Wengi wanamkubali Bob Marley ila Mfalme wa Reggae duniani ni Lucky Dube

Wengi wanamkubali Bob Marley ila Mfalme wa Reggae duniani ni Lucky Dube

Keep on resting legend
Screenshot_20200511-200214~2.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
1. Paragraph ya kwanza tu unaonekana hujui mambo ya kidunia. Aliyeuwawa ni Lucky Dube (kwa risasi) Bob alikufa tu kawaida kwa kansa iliyoanzia kwenye kidole chake cha mguu.
2. Huwezi mlinganisha Lucky Dube na mkongwe Bob. Lucky anaimba na vinanda sana (huwa tunasema nyimbo zake ni kama kwaya) Bob anaimba ile "Roots Rocky Reggae" yenyewe.
3. Kasikilize nyimbo za Bob kama "Jah live" "Jump Nyabinghi" "Roots Rock Reggae" "Chant Down Babylon" "Them Belly Fully" "Bad card" "Concrete Jungle" "Kaya" najua kwa uelewa wako umeishia zile nyimbo common kama "No woman no cry" "Africa Unite" "Zimbabwe"
4. Fanya hayo hapo juu No. 3 halafu uje ufute huu uzi wako.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa jinsi alivyoandika anaonesha hajui kitu. Kasikiliza nyimbo za lucky akapata mzuka wakuanzisha uzi.
 
Dunia yote inamtukuza na kumuhusudu Bob Marley (Culture?) kama mfalme wa muziki rege, sijui wanatumia vigezo gani hasa. Wanamshusha na kumchukulia poa Lucky Dube sijui kwakua Bob aliuawa ndio wanakua na sympathy naye.

Kwa upande wangu japo Dube alimuheshimu Bob ila kwangu dube ndio mfalme wa muziki wa rege duniani. Nyimbo safi zenye ujumbe mwanana, beats zilizoenda shule performance za hadhi ya nyota 15 alizofanya! Nina uhakika Bob angekuwepo wakati Dube Anatoa Album zake 3 za mwanazo (hasa Slave) angempigia magoti Dube na kumsujudu kwa nyimbo bora alizotoa.

Huyu jamaa anajua hasa sikiliza nyimbo zake zote 80% lazima uzipende tu, ukutaka ujue ukali wa huyu mtu angalia Live performance zake utadata.

Najua mtanipinga humu na kunipopoa ila kwangu huyu ndio nishampitisha kua Mfalme wa Rege Duniani, hakuna mwingine.

Ninauhakika huko alipo kapumzika kwa amani maana katimiza kile kilichomleta duniani (Kuhamasisha watu waamke) japo alikua na mapungufu yake kama mtu yoyote yule ila naamini huyu mtu mbingu ni yake na tunaweza mwita mtakatifu kwa kazi yake nzuri.

Sikiliza hizi






Wewe vipi, huoni kwamba huo wimbo wa pili "Buffalo soldiers" ni wimbo wa Bob marley ambao Lucky Dube karudia kuimba??!!.

Hapo inaonyesha Bob Marley ndiye King of Reggae.
 
Baada ya kukaa Ujerumani kwa miezi akipewa matibabu kwa ajili ya Cancer, iligundulika kuwa hawezi kupona tena na ana muda mfupi tu wa kuishi. Kwahiyo Bob Marley aliamua arudi nyumbani, japo aione Jamaica 🇯🇲 kwa mara ya mwisho. Kwa bahati mbaya hakufanikiwa kufika. Akiwa njiani, siku kama ya leo, tarehe 11,mwezi wa 5,mwaka 1981, Bob aliaga Dunia, Miami, Florida.

Muda mfupi kabla ya kifo chake, Bob Marley alipokea Order of Merit by the government of Jamaica. He had also been awarded Medal of Peace from United Nations 1980.

Mazishi ya Bob Marley yalikuwa ya kihistoria. Alizikwa na umati wa watu 30,000 kutoka pande zote za Dunia.
 
