What are random interesting facts about yourself?

What are random interesting facts about yourself?

Ex Convict
( harshly sentencing with viboko na vitu vingine siwezi sema nilivyoingia for almost five to four years )


Apathy


No family background or information


Kind /always smiling/funny


Former Philanthropist


Not serious


I love liquor
(Nowadays sio tena sana )


Napenda kutukana
 
Am an acrophobic.

Nikakaa hata ghorofa ya pili barazani, au nikachungulia dirishani nahisi kuna kitu kinanivuta chini hatari sana.

Kingine I always feel sad whenever I have to do something unpleasant even if necessary.
 
Naogopa sana kumuomba meanaume hela, 12 years of marriage sikumbuki siku ambayo niliwahi hata kuomba hela ya chumvi, huwa najisikia aibu kuomba hela, siku zote huwa nahakikisha naweka enough balance in case hata kama Hubby akiwa hana maisha yanaendelea bila kuomba na familia inadonga mbele

Gladly mume wangu anajua weakness yangu na he always give without asking na kama hana we do discuss the way foward na tunasonga mbele bila hiyana
 
Mimi sasa ndo balaa....

Sina rafiki sababu kubwa ni uwezo wangu wa kujua hisia za mwingine plus nimesoma vitabu vingi (1000+)kiasi kwamba najua kutofautisha fake people na really.

Sina rafiki sababu wote nimewakopa wamepotezea kunilipa,nkijaribu kumzoea mtu ananikopa hanilipi si mdai urafiki unakufa saivi sizoei mtu sababu nimestuka. More than 7 million ipo kwa marafiki zangu ambayo saivi sio marafiki tena ni watu wakupiga nao story tu.

Nina depression sometimes sababu najua vitu vingi sana kupita uwezo wangu wa kuvibeba na nafeel almost kila kitu.

Nahitaji mda wakukaa mwenyewe na siwezi kukaa na mtu yeyote duniani kwa mda mrefu.Nikitoka sehemu zenye kelele lazima nikae mwenyewe kwa mda.

Nina roho nzuri sana ingawa na improve kdg kuwa na roho mbaya.


Sipendi kelele na kila nachokisikiliza lzm nikipende kwanza,hivyo radio sisikilizi unless mada naipenda au mziki naupenda.

Siwezi kuwa mnafiki hivyo siwezi kujikomba kwa maboss.

Naongeaga ukweli ht pasipostahili hivyo kuna watu wananipemda sana kuna watu wananichukia sana

Napenda comedy movies sana bila hizo napata shida kubalance mood changes zangu

Na huruma sana ila na hasira za karibu kama Mtu hanielewi au ana mdharau mwingine

I can’t handle stress bahati mbaya sana nipo kama sponchi navyonza hisia za wengine haraka sana ziwe mbaya ziwe nzuri.


Namjua mtu kiundani sana kipaji chake ,uwezo wake ,udhaifu wake mda mchache sana nikiwa nae karibu.

Na uwezo wa kupiga story na mtu yeyote bila kujali status yake kwa kiwango kile kile cha heshima,mada nyingi nazijua hivyo sikosagi cha kuongea na mtu.

Shy kidogo,very spiritual but sipendi kwenda kanisani naona kama kupoteza mda hivi ila naamini nalindwa na nguvu kubwa sana ya kiMungu

MapenZi ya kugandana siyawezi naogopa sana mahusiano,napenda kulala mwenyewe,Nikiwa mwenyewe nakuwa na furaha zaidi ingawa najichanganya sana sometimes.

Napenda sana kucheka

Sina rafiki but i am friend material [emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji2][emoji2]

Uwaga nahisi sijaumbwa kuwa dunia hii huku kama nimepachikwa Tu.

Uwaga nahisi nimebarikiwa ila sijui hasa nimebarikiwa na nini ila najua nimebarikiwa sana kupita wengine.
 
Ngoja na mimi niandike.
Tangu darasa la 3 hadi la 5 nilikuwa "monitor".
Darasa la sita na la saba nilikuwa " Dada mkuu".

Form 1 na form 2 nilikuwa "Monitress" .
Form 3 nikawa kiongozi wa michezo na Monitress.
Form 4 nikawa kiongozi wa chakula na Monitress.

Five na six nilikuwa mweka hazina wa kikundi chetu cha dini.

