Whistleblower: Kashfa nzito suala la sukari, wamo vigogo wazito

Kwa andiko hili heshima ya JF inarudi kabisa. Hongera Sana Mkuu. Well researched.
 
Halafu kuna wapiga jaramba eti watajwa wawili hapo eti ni presidential material.
 
Huwa najiuliza tu kama kwa 1B mtu mzima wa umri wa miaka 40 tu anaweza kula maisha ya kawaida tu kula kulala mpaka akafa na still pengine akaiacha chenchi ya hio pesa kwa watoto.

Je, inakuwaje mtumishi anadokoa labda billion 20 na still bado ana tamaa tena ya mahela zaidi? Huyo mtu ikumbukwe analipiwa almost kila kitu na ofisi anapofanyia kazi!

Hayo mahela unaiba sijui billion 100 kesho tena unadokoa billion 50 hivi mahela yote huwa wanafanyia kitu gani? Au ndio wanajengea mahoteli labda!

Imagine umedokoa billion 100 tu inaweza kuwalisha familia yako na ukoo mzima mpaka mkapukutika kama hamuifuji! Na still pesa mtaiacha! Yani imagine kila mtoto aingiziwe 10B tu anaweza ikamsomesha mpaka akaoa na kulea familia na still pesa anayo tu.

Mi najiuliza kwa haya maisha dah unaiba trilion nzima na bado huriziki wakati expectancy ni miaka 60 tu kibongo bongo😂
 
 
mateso mnayoyapata wastaafu yanasababishwa na hawa viongozi vibaka, poleni wastaafu wa NSSF na watanzania kwa ujumla
 
Bagamoyo sugar nadhani Magufuli ana share kubwa sana.
 
sijajua Majaliwa anapata wapi guts za kuwaita watu wezi na kuwafukuza kazi.Mungu anakuona Majaliwa
 
Mama umefika wakati kumtimua Majaliwa ukweli unaosasa kama tiss alikuambia hukuamini sasa umesikia source ingine.....Kazi kwako achana na udini huyo kitu get muweke Makamba PM na Waziri Nishati hapo hapo....IGP amechoka na Mabeyo umri unaenda sasa 65 imetosha
 
we ngdere bdio haueleweki au umetumwa na hao mafisadi au unahusika. Uzi uko very clear
 
Sisi wananchi tuliichagua CCM ili ituongoze kumbe kuna mambo machafu sana yanayotendwa na Watendaji wake. Hapa Mwanza bei ya sukari ni Tshs.3,000. Mungu isaidie nchi hii inaelekea pabaya.
 

..na TANROADS kuhusika ktk ununuzi wa mitano ya kiwanda imekuwaje?

..kuna dokoment inayohusu manunuzi ya mitambo ya sukari ililetwa JF ina saini za wakubwa wa Tanroads.
 
Katafute na wewe ushahidi wako utuwekee humu acha kusumbua watu..
Mwenye macho haambiwi soma
Nani asiyejua nchi inavyoibiwa miaka nenda rudi cha kukushangaza hapa ni nini eti weka ushahidi?
 
Ukisoma andiko hili kisha ukaenda site kuona yanayoendelea kuna vitu utagundua haviko sawa. Kwa tuliobahatika kufika Dakawa,tumeshuhudia ujenzi wa kiwanda ukiendelea. Gharama zote za mradi inasemekana hazizidi 250billions. Hizo billion 500 zinazotajwa na mwandishi zinatoka wapi??
 
Katafute na wewe ushahidi wako utuwekee humu acha kusumbua watu..
Mwenye macho haambiwi soma
Nani asiyejua nchi inavyoibiwa miaka nenda rudi cha kukushangaza hapa ni nini eti weka ushahidi?
Pole, Mkuu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…