Dube anaimba nyimbo zenye hisia sana na ni rahisi kuzielewa, Bob anaimba nyimbo zenye hisia sana ila nyingi zina ugumu flani katika kueleweka( zina ufalsafa Fulani ndani yake). Nani mkali zaidi ya mwingine!? Sijui ila kila mtu anachagua flavour anayopenda!

Sent using Jamii Forums mobile app
Nani mkali zaidi ya mwingine mkiwa kwenu Sigimbi ndio mnaulizana hivyo,
Lakini dunia nzima inamtambua Bob Marley.

Ukiona huelewi falsafa ya Bob haikufanyi umu underrate, huyo Dube amekua influenced na kina Bob na Tosh enzi hizo anaimba kwaya kabla hajahamia kwenye Reggae.

Boost your Immune System to fight a Covid-19.
 
Haitoshi lazima aelekezwe ukweli, uwezi kumfananisha Dube na Marley kila mtu aliwika kwa zama zake na kila mtu ana vibes zake Bob ni mkubwa na Lucky ni mkubwa pia wote walifanya kazi nzuri kwenye ulimwengu wa reggae,
Lucky aliinogesha reggae na vionjo vya Africa, nampenda zaidi Dube ila ukweli Bob Marley ndo Mfalme wa reggae worldwid.

Sent using Jamii Forums mobile app

We ndio unajua. Lucky Dube mwenyewe alimheshimu na kuwathamini Bob na Toshi, niliwahi kumsikiliza akifanya mahojiano akasema Peter Tosh ndio alumpa hamasa ya kuima Reggae wakati huo alikua akiimba Mbakanfa yenye asili ya ki afrika kusini.

Bob anabaki kuwa mfalme kwa vile ni kama muasis wa reggae, hiyo haitafutika hata atokee mwingine hawezipata hiyo heshima ila atathaminiwa na kutambuliwa kazi yake.

Binafsi, namwelewa sana Dube.
 
Sio kama simpendi Lucky Dube ila muziki wake nilianza kuupotezea pale alipohusishwa na kifo cha Senzo

"Cᵒᵃᶜᵏʳᵒᵃᶜʰ ⁿᵘʰ ᵇᵘˢˢⁱⁿᵉˢˢ ⁱⁿⁿᵃ ᶠᵒʷˡ ᶠⁱᵍʰT"

Unahabari kwamba Senzo yupo hai na hiyo habari haina ukweli wowote?
 
Kwa mtu anae fahamu mziki wa reggae ni aibu kumllinganisha Bob Marley na Lucky Dube yaani ni sawa kumfananisha Franco na Fally Ipupa ni mlima na kichuguu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sjawai ona reggae ya lucky dube ni orijino hata sku1 ,,naonaga ni kama nyimbo za kwaya,..yaan hana tofaut na waimba bongo fleva wa bongo wanaojidai wanaimba RnB..hiv RnB wanaijua,hyo waachie kina Usher,rkely na chris brown

Sasa ndo lucky dube,yaan kabisa unafananisha regae ya jamieka na ya africa...

We lazima ni mchaga tuu
Mkuu umeua

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa hiyo hapo nimemu underrate Bob au siyo!?
Nani mkali zaidi ya mwingine mkiwa kwenu Sigimbi ndio mnaulizana hivyo,
Lakini dunia nzima inamtambua Bob Marley.

Ukiona huelewi falsafa ya Bob haikufanyi umu underrate, huyo Dube amekua influenced na kina Bob na Tosh enzi hizo anaimba kwaya kabla hajahamia kwenye Reggae.

Boost your Immune System to fight a Covid-19.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa mtu anae fahamu mziki wa reggae ni aibu kumllinganisha Bob Marley na Lucky Dube yaani ni sawa kumfananisha Franco na Fally Ipupa ni mlima na kichuguu.

Sent using Jamii Forums mobile app

Reggae ipo ya aina tofautitofauti kama ilivyomiziki mingine.

