Wenye tatizo la usikuvu hafifu kama langu tukutane hapa kupeana faraja

Wenye tatizo la usikuvu hafifu kama langu tukutane hapa kupeana faraja

Mimi nilikuwa na tatizo la kutosikia, na niliwah kupita hapa kweny ID nyingine kuomba msaada.
Nilizunguka hospitali zote bila kufanikiwa, jibu la madaktari ilikuwa hawaoni tatzo.

Kwa neema ya Mungu nili bahati kuja kuishi Marekani.
nikaenda hospitali kuona kama naweza kupona.

daktari wakuu aliniunganisha na watu waonahusiana na masikio.

Daktari wa sikio alinichukua vipimo na baada ya vipomo alisema ndani ya sikio kuna shimo ndo zinafanya husikie. na akaniambia sikio la kwanza nina 80% ya kupona na nyingine 70%. alinipa siku ya kufanya upasuaji sikio la kwanza. nilienda hospitali na alifanya yake. ukweli sikio lilirudi katika hali ya kusikia.

Nikapewa tarehe ya kurudia sikio la pili, now miaka miwili sijarudi kwa daktar. nimeridhika na hili moja linasikia vizuri maana sijawah kuitwa kiziwi kama zamani.

Daktari aliwahi kuniuliza, hao madaktari wa africa walikuwa wanakuambie?. nikamjibu walisema hawaoni tatizo. ila nikamwambia naisi ni ukosefu wa vifaa kama hvi ninavyoviona hapa.

Kutosikia sio kitu kizuri, kinapunguza hata hujasiri
 
pole sana Mweneyzi Mungu akuwekee wepesi ....umejaribu dawa za asili pia??
 
Ili uwe huru ukiwa unasemeshwa kitu na husikii,mwambie huyo anayekusemesha kuwa,'sisikii vizuri tafadhali ongeza sauti',nimeshazoea na wala sioni aibu sasa hivi,ingawa mwanzoni ilinipa shida sana.Changanya na maombi sana mkuu,hakuna kitu ambacho Mungu anashindwa,mimi sasa hivi hali yangu ni kama inaimarika zaidi,na ninajipa tumaini iko siku Mungu ataniponya na nitaleta mrejesho humu ndani.....
Nami nafanya ivyo namwambia kabisa mtu nina shida ya kusikia kuanzia mwanzo wa maongezi ingawa siwezi kufanya ivyo kama matangazo kwa kila mtu mwingine naishia kumsikiliza tu basi natabasamu, kutikisa kichwa au kuonesha tu sapoti yoyote ingawa sometimes nakuwa sijamwelewa alichosema especially kama tupo sehemu yenye makelele
 
Umesema sawa mkuu nikimsikiliza mtu akiongea kwenye simu au vyombo vya sauti yaani spika kutoka kwenye redio, tv au kompyuta ule ile sauti naisikia ila haiji katika mpangilio wa kuweza kuelewa mtu kasema nini ila tukiwa karibu tunaelewana shida mtu akiwa mbali, ana kigugumizi au sauti ikiwa inatoka kupitia spika mfano mic, simu, redio, tv, kompyuta n.k kuhusu maumivu ya kiuno, ganzi n.k izo dalili sina
Hyo ni tinittus mkuu usihangaike mama angu mdogo anayo since mdogo mpaka sana ana miaka 40 na kitu kashazoea kwa vile mwanamke ila nae kuongea pia kapoteza uwezo sio kwamba hajui ila anamua tu kuwa kama bubu ila anashikia sometime anaishi kawaida tu ...usijipe shida mpaka watu hwaoni wanaishi huenda one day unaweza kurudi.

Ili tatizo Linaweza kutokea katika hali flani za kushtua ubongo pia,..Linaweza sbabishwa na hata homa kali haswa malaria ,hata vile vidonge vya quinine pia zinahusika kingine saikolojia mawazo sana kichwani kupelekea kuathiri ubongo.

Ila achana na hawa watu coz asilimia ya watu wengi weny tatizo hilo ni vichwa la unabisha fuatilia yaani darasani wako vizuri so Kuna myth kwamba wanarogwa achana nazo .
 
Mimi nilikuwa na tatizo la kutosikia, na niliwah kupita hapa kweny ID nyingine kuomba msaada.
Nilizunguka hospitali zote bila kufanikiwa, jibu la madaktari ilikuwa hawaoni tatzo.

Kwa neema ya Mungu nili bahati kuja kuishi Marekani.
nikaenda hospitali kuona kama naweza kupona.

daktari wakuu aliniunganisha na watu waonahusiana na masikio.

