW

NB: Ni bora kununua mpunga kuliko mahindi sababu mpunga hauna gharama sana kwenye kutunza kama mahindi

UKITAKA MALI UTAIPATA SHAMBANI UKU NILIKO KUNA FURSA NJOO TUWEKEZE

Ushauri maoni kurekebishana ruksa, nawakaribisha.
When the deal is too good think twice
 
Kuna makala moja aliandika Mh Kingwangala kuhusu biashara ya mpunga. Mh aliingizwa cha kike na mtu anaemuamini sana. Itafuteni mtakuja kunielewa

Kwa kifupi hii biashara sio rahisi km mtoa mada alivyosema
SI alikuwa anafanya kilimo cha kupiga simu
 
Kwenye mahindi usiweke pesa, watu wana mahindi ya mwaka jana walinunua kwa 800, saizi bei ni 550 mpk 500
That's business sometimes you fail sometimes you you have to accept don't worry to take risks next time failure is a part of success embrace it duu umepigaje hapo.
 
Kama una hela nunua mahindi kipindi hichi then hifadhi! Kwanzia Sep-Dec mahindi yataadimika na bei itakuwa juu!
 
Kama una hela nunua mahindi kipindi hichi then hifadhi! Kwanzia Sep-Dec mahindi yataadimika na bei itakuwa juu
 
Inawezikana kabisa mfano ipo mingi sana, Mwaka huu hiyo 7Milioni unaweza kupata 20+ Milioni ,
Mahindi Gunia Moja Leo ni Tshs 35000 , ukinunua Mahindi Gunia 200 za Mahindi unaweza kabisa kuuza mwezi Desimba Kwa Tsh Laki Moja na Zaidi Kwa Gunia Moja, Sababu kwanini Mahindi yatapanda Bei ni maljirani zetu wengi Wana njaa na ukame mwaka huu Zambia. , Malawi, Angola, Zimbabwe na Msumbiji Kwa Upande wa mikoa ya kusini magharibi na nyanda za juu kusini. Mahindi Yao yatavuka sana kwenda upande wa Zambia na Malawi Kwa Kasi.
Ruvuma Mahindi Yao yatavushwa sana kuingia Msumbiji na Malawi
Mahindi ya Kiteto, kondoa, Babati, mbulu na Karatu yayakwenda sana upande wa Kenya kupitia namanga ma Tarakea.
Piya mwaka huu wengi wa Mvua umeathiri sana kiimo Cha mahindi kwenye Mashamba ya kichanga na udongo mwepesi Mahindi ya metitia chini, kwenye maeneo ya mbuga na udongo wa mfinyazi ndio watavuna vizuri.
nunua wewe halafu wapelekee
 
Nimenunua gunia 20 za debe sita kwa 6000@ natest zali ikinipendeza nitaendelea nayo mwakani
Matumizi yake
1 .gunia tupu 20=12000
2.usafiri 2000= 40000
3.mpunga gunia 20*36000= 720000
4. Gharama ndogo ndogo = 50000

JUMLA 822000
TUKUTANE JANUARY
Mkuu tunaomba mrejesho
 
Kufikia July mchele utakuwa aukamatiki mwaka huu mvua chache sana kwa baadhi ya mikoa majaruba mengi hayana maji mpk sasa na gunia la mpunga mpaka sasa lina 70k sasa sijui mpka july itakuaje
 
Back
Top Bottom