Wenye uzoefu na biashara ya mkataba kwa bodaboda na bajaji naomba mnielimishe

Wenye uzoefu na biashara ya mkataba kwa bodaboda na bajaji naomba mnielimishe

Gharama anazopaswa kuingia mmiliki ni zipi,marejesho yanapaswa kuwa vipi?Changamoto zake ni zipi?Faida zake zinakuwaje hasa "mambo" yakienda vizuri!!Matatizo ya kutarajia ni yapi?Aina nzuri za bodaboda ni zipi?Mkataba unakuwaje?Kimsingi sijawahifanya biashara hii,ninataka tu "niwasaidie" vijana wawili walionifuata na kuniomba msaada kwani uchumi umeyumba kwetu sote!Kila mtu na "siri" yake!
Naomba sample ya mkataba pls

Sent from my TECNO BC1 using JamiiForums mobile app
 
nani amekuambia nyumba haina risk?

Likipita tetemeko?kama je ulijenga kimakosa mradi wa serkali unapita na hawalipi fidia?ikiwaka moto na huna bima?

Shoti ya umeme
 
nani amekuambia nyumba haina risk?

Likipita tetemeko?kama je ulijenga kimakosa mradi wa serkali unapita na hawalipi fidia?ikiwaka moto na huna bima?

Kuungua Gesi
 
Mkataba wa bajaji wenyewe unakuaje wakuu kama boda boda ni mwaka bajaji je?
 
Bajaji inaweza kuwa na nafuu kidogo kuliko boda hasa kama utapata dogo anaejua kutunza chombo na kutafuta maokoto. Ila ukiifanya wewe mwenyewe ndio inakuwa bingo zaidi.
 
Gharama anazopaswa kuingia mmiliki ni zipi, marejesho yanapaswa kuwa vipi? Changamoto zake ni zipi? Faida zake zinakuwaje hasa "mambo" yakienda vizuri. Matatizo ya kutarajia ni yapi?

Aina nzuri za bodaboda ni zipi? Mkataba unakuwaje? Kimsingi sijawahifanya biashara hii, ninataka tu "niwasaidie" vijana wawili walionifuata na kuniomba msaada kwani uchumi umeyumba kwetu sote!

Kila mtu na "siri" yake!
Kwa pikipiki mpya boxer 150 mkataba ni miezi 16 kila siku lazima atoe 10000

Kwa pikipiki kama kinglion mpya mkataba ni miezi 14 kila siku lazima atoe 10000


Gharama za service na matengenezo ni juu yake.

Mara nyingi nimeona mkataba wa asipotoa hiyo hela kwa mfululizo wa siku 15, basi una haki ya kuchukua chombo chako
 
Bajaji inaweza kuwa na nafuu kidogo kuliko boda hasa kama utapata dogo anaejua kutunza chombo na kutafuta maokoto. Ila ukiifanya wewe mwenyewe ndio inakuwa bingo zbajaji nayo Ina

Bajaji inaweza kuwa na nafuu kidogo kuliko boda hasa kama utapata dogo anaejua kutunza chombo na kutafuta maokoto. Ila ukiifanya wewe mwenyewe ndio inakuwa bingo zaidi.
Vip kwa upande wa muda yaani ikifika miezi mingapi namuachia bajaji au hilli la muda limekaaje kwa upande wa bajaji
 
Mimi naona Biashara ya mkataba ni kichaa

Biashara pasua kichwa hiyo ni sawa na kujaza maji kwenye tenga.
Ipo hivi pikipiki aina ya boxer inauzwa mil 2.8, hesabu ya siku unaletewa elfu 10 na mkataba kwa kawaida ni miezi 13..ukiwa unaletewa kila siku elfu 10 kwa mwezi utakuwa umeingiza laki 3,laki 3*13=3900000
3900000-2800000=1100000
Faida kwa mwaka mzima unapata mil 1.1
1100000÷13=84615...

Unatoa mil 2.8 mfukoni halafu kwa mwezi faida unaingiza elfu 84615 kama sio utahaira ni nini? Na hapo ukiigawanya kwa siku ni kama unaingiza 2800.

Sasa kwa mtaji milioni 3 kasoro sio sahihi kuingiza 3000 kwa siku. Huku mama muuza mihogo anaingiza zaidi ya hiyo kwa mtaji chini ya elfu 30.

