MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, leo Ijumaa, Julai 20, 2018 inatarajiwa kutoa hukumu katika kesi ya dawa za kulevya inayomkabili muigizaji wa filamu nchini, Wema Sepetu na wenzake wawili.
Mrembo wa sinema za Kibongo, Wema Sepetu tayari amewasili katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar kwa ajili ya kusikiliza hukumu ya kesi ya matumizi ya madawa ya kulevya inayomkabili.
Hukumu ya kesi ya dawa za kulevya inayomkabili Mrembo na mwigizaji Wema Sepetu imeanza kusomwa na Hakimu Thomas Simba katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam muda huu.
=======
View attachment 813906
Msanii wa filamu ambae pia alikuwa Miss Tanzania 2006 Wema Sepetu amekutwa na hatia ya kukutwa na kutumia dawa za kulevya.
Ahukumiwa jela mwaka mmoja au kulipa faini ya milioni 2.
Washtakiwa wawili kwenye kesi hiyo ambao ni wafanyakazi wake wa ndani wameachiwa huru baada ya kukutwa hawana hatia
Habari zaidi, soma=>
Sakata la Madawa ya Kulevya: Wema Sepetu afikishwa Mahakamani, apata dhamana
Mkemia Mkuu: Mkojo wa Wema Sepetu ulikuwa na bangi
Wema amelipa faini, wakili wake, Msando amezungumza