Chuo nilikuwa CR miaka yote na Mbunge mwaka wa pili.

Kazini Mimi ni mwalimu wa nidhamu.
Born to be a leader, ukiweza achana na chaki uingie siasani. Huko uongozi+uongo unakula pesa za wananchi bure kabisa.
 
Huwa nafuatilia tabia ya mwanafunzi hadi mtaani na kwenye instagram[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]. Mbona wanakoma. Vikao vya wazazi kila leo mpaka mtoto abadilike. Na nikiamua kula sahani moja na wewe nitaacha tuu endapo utabadilika.

Form 4 wa miaka kadhaa nyuma walinikatia jina.
Sikuwahi kulijua hadi siku ya mahafali yao. Wakati walimu wanaitwa mimi zamu yangu MC akanitaja jina langu, masomo ninayofundisha akamalizia kwa kusema "wengi wanamjua kama ...." Wanafunzi wakalitaja wote kwa pamoja. Nilicheka sana.

Sema wanafunzi wananipenda. Hadi wazazi wao wananipenda na simu wananipigia kunishitakia tabia za watoto wao na awards wameshanipa mbili.
skuli tulizosoma sisi, ungekua hapo, ungeilaani kazi ya ualimu maana hata headmaster tuliwahi kumtia kipondo.
 
Natamani ningeandika kwa ID nyingine.

Sijipendi, sioni sababu yakuishi. Sifurahii maisha na sijui ni kwa nini. Sina maisha mazuri ila ninakula na kulala kwangu na siombi cha mtu.
Ukiniona huwezijua kama moyo wangu umepondeka kwasababu ninadress smart, ninacheka inapobidi (sio sana), ninachangamka nikiamua.

Sina hofu ya aina yoyote kwenye maisha yangu.

Sijisikii tena kuchase ndoto zangu.

Tangu nipo shule ya msingi nimekua nikijaribu kujiua ila nashindwa. Sijui kama ngao ya maji ilikua haiui ila nikiwa darasa la sita nilikunywa ngao na sikufa wala sikuumwa tumbo. Vingine siwezi kuandika. Jaribio lamwisho la kujiua nililifanya nikiwa form six. Halikufanikiwa

Mwaka jana nilipata kazi serikalini, msimamizi mkuu wa ngazi ya wilaya akanitishia kunifuta kazi kwa sababu zisizo za msingi, nikamwambia "me nimeshaifuta hiyo kazi kichwani, kazi kwako".

Mwaka huu mkurugenzi wa mamlaka niliyopo kwa muda alikuja kiukaguzi akaongea maneno machafu sana, akatusimangia watu chai ya ofisi nikamwambia mkuu ni chai ya rangi na chapati mbili kama unaona tunafaidi sana sema tukuagizie kuliko kuitolea macho ukidhani ni chai zenu za makao makuu.

Sijui kama mtoa mada alitaka haya au mengine, nowadays nina mashaka hata na uelewa wangu.
If you ever need help, open up.

JF itakuponya.
 
Nimeshindwa kukasirika kabisa japo sicheki cheki hovyo, huu ni ugonjwa nimeambiwa na wengi Sana, nahisi nina gene za amani sipendi violence ya aina yeyote



Sent using Jamii Forums mobile app
 
skuli tulizosoma sisi, ungekua hapo, ungeilaani kazi ya ualimu maana hata headmaster tuliwahi kumtia kipondo.
Wanafunzi wa siku hizi ni wadogo sana. Kipindi chetu tulikuwa wakubwa umri na miili.
Watoto wa siku hizi hawana hizo akili za kupiga.
 
Born to be a leader, ukiweza achana na chaki uingie siasani. Huko uongozi+uongo unakula pesa za wananchi bure kabisa.
Jukwaa la siasa lenyewe nikienda naona mapicha picha tu. Siasa nitaziweza kweli???
 
Sijui jina langu la ukoo na wala kabila langu.
Sijawahi fika Dar ila sijawah ishi kijijini.
Sijawahi kuwa na dem wala mchumba japo natongozwa some time.
Sina maajabu yoyote .
 
Sijui jina langu la ukoo na wala kabila langu.
Sijawahi fika Dar ila sijawah ishi kijijini.
Sijawahi kuwa na dem wala mchumba japo natongozwa some time.
Sina maajabu yoyote .
Wewe Ni bikra?
 
Back
Top Bottom