Na hapo hapo mwisho wa mwaka piki piki inakuwa sio yako.. mtaji wote umekwisha

NB: Hapo bado haujapewa taarifa ya kuibiwa pikipiki, service ikiwa kubwa ni juu ya boss
Daaah! umechanganua vema.
 
Mimi naona Biashara ya mkataba ni kichaa

Biashara pasua kichwa hiyo ni sawa na kujaza maji kwenye tenga.
Ipo hivi pikipiki aina ya boxer inauzwa mil 2.8, hesabu ya siku unaletewa elfu 10 na mkataba kwa kawaida ni miezi 13..ukiwa unaletewa kila siku elfu 10 kwa mwezi utakuwa umeingiza laki 3,laki 3*13=3900000
3900000-2800000=1100000
Faida kwa mwaka mzima unapata mil 1.1
1100000÷13=84615...

Unatoa mil 2.8 mfukoni halafu kwa mwezi faida unaingiza elfu 84615 kama sio utahaira ni nini? Na hapo ukiigawanya kwa siku ni kama unaingiza 2800.

Sasa kwa mtaji milioni 3 kasoro sio sahihi kuingiza 3000 kwa siku. Huku mama muuza mihogo anaingiza zaidi ya hiyo kwa mtaji chini ya elfu 30.

Na hapo hapo mwisho wa mwaka piki piki inakuwa sio yako.. mtaji wote umekwisha

NB: Hapo bado haujapewa taarifa ya kuibiwa pikipiki, service ikiwa kubwa ni juu ya boss
Daaah! umechanganua vema.
 
Gharama anazopaswa kuingia mmiliki ni zipi, marejesho yanapaswa kuwa vipi? Changamoto zake ni zipi? Faida zake zinakuwaje hasa "mambo" yakienda vizuri. Matatizo ya kutarajia ni yapi?

Aina nzuri za bodaboda ni zipi? Mkataba unakuwaje? Kimsingi sijawahifanya biashara hii, ninataka tu "niwasaidie" vijana wawili walionifuata na kuniomba msaada kwani uchumi umeyumba kwetu sote!

Kila mtu na "siri" yake!
Kwa uzoefu wangu hii ni biashara kichaa.
1. Inamnufaisha zaidi dereva. Dereva anapiga hesabu ya pesa yake halafu ndio anaanza kutafuta ya boss
2. Haikui maana baada ya mwaka pikipiki sio yako tena
3. Haina security. Pikipiki ikiibiwa biashara imekufa maana kumdai bodaboda ni wazi hatoweza kukulipa na wala hana mali yoyote ya kukamata dhamana.
Kama utaendesha mwenyewe sawa ila kumpa bodaboda utakula hasara tu. Pesa ya kununua boxer ni bora utafute chimbo ambalo magari yanapita pita ufungue carwash
 
Mimi naona Biashara ya mkataba ni kichaa

Biashara pasua kichwa hiyo ni sawa na kujaza maji kwenye tenga.
Ipo hivi pikipiki aina ya boxer inauzwa mil 2.8, hesabu ya siku unaletewa elfu 10 na mkataba kwa kawaida ni miezi 13..ukiwa unaletewa kila siku elfu 10 kwa mwezi utakuwa umeingiza laki 3,laki 3*13=3900000
3900000-2800000=1100000
Faida kwa mwaka mzima unapata mil 1.1
1100000÷13=84615...

Unatoa mil 2.8 mfukoni halafu kwa mwezi faida unaingiza elfu 84615 kama sio utahaira ni nini? Na hapo ukiigawanya kwa siku ni kama unaingiza 2800.

Sasa kwa mtaji milioni 3 kasoro sio sahihi kuingiza 3000 kwa siku. Huku mama muuza mihogo anaingiza zaidi ya hiyo kwa mtaji chini ya elfu 30.

Na hapo hapo mwisho wa mwaka piki piki inakuwa sio yako.. mtaji wote umekwisha

NB: Hapo bado haujapewa taarifa ya kuibiwa pikipiki, service ikiwa kubwa ni juu ya boss
Hili jambo nilikua nawaza saana, ila sasa mbona kila leo Biashara inazidi kushika Kazi.
 
Binafsi hii biashara ya boda mwaka 2016- 2019 nilikua nazo 10 kati ya hzo 6 zilimaliza salama 4 zikaibwa kiufup ni biashara kichaa umasikini jiran yako
 
Back
Top Bottom