Wewe dada na kaka Mungu awabariki sana

ALPARSLAN

JF-Expert Member
Joined
Aug 27, 2024
Posts
467
Reaction score
1,181
Mnamo September 6 niliandika Uzi uliohusu Hali ya biashara yangu kukosa wateja, nilipokea maoni mbalimbali kwenye Uzi na PM pia (Nawashukuruni nyote kwa maoni yenu na ushauri )
Miongoni mwa PM nilizopokea ni za huyu dada (sitopenda kumtaja) dada huyu yupo Kigamboni

Alinifuata PM akanambia kama sitojari niende Kigamboni siku ya weekend tuweze kuonana huenda nitaongeza kitu chanya kwenye biashara yangu

Kiukweli nafsi ilinisuta nikasema usije kuwa mtego pia mtu mwenyewe licha ya kuonekana ni mcheshi kwenye comment na nyuzi zake hapa jf ila pia anaonekana ni mtu ambae masihala ni mengi na anapenda sana ushari hasa pale mtu akimkwaza

Kwanza sikujua kama ni ID ya kike licha ya kunambia yeye ni Ke ila sikujiridhisha kabisa 100%
Ila niliamua kumcheki jamaa yangu na kumwambia anisindikize kwa ajili ya usalama wangu.

Jamaa alikubali na akanisindikiza mpaka Kigamboni nilivofika nikamcheki PM akawa yupo offline maana hakutaka kunipa no ya simu basi nikavuta subra hatimaye akawa amenijibu na kunambia atafika hapo feri muda si mrefu hivo anikute NMB ATM ya feri.

Baada ya dakika kama 20 nikaona Toyata Rush ikipaki nje ya ATM mwanaume akashusha kioo cha gari huku akiwa anatuangalia sisi maana tulionekana kuzubaa akamwambia mwenzake ambaye ni huyu dada "bila shaka ni hawa"

Dada mzuri mrefu mweupeee alikuwa amevaa miwani na ushungi akashuka kwenye gari na kuniita Alparsalan maana nilikuwa nimemkazia macho kweli nikaitika akasema ni wewe nkamwambia ndio akasema upo na huyo akimnyooseha kidole jamaa alonisindikiza nkamwambia ndio akasema kama hamtojali ingieni kwenye gari tuondoke.

Nilisita kidogo ila jamaa yangu akasema twende tu tukaingia kwenye gari

Nitaendelea kuhadithia baadae nisiwachoshe
 
Uzi wenyewe ni huu👇
 
Nipoishia.....
Nilisita kidogo ila jamaa yangu akasema twende tu tukaingia kwenye gari..... Endelea 👇

Tulivoingia kwenye gari mume wa huyo dada akashuka na yeye akaelekea ATM Akadraw hela wakati huo huyo dada anaoengea na simu dada alivomaliza kuongea na simu wakawa wanateta jambo na mume wake Kisha wakaigia ndani ya gari.

Wese likakanyagwa na mume Wa huyo dada kimya kimya hakuna mtu anayeongea huku roho ikinidunda najiuliza naenda wapi Mimi je huko ninakoenda ni salama? Baada ya dakika kama 10 gari ikasimama mbele ya geti la nyumba dada akasema shukeni tukashuka. Mume wa huyo dada akateta jambo na mkewe Kisha akaingiza gari ndani na kumwambia huyo dada asikawie huko anakoenda.

Hapo roho ikawa Umetulia kidogo maana tukaanza kutembea kwa miguu kuelekea sehemu tulipofika hiyo sehemu ilionekana kuchangamka saana yani Kuna biashara za tumbo za Kila aina basi tukaingia kwenye kibanda Fulani cha chipsi huyo dada akasema
"Alparsalan Mimi sio mkaaji ila huyu kaka (muuza chipsi na kuku) nimeshaongea nae Kila kitu atakupa ABCD za kuboresha biashara yako usiwe na hofu upo sehemu salama usisite kunitafuta PM ukishamalizana nae au kama utaweza kupakumbuka nyumbani utaningongea mimi nipo mpaka Jioni" Kumbuka ilikuwa kama saa 7 mchana basi yeye akawa ameondoka

