Wanajamvi yapata kama Wiki mbili na sehemu sasa tangu nilivyoleta uzi wangu kuwataka kinadada waache kumsumbua Mungu kwa matatizo yao ya kujitakia.
mara baada ya uzi huo akaja Lara 1 a. k. a kubwa la maadui, jeshi la mtu mmoja, akanichamba ile mbaya, hakuishia hapo tu akaenda mbali zaidi kwa kumtukana hadi mama yangu,
Cha ajabu Wiki jana Lara 1 amerudi na kukaa upande wangu, anaunga mkono kile Nilichokuwa nawaasa mabinti, akimshauri wema ktk uzi wake Lara 1 anasisitiza kwa wema ajitunze hadi aolewe, asipagawishwe na kibibi kama zari aliyezaa na Diamond, anamsisitizia kuwa kuzaa bila ya kuwa kwenye ndoa ni nuksi, Lara 1, umeingia kwenye 18 zangu kiulainiiiiii........!