Wenye uzoefu wa kuishi kwa ndugu nipeni muongozo

Wenye uzoefu wa kuishi kwa ndugu nipeni muongozo

Palina

JF-Expert Member
Joined
Oct 9, 2021
Posts
3,551
Reaction score
9,522
Binafsi mwezi huu wa tatu hivi karibuni nilisafiri kwenda mkoa X ila ni ndani ndani mpakani na Msumbiji huku.

Kwakuwa ni kwa kaka yangu sikua na mashaka kwenda, bro ameshaoa tayari na pia ana watoto wawili sema anaeishi ni mmoja mwingine yupo kwa shangazi (yaani bibi)

Haya wiki ya kwanza picha linaanza sijui ilitokeaje dogo akavunja miwani yangu ni glasses alidondosha chini, nikamwambia bro akanizungushaa nikasema nitalimaliza mimi mwenyewe.

Sijakaa kidogo USB ya chaja imekatika ila nijua moja kwa moja dogo kaikata ni mtundu mno hili nalo niliongea nae akanizungusha.

Tangu nije hapa yaani ni ugali kwa kwenda mbele😞😞 ni almost wiki ya pili hii labda pasaka MUNGU asaidie niuone wali walau kwa mbaali.

Yaan huyu mama wa hapa najiuliza sijui ana ugomvi na mimi maana tangia nije hata kupika anataka nipike mimi, nikichat kosa anamwambia bro mi nachat tu eti sifanyi kazi ilihali namsaidiaga

Wenye uzoefu hii familia naishije nayo au nirudi tu kwetu


==========UPDATE===========



Hatimaye.. MUNGU kajaalia nimeweza kurudi home safetly. Nilichojifunza ni kuwa heri mtu afikie lodge ila si kwa ndugu (haiko applied kwa wote)



Asanteni nyote kwa encouraging words



Paubae.
 
Back
Top Bottom