Daktari wa sikio alinichukua vipimo na baada ya vipomo alisema ndani ya sikio kuna shimo ndo zinafanya husikie. na akaniambia sikio la kwanza nina 80% ya kupona na nyingine 70%. alinipa siku ya kufanya upasuaji sikio la kwanza. nilienda hospitali na alifanya yake. ukweli sikio lilirudi katika hali ya kusikia.

Nikapewa tarehe ya kurudia sikio la pili, now miaka miwili sijarudi kwa daktar. nimeridhika na hili moja linasikia vizuri maana sijawah kuitwa kiziwi kama zamani.

Daktari aliwahi kuniuliza, hao madaktari wa africa walikuwa wanakuambie?. nikamjibu walisema hawaoni tatizo. ila nikamwambia naisi ni ukosefu wa vifaa kama hvi ninavyoviona hapa.

Kutosikia sio kitu kizuri, kinapunguza hata hujasiri
Safi sana
 
Mimi nilikuwa na tatizo la kutosikia, na niliwah kupita hapa kweny ID nyingine kuomba msaada.
Nilizunguka hospitali zote bila kufanikiwa, jibu la madaktari ilikuwa hawaoni tatzo.

Kwa neema ya Mungu nili bahati kuja kuishi Marekani.
nikaenda hospitali kuona kama naweza kupona.

daktari wakuu aliniunganisha na watu waonahusiana na masikio.

Daktari wa sikio alinichukua vipimo na baada ya vipomo alisema ndani ya sikio kuna shimo ndo zinafanya husikie. na akaniambia sikio la kwanza nina 80% ya kupona na nyingine 70%. alinipa siku ya kufanya upasuaji sikio la kwanza. nilienda hospitali na alifanya yake. ukweli sikio lilirudi katika hali ya kusikia.

Nikapewa tarehe ya kurudia sikio la pili, now miaka miwili sijarudi kwa daktar. nimeridhika na hili moja linasikia vizuri maana sijawah kuitwa kiziwi kama zamani.

Daktari aliwahi kuniuliza, hao madaktari wa africa walikuwa wanakuambie?. nikamjibu walisema hawaoni tatizo. ila nikamwambia naisi ni ukosefu wa vifaa kama hvi ninavyoviona hapa.

Kutosikia sio kitu kizuri, kinapunguza hata hujasiri
Naomba mawasiliano au jina la iyo clinic mkuu.. who knows labda siku moja nami nitapata msaada niweze kufika uko
 
Hyo ni tinittus mkuu usihangaike mama angu mdogo anayo since mdogo mpaka sana ana miaka 40 na kitu kashazoea kwa vile mwanamke ila nae kuongea pia kapoteza uwezo sio kwamba hajui ila anamua tu kuwa kama bubu ila anashikia sometime anaishi kawaida tu ...usijipe shida mpaka watu hwaoni wanaishi huenda one day unaweza kurudi.

Ili tatizo Linaweza kutokea katika hali flani za kushtua ubongo pia,..Linaweza sbabishwa na hata homa kali haswa malaria ,hata vile vidonge vya quinine pia zinahusika kingine saikolojia mawazo sana kichwani kupelekea kuathiri ubongo.

Ila achana na hawa watu coz asilimia ya watu wengi weny tatizo hilo ni vichwa la unabisha fuatilia yaani darasani wako vizuri so Kuna myth kwamba wanarogwa achana nazo .
Unaongea mambo mengi yanayonigusa moja kwa moja, mimi pia primary nilikua vizuri class nishawahi kupiga interview pale feza nikaperfom vizuri ila bi mkubwa akakataa kusoma pale maana braza angu niliefanya nae interview yeye alifeli wakamkataa na bi mkubwa anataka wote tusome shule moja nakumbuka yule mwalimu mkuu enzi izo alikua mzungu mtu wa ujerumani akampa bi mkubwa mpaka ofa ya punguzo la ada nisome pale feza ya mikocheni ila bi mkubwa akachomoa msimamo wake tusome shule moja na bro., primary nimesoma miaka mitano tu maana madarasa mengine nilikua nalukishwa sababu ya uwezo mkubwa class, nakumbuka mtihani wa taifa s.t.d 7 somo hesabu nilipata 49/50 siku naenda kutembelea shule niliyomaliza std 7 mwalimu mkuu akawa ananitania kama ananichapa kwanini niliiacha iyo moja iliyobaki. kuhusu story za kulogwa nishawahi kuambiwa uenda watu wamenichezea kualibu future yangu ila ni vile siamini kabisa hayo mambo ya ulozi
 
Pole sana,kutana na ma specialists wa ENT,ungekua Dodoma,ungeenda pale Benjamin Mkapa,ukutane Dr.Mkinga au Bukano,wakufanyie intensive examination ya masikio,you never know,unaweza ukapona.
Pole Sana,once again.
 