Kwakuwa hii ni ishu ya burudani kila mmoja ana preference zake, mwingine anavutiwa na Bob mwingine anapenda kusikiliza nyimbo za Lucky Dube. Hauwezi kulazimisha kila anaesikiliza Reggae amsikilize au kuvutiwa na nyimbo za Bob.

Hauwezi kusema Lucky Dube hakuimba reggae wakati hadi mauti inamfika ulimwengu na dunia kwa ujumla inamtambua kama mwanamziki wa kimataifa wa Reggae. Ntakubaliana na wewe reggae zao zipo tofauri lakini sio kweli kwamba Lucky Dube hakuimba Reggae.
 
Umenikumbusha kuna wajinga flan wakataka kuanzisha propaganda eti Taylor Swift ni mkali kuliko Michael Jackson hahahaha kizazi cha dotcom kina wazimu sana,

Hawajui kuheshimu michango ya waliowatangulia,
Pathetic.

Boost your Immune System to fight a Covid-19.
 
Wabongo wajuaji sana!
Reggae ipo ya aina tofautitofauti kama ilivyomiziki mingine.

Kwakuwa hii ni ishu ya burudani kila mmoja ana preference zake, mwingine anavutiwa na Bob mwingine anapenda kusikiliza nyimbo za Lucky Dube. Hauwezi kulazimisha kila anaesikiliza Reggae amsikilize au kuvutiwa na nyimbo za Bob.

Hauwezi kusema Lucky Dube hakuimba reggae wakati hadi mauti inamfika ulimwengu na dunia kwa ujumla inamtambua kama mwanamziki wa kimataifa wa Reggae. Ntakubaliana na wewe reggae zao zipo tofauri lakini sio kweli kwamba Lucky Dube hakuimba Reggae.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umenikumbusha kuna wajinga flan wakataka kuanzisha propaganda eti Taylor Swift ni mkali kuliko Michael Jackson hahahaha kizazi cha dotcom kina wazimu sana,

Hawajui kuheshimu michango ya waliowatangulia,
Pathetic.

Boost your Immune System to fight a Covid-19.
kwahiyo hoja hapa inakuwa kutangulia sio!!!
 
Reggae ipo ya aina tofautitofauti kama ilivyomiziki mingine.

Kwakuwa hii ni ishu ya burudani kila mmoja ana preference zake, mwingine anavutiwa na Bob mwingine anapenda kusikiliza nyimbo za Lucky Dube. Hauwezi kulazimisha kila anaesikiliza Reggae amsikilize au kuvutiwa na nyimbo za Bob.

Hauwezi kusema Lucky Dube hakuimba reggae wakati hadi mauti inamfika ulimwengu na dunia kwa ujumla inamtambua kama mwanamziki wa kimataifa wa Reggae. Ntakubaliana na wewe reggae zao zipo tofauri lakini sio kweli kwamba Lucky Dube hakuimba Reggae.


Mkuu hii topic inadai mfalme wa Reggae Duniani ni Lucky Dube, au hujailewa?
 
Mkuu hii topic inadai mfalme wa Reggae Duniani ni Lucky Dube, au hujailewa?

Nimeielewa sana, nilikua namjibu mhusika niliyemnukuu.

Kuhusu Luck Dube kuwa mfalme wa reggae ngumu. Ni sawa na mchezaji aibuke leo mcheza soka useme huyo ndio mfalme wa soka kumpiku Pelle. Yaani kuna ile heshima anapewa mtu kwa kazi aliyoifanya.

Lucky Dube alikua vizuri sana tu kwa eneo lake ila mfalme wa reggae anabaki kuwa Bob.

Unafikiri akitokea kiongozi wa kutolewa mfano leo akafanya maajabu ataitwa Baba wa taifa? Hiyo ni heshima ya Mwl. Nyerere tu, haitafutika kamwe.

Naamini umenielewa mkuu.
 
Back
Top Bottom