Wenzetu mmewezaje kuvunja 'cycle' ya umasikini wa ukoo/familia?

Jinsi ya kuutokomeza umaskini ni kuhakikisha wanafamilia wameenda shule na kupata elimu ya kutosha. Watu wakiwa na elimu wanaweza pambana angalau wakaweza kujimudu hata kama sio kuwa matajiri. Mzazi ahakikishe kwa namna yoyote ile mtoto apende shule. Binafsi nimesoma shule za serikali mwanzo mwisho. Mzee wangu alikuwa ananijaza sana matumaini.. yaani alikuwa ananijaza upepo nikienda shule hata bila pocket money najiona niko sawa na kuamini baba atatuma. Ile spirit niliyojazwa na mzee wangu ikanifanya niwashike wadogo mkono kwenye ishu za shule. Kwa sasa familia nzima imefika chuo kikuu na angalau kila mtu anajishughulisha.

Mbinu yangu ya elimu inaweza isifanye kazi pia kama wanafamilia hawana nidhamu. Familia iliyokosa maadili hata wawe na akili za darasani wanaweza bado wakaendelea kuwa maskini. Wanafamilia wanatakiwa kuheshimiana na kuishi kama timu. Sio mmoja ajione bora zaidi.
 
Sio kwamba koo ina laana no tatizo start up na unakua unafanya hustling bila back up yoyote hivyo kua ngumu mno kutoboa
Hizo familiar zinaitwa advanced marginalized communities. Yaani shida zote huko zipoo. Tatizo Linalosababisha hili ni social inequality. Gepu limekuwa KUBWA MNO Kati ya tajiri na maskini limekuwa kubwa Sana. Kwa kadri Gepu lilivyokuwa kubwa ndivyo hizo familia zinakutana na shida nganganga, na hivyo hivyo familia za kitajiri haijui kule bondeni Kwa maskini shida nini, mbona watu wamelala fofofo.
 
Umesomea UCHAWA wa Mama, eeh?
 
Kuna familia unaenda unakuta baba ni mfanyabiashara mama mtumishi watoto maengeneer wengine madaktari, hiyo yote ni misingi bora waliojiwekea wazazi katika kutengeneza koo bora.

Na kuna familia zingine unakuta wazazi wana uwezo wa kawaida tu lakini ukiangalia watoto wapo juu kiuchumi na wengine wana elimu kubwa.

Baba kuwa maskini haimzuii kutengeneza ukoo bora cha muhimu ni kuwa na future na familia yako.
 
Jua kwamba matatizo mengi ya kifamilia ni ya kijenetic mengine ni ya kimazingira na mengine ni ya kimalezi na mengine ni ya kiroho. Yote haya yaweza kutengeneza mzunguko usio na mwisho (vicious cycle) ambapo ni ngumu kutoka.

Chunguza vizuri kujua nini chanzo cha kushindwa kwa familia au ukoo wenu, halafu chukua hatua stahiki.
 

Sie kwetu kila siku tunalalamikaga MAISHA MAGUMU [emoji18]
 
Kazia
 
Mkuu mimi na kupinga umasikini ni man made hauna uhusiano wowote na uumbaji au kiroho, hayo yote ni visingizio vya wale walioshinda kupambanua udhaifu wao na kuishia kumsingizia Mungu.......wa kuristo wa kimißsionary ndo walioanzisha hiyo theory ya kusema umasikini unatoka kwa Mungu, na masikini amebarikiwa kwake ataenda mbinguni, hizo kauli zilitumiwa na hao watu ili exploit mali za waafrika na kutengeneza utii kwa wafasi wao masikini, we can fight and eradicate poverty.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…