Mimi ni kijana wa kiume umri miaka 30 kwa sasa naishi iringa mjini, nimeondoka dar february baada ya kula sana msoto nikaamua ngoja niende sehemu ambayo hakuna anaenijua nipate utulivu wa akili, hapa iringa nimepewa hifadhi ya kulala tu na ndugu.

Twende kwenye main topic sasa, nina tatizo la kushindwa kusikia vizuri, nishazunguka kwenye hospitali nyingi sana tangu mwaka 2007 ambapo nilianza kuhisi tatizo. Mara ya mwisho nilsaidiwa pesa na jirani yetu wakati nipo Dar nikaenda hospitali ya CCBRT miaka kama minne hivi imepita baada ya vipimo waliniambia ngoma ya masikio haina tatizo, tatizo ni mishipa na hata nikifanya operation haitasaidia chochote.

Nikapewa dawa za kumeza asubuhi, mchana na jioni kwa miezi mitafu nikimaliza dozi nirudi hospital baada ya kumaliza dozi na kurudi hapakua na maendeleo yoyote, nikaambiwa suluhisho pekee ni kuvaa earing device ambazo ni gharama na zina risk kuongeza tatizo na kupelekea kuwa kiziwi kabisa basi nikaachana na mpango wa earing device na mambo ya kuwenda hospital maana nishaibgia gharama nyingi bila mafanikio, nikakubaliana na hali yangu, ndio mtihani wangu huo hapa duniani

Shule ya msingi nilimaliza nikiwa sawa kabisa nikafaulu kwa daraja A na kupangiwa kwenda Azania secondary. Wakati nikiwa form 1 mama angu alifariki nikawa yatima rasmi (maana baba alifariki nikiwa na mwaka mmoja tu hata kumbukumbu ya sura yake sina nimeoneshwa picha zake tu). Kwa kweli ugumu wa maisha niiyoishi kutokea kifo cha mama mimi mwenyewe ndo nayajua naomba nisiandike maana nitaitaji kujaza kitabu kizima.

Kuanzia kifo cha nikawa nasomeshwa kwa msaada wa baadhi ya ndugu na majirani, nilipofika around form 3 hivi ndo nikaanza kuhisi utofauti kwenye suala la kusikia napata shida kumsikia mtu akiongea kwa sauti ya chini, mtu mwenye kigugumizi, mtu akiongea akiwa mbali na kuongea na mtu kwa simu ndo simwelewi kabisa.

Kwa kweli shule ilikua chungu nikaanza utoro hata kujumuika na wanafunzi wenzangu ilikua shida darasani nikashuka sana form 4 sikufanya vzr. Nikasoma certificate, diploma na bachelor degree, ila najilaumu sana kupoteza huo muda kusoma chuo.

Ningeweza kurudisha muda nyuma ningesoma masomo ambayo yanaendana na hali yangu mfano uandishi maana nipo passionate sana na kuandika au ubunifu wa mavazi. Maana watu wananisifia sana najua kuchagua nguo nzuri kuna wengine huwa wananipa hela nikawanunulie au niwasindikize dukani kuwasaidia kuchagua au ningesomea ufundi.

Ila nikasoma masomo ya biashara ingawa ufaulu wangu wa chuo ni mzuri ila ni vigumu kupata ajira au kujiajiri. Maana mambo ya selling, marketing, uhasibu, customer care na ku-organize shughuli zote za biashara kwa kiasi kikubwa yanahitaji kuonana na watu kuwasiliana nao, presentation, seminars n.k.

Kwenye kutafuta kazi ni kisanga embu fikiria ugumu wa kupata ajira sasa ongeza na tatizo la kusikia vizuri ni balaa na nusu. Fursa nyingi sana zinanipita ni mwaka wa 6 sasa tangu nimalize chuo sijawahi kupata ajira yoyote, napigiwa simu za kuitwa kwenye interview siwezi kuongea na kuelewana na mtu kwenye simu, nikijaribu kujibu ujumbe kwa kuweka wazi nina changamoto ya kusikia waajiri wanaona nafanya ujanja janja tu wananijibu tu "asante" na mchakato unakua umeishia hapo.