Nitaendelea, nimechoka kuandika
 
Nimecheka hapo alipo ita ALPARSALAN 😊

KWAIO
WENYE WAJINA KAMA inamankusweke , mjingamimi ,
mshamba_hachekwi , Nikifa MkeWangu Asiolewe , Mjanja M1 , mwendazake-ndago kwa uchache
 
Nilipoishia...
"Alparsalan Mimi sio mkaaji ila huyu kaka (muuza chipsi na kuku) nimeshaongea nae Kila kitu atakupa ABCD za kuboresha biashara Yako usiwe na hofu upo sehemu salama usisite kunitafuta PM ukishamalizana nae au kama utaweza kupakumbuka nyumbani utaningongea mm nipo mpaka Jioni" Kumbuka ilikuwa kama saa 7 mchana basi yeye akawa ameondoka

Alivyoondoka huyo jamaa muuza chips akawa amenihoji hoji lengo ilikuwa kunifahamu vizuri basi tukawa tumeongea mambo mengi ya kuboresha huduma ya biashara hasa biashara za tumbo hasa hii ninayoifanya akawa amenipa ABDD"s za kutosha nikisema niziseme hapa ntawachosha

Wakati huo akiwa ananipa ABC'S wateja wakamiminika akasema ngoja nimpigie wife aje hapa akufundishe jambo
Na kweli wife ake alipigiwa simu na baada ya dakika kama 20 alifika
Alivofika akamwambia mume wake (muuza chips)
"Baba Fulani Mimi kwa hapa siwezi labda twende nyumbani Fulani Yuko peke ake nyumbani na nimemuacha kalala"
Basi huyo jamaa akasema niongozane na wife yake nyumbani maana yeye ana wateja
Kiukweli nilichoka hata jamaa alonisindikiza alisema amechoka pia na mizunguko ila nkamwambia tukaze tu
Basi tulifika kwa huyo jamaa muuza chips tukaka nje


Bila kupoteza muda mke WA muuza chips akanambia enhee mliishia wapi?
Skumuelewa kabisa nkasema sjakuelewa dada akasema Hilo Somo la pilipili na kachumbari mmeishia wapi

Ndo nkamjibu tulikuwa Bado hatujaanza
Basi bila kupoteza akanifundisha namna ya kutengeneza kachumbari tamu na pilipili
Baada ya hapo akaniuliza kama nimemuelewa nikamjibu ndio
Akasema nakupa ingredients ufanye kwa vitendo
Akanipa ingredients nikaandaa pilipili ilivyopoa tukaionja ilikuwa tamu Kweli kweli
Akasema kama umeelewa basi mm nshamaliza Rudi kwa Mume wangu (muuza chips) kama mtakumbuka njia Tunasema hatuwezi kumbuka njia hivyo akatupa mtoto atupeleke mpaka pale kwajama muuza chipsi tulivofika muuza chips akaniuliza kama somo limeniingia nkasema ndio nikamuonjesha kasema wow umemsidi na mwalimu tukacheka kweli
Basi muda huo ilikuwa viazi vimeisha vijana wake WA kazi ndo walikuwa ndo kwanza wanamenya hivyo hakuwa na wateja
Aliamaua kutusundikiza kuelekea kwa hyu dada alonikutanisha nawe wakati tukiwa njiani akasema nimesahau kukuuliza unakaa kigamboni maeneo gani
Nkamwambia Mimi sikai huku Mimi nakaa buguruni akastaaju akasema alijua nakaa huku kigamboni nkamwambia hapana!
Akanambia buguruni alishawahi fanyi baisahara yake hii ila baada ya kuoa alihama nado akaja kigamboni akaniuliza sehemu ninayo fanyia biashara nkamtajia akasema hapo napajua ila kwa aina ya biashra Yako utachelewa kutoka Maana hapana mzunguko Sana basi tukafika Mpaka kwa huyo dada tukaagana na huyo dada dada akatupa buku 5 ya nauli tukasepa

Itaendelea...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…