Mbaya zaidi sina connection kwenye familia na ndugu wa karibu hakuna ambae anashikilia kitengo kizuri au mfanyabiashara mkubwa kidogo kusema anaweza akaniingiza kwenye mishe zake, nimepambana sana kutafuta mtu wa kunisaidia nimewafata watu mpaka sebureni kwao kuwaomba na kuwaambia nipo tayari kufanya kazi bure kama akihitaji kujiridhisha na uwezo wangu lakini nimeambulia patupu. Ni kama miaka 6 ya kusoma chuo kuanzia certicate nimepoteza muda na kuingia gharama tu, kwa sasa bado nipo mtaani sina mbele wala nyuma ingawa ufaulu wangu nilioupata chuo ni mzuri tu.

Ushauri wangu kwa wenye tatizo kama langu usikate tamaa, potezea dhiaka unazofanyiwa na watu, jikubali, pale unapokutana na mtu ambae haujuani nae jieleze kwamba una changamoto ya kusikia usione noma, chagua marafiki wachache ambao wanaelewa hali yako na pia jishughulishe au somea mambo ambayo yanaendana na changamoto inayokukabili yaani hauonani sana na watu na kufanya mazungumzo nao mfano uhandishi, ufundi, ubunifu n.k.

Lifestyle yangu kwa kiasi kikubwa ni ya upweke, sio mtu wa kuchangamana na watu kampani yangu kubwa ni kwenye vibanda umiza nikienda kuangalia mpira (story za ucheshi, majigambo na utani wa kishabiki vibandani angalao nasahau kwa muda matatizo yangu) hakuna kipindi chochote cha kwenye tv ninachokifatilia maana sisikii vizuri wanachoongea, nikiangalia tv ni mpira na movie zenye english subtitle tu, kuwasiliana na watu kwenye simu ni kwa sms tu, dharau, dhiaka, kupuuzwa, kuonekana mtu mwenye malingo kwa kutoitikia salamu au nikiongeleshwa alafu sijasikia ni changamoto ambazo nakutana nazo sana kwa ambao hawanijui na baadhi wananijua ila wanataka kunifanyia bullying tu mbele za watu.

Tusikate tamaa ndugu zangu kikubwa wote tupo hai
Pole sana kaka,
Hiyo shida inanisumbua pia,
Najikuta confidence inapungua saana, na upweke kwa wingi, lakini nashukuru Mungu amenipa akili sana, performance yangu ni nzuri. Ila masikio bado ni changamoto kwangu nimeenda kwa wataalam MNH, wameniambia hakuna dawa, wakasema ninunue hearing devices,
Sijazinunua napambana na hali yangu.
Usife moyo haupo peke yako.
 
Pole kijana na mimi nina tatizo kama lako ila mimi sikio langu moja halisikii vizuri

Nilianza primary kutosikia vizuri ila nilikomaa na kitabu nikafaulu shule ya serikali nakufaulu mtihani wa seminari
Nikapiga kitabu nikaenda A level shule nzuri ya serikali nikaenda chuo

Nikaingia mtaani nikaa miaka mitatu natafuta ajira naomba ajira hata siitwi kwenye interview private wala utumishi

Baadaye nikazidisha maombi sana nakuombewa nakaomba ajira tena utumishi nikaitwa ya kwanza NHC Duke dar nikafanya written nikadunda


Nikaitwa ingine tena ya pili ya utumishi nikafanya nikafaulu sasa hivi nipo Dodoma wizarani hapa napiga kazi naishi watu vizuri tu wala hawanibagui

Jaribu utumishi Mkuu Ajira unaweza kupata
Hakikisha unakuwa mtu wamaombi sana sana Mkuu

Kikubwa usikate tamaa hata majaribu yawe makubwa

Mwenyezi Mungu akubariki sana sana Mkuu
 
Hyo ni tinittus mkuu usihangaike mama angu mdogo anayo since mdogo mpaka sana ana miaka 40 na kitu kashazoea kwa vile mwanamke ila nae kuongea pia kapoteza uwezo sio kwamba hajui ila anamua tu kuwa kama bubu ila anashikia sometime anaishi kawaida tu ...usijipe shida mpaka watu hwaoni wanaishi huenda one day unaweza kurudi.

Ili tatizo Linaweza kutokea katika hali flani za kushtua ubongo pia,..Linaweza sbabishwa na hata homa kali haswa malaria ,hata vile vidonge vya quinine pia zinahusika kingine saikolojia mawazo sana kichwani kupelekea kuathiri ubongo.

Ila achana na hawa watu coz asilimia ya watu wengi weny tatizo hilo ni vichwa la unabisha fuatilia yaani darasani wako vizuri so Kuna myth kwamba wanarogwa achana nazo .
Hii ni kweli kaka,
Akili ipo active sana,
Nashukuru Mungu nilifanikiwa kupata shule ya vipaji maalum. Ijapokuwa nipo na hili tatizo.
 
Back
Top Bottom